Picha ya Mwigulu Nchemba na Mwanae yazua mjadala mitandaoni

Mkuu ulibahatika kumsikia Mwigulu wakati akitangaza nia? hii jamani ni kuwa betray watanzania kwasababu wakati watoto wao wakisoma shule ambazo wewe unaziita St. Kayumba wao wanasomesha watoto International school hauoni kuwa hili ni tabaka???.. Hivi unafikiria waziri huyu anaesomesha watoto huko atakuwa na uchungu na watoto wa wanyonge??? hebu jaribu kuufahamu uzalendo kwa maana na vitendo maana huyu ni kiongozi anatakiwa a lead by example
Kwani UZALENDO una maana gani??????
Kutumia bidhaa au huduma za ndani ya nchi/haijalishi zina ubora ama la?
Okey, ampeleke kijana wake St Kayumba, je huko St Kayumba vifaa vyote watumiavyo kwa kutoa elimu vinatengenezwa nchini? Lakini pia hizo fedha atakazozi-save baada ya kutompeleka kijana wake shule za gharama atazitumiaje tumuone ni MZALENDO??? je akizitumia kwa kuongeza mjengo mwingine wa maana wenye thamani kutoka ulaya au kuagiza gari nyingine toka Ulaya, hapo ndio atakuwa MZALENDO?????

UZALENDO ni nini sasa????

Mimi nadhani picture hii ukiitafsiri kwa lugha ya KIZALENDO sidhani kama tutapata majibu zaidi ya kuwa perplexed tu, viongozi wengi tu nchi hii na hata Africa kwa ujumla baadhi ya ngazi za elimu yao wameipatia ULAYA kwenye elimu bora huko Mf Nyerere n.k na bado waliweza kuziletea nchi zao manufaa (Je kutotumia huduma ya elimu ya ndani hawakuwa wazalendo ???, lakini hii huduma nzuri ya elimu waliyoipata nje ya nchi zao ndio imewafanya/wawezesha wafanye mambo makubwa katika nchi zao)

Kwa mfano huyo kijana wake akamaliza hapo na matokeo mazuri (kwa sababu shule ni nzuri) yatakayomuweza kuwa admitted katika prestigious universties ambako atapata elimu bora kisha kuja kuajiriwa na serikali, akaitumia elimu na ujuzi wake vizuri kuwatumikia wananchi wa Taifa la Tanzania, je hatokuwa MZALENDO??

UZALENDO ni nini sasa!!!??
 
Watoto Wa Mbowe chekechea wanasoma ulaya wakati chadema ambacho kinadai ni chama kikuu cha upinzani hakina hata ofisi/ pango lao pale ufipa utafikili ni bafu

Ndo maana nasema uzalendo ni kazi. Wote hao hawafai kuongoza ni basi tu. Kiongozi ni kama Nyerere, Castro brothers, Nasser, Mao, Sankara, Lee Kwan yu, Che guevara, Lumumba, Pancho Villa, Ayatollah Khamenei. Wasome hao na Maisha yao ndo utapata maana ya kiongozi.

Kiongozi anatakiwa awe kama Mtumishi, Lakini hawa wakwetu wakipata tu uongozi wanawaza matumbo yao na familia zao.

Hakuna kazi ngumu kama uongozi.

Anyway, nasikia mkuu wa kaya wakwake wanasoma ST. KAYUMBA. CONGRATS MAGU.
 
View attachment 321828
Picha ya Waziri wa Kilimo na Mifugo na Mbunge wa Iramba Mashariki imezua "hisia" tofauti na mijadala mitandaoni.Picha hiyo inamuonyesha Mh.Mwigulu akiwa na mwanae wa kiume,na "Caption" ya picha inayosomeka elimuniufunguo. Kikubwa kilichozua mjadala ni nembo katika fulana ya mtoto yenye maandishi ya FEZA SCHOOL.

Maswali na mijadala ya wengi ni kuwa,itakuwaje na moyo wa kuimarisha elimu ktk shule za umma kama sehemu ya mawaziri ambao ni watekelezaji wa sera ya Elimubure na Uboreshwaji wa elimu katika shule za umma wanakimbiza watoto wao katika shule binafsi? Kwanini Mawaziri ambao ni sehemu ya utekelezaji wa sera wanaoamini katika elimu bora katika shule za umma wao hawawapeleki watoto wao huko?

Picha hii imezua mijadala tofautitofauti na wapo wanoona Mh.Mwigulu yupo sahihi kupeleka watoto shule binafsi sababu ukweli ni kuwa shule za serikali elimu yao ni duni na isiyo na ushindani.

Hivyo mawaziri kuwapeleka watoto shule binafsi na zenye ubora kama FEZA SCHOOL ni kuwaepusha na elimu duni inayotolewa na serikali
KWA KWELI KWA SASA SHULE ZA SERIKALI NI ZA MASKINI
 
Achen wivu wa kijinga, kama pesa anayo kwann asimpeleke mtoto wake akapate elimu bora, hakuna mtu yoyote aliekatazwa kumpeleka mtoto wake kwenye shule hizo. Wivu tu na uswahil mwing ndio mnachojua
sijui kama uko na Elimu ya juu.na kama unayo ni ya mlungi Dvs 5
swissme
 
Tatizo ni pale wanapozisifia shule za serikali watoto wao hawasomi huko kama zingekua bora kwa nini wasiwasomeshe huko wao?,uzalendo ni zaidi ya kuvaa tai na skafu za rangi ya bendera ya taifa.
Huyo ndiye mwigulu
 
Hata ningekua mm Wazir siwez mpeleka sehem nisiyo na uhakika nayo,,,Risk kumpeleka mtoto shule za bure
 
Kwa hoja zako ,ina maana serekali imedandia hoja ya elim bure kwa Mbele,binafsi nilienda nilienda shulen nikamuliza mkuu wa shule kuwa tutengeneze utaratibu wa watoto wale tuchangie ,mahindi na maharagebkama zaman ,shule ya msingi kasema pia ni mchango hauruhusiwi ni marufuku ,ila ninachoona hakuna elimu bure bali mateso kwa watoto maskin kwa kisingizio cha elimu bure,babarosa leteni fedha ya chakula shulen ,hutaona nalalamika,leten mdawati wekeni walinzi...mtoto hawez faulu akishinda njas hata kama mwalim anafundisha usiku na mchana...na kufaulu mtoto anaye kaa chini ni nfoto pia



Wewe Hauna Akili!
 
...maigizo yanaendelea
Wakiwa bungeni wanavokamia kuongea utazani kweli wana uchungu, hahaha, !!
 
image-jpeg.321828


DNA inamhusu Mh...
 
Back
Top Bottom