Picha: Ramani ya Mkoa wa Simiyu kiafya

Picha: Ramani ya Mkoa wa Simiyu kiafya

John John Msakuzi

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2025
Posts
279
Reaction score
99
1755256359775.png

Akiongea na wanahabari, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Anamringi Macha, amesema kuwa katika kipindi cha mwaka 2020 hadi 2025, Mkoa wa Simiyu umepokea jumla ya Shilingi Bilioni 69.75 kwa sekta ya afya, ikiwemo Shilingi Bilioni 26.80 kwa miradi ya afya, Shilingi Bilioni 10.96 kwa vifaa tiba na Shilingi Bilioni 31.99 kwa dawa. Zahanati zimeongezeka kutoka 190 hadi 242, vituo vya afya kutoka 10 hadi 21, na nyumba za watumishi kutoka 175 hadi 252.

Bajeti ya dawa na vifaa tiba imeongezeka kutoka Bilioni 4.9 hadi 8.2, huku upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi ukipanda kutoka asilimia 45 hadi 93. Magari ya wagonjwa yameongezeka kutoka 5 hadi 15, magari ya usimamizi kutoka 5 hadi 13, na watumishi wa kada ya afya kutoka 1,723 hadi 2,168 (ongezeko la 25%).

Serikali imekamilisha ujenzi wa Hospitali za Wilaya za Bariadi, Itilima na Busega, ukarabati wa hospitali kongwe 3 (Bariadi Mji, Maswa, Meatu), majengo 2 ya wagonjwa mahututi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa na Meatu, na majengo 4 ya huduma za dharura katika Hospitali ya Rufaa na hospitali za Bariadi, Maswa na Itilima. Mkoa umepokea vifaa tiba: CT Scan, X-Ray 6, Ultrasound 7, dental chairs 13 na mtambo wa oksijeni (mitungi 80–100 kwa siku).

Wagonjwa waliopatiwa huduma katika Hospitali ya Rufaa wameshuka kutoka 7,000 hadi 35,636, na jengo la Mama na Mtoto lenye vitanda 140 limekamilika kwa Bilioni 7.044. Kujengwa kwa hospitali kumepunguza gharama na kuokoa maisha ya wananchi waliokuwa wanasafiri Bugando au maeneo mengine kupata huduma.​


Kipengele 2020 2025Maelezo
Jumla ya fedha kwa afya (Billion TZS)69.75Utekelezaji wa miradi, vifaa tiba, dawa
Miradi ya afya (Billion TZS)26.80
Vifaa tiba (Billion TZS)10.96
Dawa (Billion TZS)31.99
Zahanati190242Ongezeko la 52 zahanati
Vituo vya afya1021Ongezeko la 11 vituo
Nyumba za watumishi wa afya175252Ongezeko la 77 nyumba
Bajeti ya dawa na vifaa tiba (Billion TZS)4.98.2
Upatikanaji wa dawa, vifaa tiba & vitendanishi (%)45%93%Ongezeko la 48%
Magari ya wagonjwa515Ongezeko la 10 magari
Magari ya usimamizi wa afya513Ongezeko la 8 magari
Watumishi wa kada ya afya1,7232,168Ongezeko la 25%
Wagonjwa waliopatiwa huduma7,00035,636Ongezeko kubwa
Hospitali za Wilaya zilizojengwa3Bariadi, Itilima, Busega
Hospitali kongwe zilizokarabatiwa3Bariadi Mji, Maswa, Meatu
Majengo ya wagonjwa mahututi (ICU)2Rufaa ya Mkoa na Meatu
Majengo ya dharura4Rufaa ya Mkoa + hospitali 3 za halmashauri
Vifaa tiba vya teknolojiaCT Scan 1, X-Ray 6, Ultrasound 7, Dental chairs 13, Mtambo oksijeni (mitungi 80–100)
Jengo la Mama na Mtoto1Vitanda 140, gharama Bilioni 7.044
 
Kwa hizo kazi alizofanta, anastahili mi5Tena
 

RAIS SAMIA: KIONGOZI WA MABADILIKO NA MAENDELEO YA KWELI​


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameendelea kuthibitisha kuwa uongozi wake ni wa vitendo, uwajibikaji na matokeo chanya kwa Taifa. Tangu aingie madarakani mwaka 2021, ameweka msisitizo mkubwa katika kukuza uchumi, kuboresha maisha ya wananchi na kulinda amani na mshikamano wa kitaifa.


Katika kipindi cha uongozi wake, Tanzania imepiga hatua kubwa katika sekta za elimu, afya, nishati, maji, kilimo, miundombinu na ushirikiano wa kimataifa. Kupitia falsafa ya “Kazi Iendelee”, Rais Samia ameonyesha uthubutu wa kusimamia utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Reli ya Kisasa (SGR), Mradi wa Kufua Umeme wa Maji – Julius Nyerere, ujenzi wa barabara na madaraja makubwa, upanuzi wa shule na hospitali, sambamba na kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama.


Aidha, sera zake zimeimarisha uchumi kwa kuongeza mapato ya ndani, kupunguza utegemezi, na kuvutia wawekezaji wakubwa kutoka ndani na nje ya nchi. Kupitia ziara zake za kidiplomasia, Tanzania sasa imeimarika kimataifa, ikiheshimika kama nchi ya amani, fursa na mshirika thabiti katika maendeleo ya kikanda na kimataifa.


Zaidi ya yote, Rais Samia Suluhu Hassan amejipambanua kama kiongozi anayejali wananchi, hasa wanawake na vijana, akihamasisha ushiriki wao katika uchumi, siasa na uongozi. Hii imemfanya kuwa mfano wa kuigwa Afrika na duniani kote, akiweka historia kama mwanamke wa kwanza kuwa Rais wa Tanzania na kuongoza nchi kwa ufanisi mkubwa.
 
Back
Top Bottom