Picha: ODM walipokutana uso kwa uso na Jubilee, sijui nini kingetokea kama ingekuwa CHADEMA na CCM

6dfd5c531c0b33402485b82a7e496a18.jpg
wafia Chama .......uyo jamaa kama anaenda kuua chatu kumbe tofa anaenda kumtwisha binadamu
Elimu ndugu, sio hao tu, hata wale wanaowaita wapinzani wao kwa majina mabaya na matusi ni mbegu tu, zikioteshwa na kukomaa matunda yake ndio hayo. Ubongo wa mwanadamu uko na udhaifu sana.
 
Hivi hata Democratic na Republican wana hizi sijui yellow sijui black gurds
 
Kenya hawakuwahi kuwa na itikadi kama zetu, kwahiyo hii safari walitakiwa wawe wameshaianza tangu mwaka 1962 huko wakati sisi tumeanza 1992 miaka 30 baadae, na hadi sasa tuko makini kuliko wao. Kiaje wao wawe wanapaa sasa?

Ok labda kama nimeliangalia hili suala kwa wigo mwembamba lkn ukiangalia yanayotokea nchini kwetu tena ni tofauti kiasi na kenya kabisa, mfano ndani ya kenya unaona rais wao anawachukulia wapinzani kama marafiki lkn ni kinyume na nchini kwetu.. iliwai kusikika na kiongozi mkuu wa nchi hii sasa akidaI wapinzani ni marufuku kukanyaga ikulu sasa hayo ndio mambo gani? ikulu si ya watanzania? pili hakuna jambo ambalo lingeweza kuinenepesha nchi hii kama kuwashirikisha watu wa kila aina katika kuijenga hii nchi.. hapa namanisha linapokuja suala la ujenzi wa nchi itikadi za kisiasa ziwekwe kando kabisa, mimi sioni taabu rais kumteua mpinzani kuwa waziri sema tumekumbatia katiba na sheria za kizamani ambazo zinatufanya kuwa masjkini wa kutupwa ndani ya uwepo wa mali nyingi kama madini n.k sasa wakenya wenzetu kiukweli wanatuzidi na tusipokuwa makini watatuzidi zaidi.......
 
Siku ujinga ukipungua kwa kiasi kikubwa tutakuwa na siasa za level ya juu sana tu.
Haiwezekani jamaa anaahidi Kuwajengea zahanati wananchi, anaweka msingi, miaka mitano ikikaribia kuisha anakuja anaweka kama kozi mbili, mkimchagua anaacha tena ikikaribia anaweka hadi kwenye lenta. mtu anaishi kiujanjaujanja miaka hata 20 inapita ni kiongozi...
.

Sema kwamba, siku ujinga ukipungua, CCM itatolewa madarakani na taifa litaanza kusonga mbele kikwelikweli! Sasa CCM ina-capitalise kwenye ujinga wa watanzania wengi; ndiyo maana CCM inashinda zaidi kwenye maeneo ambayo yana watu wenye viwango vidogo vye elimu.

Haiwezekani kwa miaka 55+ licha ya umaskini wa kutupa, ahadi za uongo za maisha bora, ahadi za uongo za kupambana na rushwa n.k., CCM bado inashinda chaguzi!
 
Kwa mistari miwili nitajie sera za ujumla za cdm, pia nitajie ni nini sera ya cdm kuhusiana na ardhi? Irani na sera ni vitu viwili, lakini kikubwa hapa ni itikadi, hiyo ndiyo itakayoongoza sera zote. Haya, zinawekeza mmeandikiwa nilishawahi kukihubiri majukwaani? Labda kweli mimi ni mweupe.
Kapitoa katiba ya chadema ipo humu jukwaanu ukishindwa ntaipaste hapa kursa yenye itikadi na sera kuu za chama..... zipo zinahubiriwa sana na mojawapo ilikuwa ni nguvu ya umma kwamba wananchi ndio wenye sauti kwenye uongozi wa serikali na uendeshwaji wa maliasili za taifa kwa itikadi hyo ikazaa ilani ambapo zinazaa sera mbalimbal za chama.

Zimehubiriwa majukwaani ndio hizo itikadi na ndio maana chadema ikakubalika mpaka kwa watoto wa shule sa msingi maana itikadi ya NGUVU YA UMMA imeaminisha watu kuwa chadema ni chama kinachojali maslahi ya wananchi wote na imejinasibu hivyo kupitia shughuli za kibunge kma mnavyoona sera zote za kinonyaji huwa zinapingwa na upinzani tu ssa majukwaa gani tena ulitaka tuhubiri itikadi yetu kuu ya PEOPLE'S POWER???

anyway kma hujasoma katiba ulikuwa huna haki ya kutoa povu humu maana unalalamika usichokijua....... ni vzuri upitie makabrasha kma za KUB, ilani ya uchaguzi na katiba ya chama kabla hujaanza kusema vyama havina itikadi zaidi ya rambirambi cjui bashite!!! Umenishangaza mkuuu
 
Mimi ni mweupe, sasa wewe mweusi uwe makini pia, sijasema "mpinzani" nimesema "upinzani". Kisiasa, cdm ina upinzani na ccm na ccm kina upinzani na cdm. Huu upinzani kwa Tz, japo ulitakiwa uwe ni wa kisiasa tena kwa hoja, kwetu ni uadui.

Kwa hili, nilimaanisha upinzani ni uadui, ccm anamfanyia uadui cdm na cdm anamfanyia ccm, hali iko hivyo. Ukijifanya kipofu, upofu hautakupa nafasi ya kuliona hili.
Chadema imemfanyia nani uadui??? Yaani ccm anaanzisha uadui mpinzani aki retaliate ndio unasema WOTE TUNACHUKI!!!! get serious mkuu...... ccm ndio wamepandikiza chuki ona kwanza bunge la katiba waliposema zenji haitoki kwa kura mara cjui zenji ni ya watu weusi!!!! Mara rais hatotokea kaskazini and all that kuwa wapinzani wakishinda jeshi litapindua nchi!!! Cjui CUF ya waislam chadema ya wakristo na wachagga n.k Ssa wewe ulitaka wapinzani wacheke na hao hao maccm?

Ni bora ungeshauri hao maccm waache ubaguzi maana ndio wachochea chuki zote hizi na wao ndio wakulaumiwa sioni wapi ccm wakijirekebisha hawa wapinzani watakwaruzana nao??? its simple logic nashangaa ssa wwe unatoka povu kuwa neutral wakati unajua kosa lipo kwa CCM!!

Wwe unafkiti wapinzani wangekuwa wanafanya hila za ccm tz pangekalika??? Au wangekuwa wako hai hao viongozi wa upinzani?? Funny afu na wwe ni great thinker
 
Sema kwamba, siku ujinga ukipungua, CCM itatolewa madarakani na taifa litaanza kusonga mbele kikwelikweli! Sasa CCM ina-capitalise kwenye ujinga wa watanzania wengi; ndiyo maana CCM inashinda zaidi kwenye maeneo ambayo yana watu wenye viwango vidogo vye elimu.

Haiwezekani kwa miaka 55+ licha ya umaskini wa kutupa, ahadi za uongo za maisha bora, ahadi za uongo za kupambana na rushwa n.k., CCM bado inashinda chaguzi!
wapinzani wanacapitalize kwenye matatizo ya CCM.
Binafsi nadhani wapinzani ndio wanaongoza kwa kuendeleza ujinga.
Hakuna competent mbadala wa CCM. Nitaamini sana nikisikia CCM inajibadilisha kuliko kuamini upinzani utaleta kitu kipya.
 
wapinzani wanacapitalize kwenye matatizo ya CCM..
Chief, that's obvious in multipartism!

Binafsi nadhani wapinzani ndio wanaongoza kwa kuendeleza ujinga..

Unaeleza kufafanua kwa mifano?

Maana ninavyojua CCM ndiyo iliyo madarakani. Unaweza kuona namna gani wanazalisha na kudumisha ujinga kwa wanavyoendesha sekta ya elimu ya umma na kuminya uhuru wa habari. Elimu na habari ndiyo misingi ya taifa lenye watu werevu. Ndiyo maana mataifa mengi ya Ulaya wanatoa elimu bure (ya umma) na angalau kunakuwa na magazeti ya bure ili wananchi wapate taarifa, hata wale wasioweza kununua.

Hakuna competent mbadala wa CCM. .
Typical excuse kwa wanaogopa mabadiliko makubwa. Kwa hiyo wewe kwa akili zako unaona bora kuendelea kuwa na impotent CCM, kuliko kuwa na mbadala ambao hufahamu watatendaji na watawajibikaje?

Naamini watanzania wangeweza kuwa hakuna competent mbadala wa wakoloni, hadi leo tungekuwa tunatawaliwa na wakoloni!

Nitaamini sana nikisikia CCM inajibadilisha kuliko kuamini upinzani utaleta kitu kipya.

CCM haiwezi kujibadilisha kamwe! It is rotten to its roots!

Hivi unaweza kunitajia taifa lenye kufuata demokrasia ambalo limeongozwa na chama kimoja kwa zaidi ya miaka 30 na taifa hilo likaendelea?

Mnataka CCM ifanye kuonyesha kwamba kimeshashindwa?
 
Chief, that's obvious in multipartism!



Unaeleza kufafanua kwa mifano?

Maana ninavyojua CCM ndiyo iliyo madarakani. Unaweza kuona namna gani wanazalisha na kudumisha ujinga kwa wanavyoendesha sekta ya elimu ya umma na kuminya uhuru wa habari. Elimu na habari ndiyo misingi ya taifa lenye watu werevu. Ndiyo maana mataifa mengi ya Ulaya wanatoa elimu bure (ya umma) na angalau kunakuwa na magazeti ya bure ili wananchi wapate taarifa, hata wale wasioweza kununua.


Typical excuse kwa wanaogopa mabadiliko makubwa. Kwa hiyo wewe kwa akili zako unaona bora kuendelea kuwa na impotent CCM, kuliko kuwa na mbadala ambao hufahamu watatendaji na watawajibikaje?

Naamini watanzania wangeweza kuwa hakuna competent mbadala wa wakoloni, hadi leo tungekuwa tunatawaliwa na wakoloni!



CCM haiwezi kujibadilisha kamwe! It is rotten to its roots!

Hivi unaweza kunitajia taifa lenye kufuata demokrasia ambalo limeongozwa na chama kimoja kwa zaidi ya miaka 30 na taifa hilo likaendelea?

Mnataka CCM ifanye kuonyesha kwamba kimeshashindwa?
ccm inaundergo evolution.
ni sawa na kumlazimisha mwanadamu(Modern Man) kuwa Zinanthropus kwa sababu alipokuwa zinjanthropus alikwa na udhaifu. Kama CCM imewahi kusababisha matatizo na leo inajinadi kujirekebisha na kuja kwa ubora zaidi inabidi uielewe.

Siku zote CCM huwa haina matatizo, wenye matatizo na wanayoyasababisha ni wabinafsi wachache....
Ila misingi yake iko sawa tu.
Maoni yangu naona hawa wapinzani ni weakest compared to CCM ya miaka yoyote ile.
Weakest sio kwa idadi au kifedha bali tukiangalia wanaweza kudeliver nini kwa kuangalia mfumo wa maisha yao hata matumizi ya kodi kidogo wanazopewa kama ruzuku.

Ni maoni yangu sio lazima yawe sahihi kwa upande wako mkuu.
 
wapinzani wanacapitalize kwenye matatizo ya CCM.
Binafsi nadhani wapinzani ndio wanaongoza kwa kuendeleza ujinga.
Hakuna competent mbadala wa CCM. Nitaamini sana nikisikia CCM inajibadilisha kuliko kuamini upinzani utaleta kitu kipya.
Maneno haya yanaweza kusemwa na mtu mpumbavu tuu . .

Tulipopata Uhuru 1961, ni mtanzania gani alikua ameandaliwa kuwa Raisi, Waziri Mkuu, au hata Waziri . . ?!

Unasema wapinzani wana "capitalize" kwenye matatizo ya ccm . . , una maana gani . . ?!
Yaani ulitaka mtoe bure dhahabu yetu wapinzani wakae kimya . . ?!
Ulitaka wapinzani wazungumzie nini labda . . , au wazungumzie kutatua matatizo ya wananchi wa Kenya . . ?!
 
ccm inaundergo evolution
ni sawa na kumlazimisha mwanadamu(Modern Man) kuwa Zinanthropus kwa sababu alipokuwa zinjanthropus alikwa na udhaifu. Kama CCM imewahi kusababisha matatizo na leo inajinadi kujirekebisha na kuja kwa ubora zaidi inabidi uielewe.

Tatizo lako ni moja tu: uwa haujibu maswali specifically kama ulivyouliza. Mimi nime-quote specific parts ya hoja zako na kukuuliza maswali. Wewe unakuja unatoa generalised responses.

Nilikuuliza kwamba unaweza kufafanua ni namna gani upinzani wanaongoza kwa kuendeleza ujinga

Sasa nakuomba unifafanulie namna ambavyo CCM inago evolution.

Na tatu, je CCM imeshawahi kukiri kusababisha hayo matatizo? Imetuomba watanzania msamaha? Imewachukulia hatua gani waliosababisha matatizo hayo?


Siku zote CCM huwa haina matatizo, wenye matatizo na wanayoyasababisha ni wabinafsi wachache....
Ila misingi yake iko sawa tu.

Ulisoma kweli hili kabla ya kuliandika? Chama kinaundwa na watu! Bila watu hakuna chama! Hao wabinafsi wachache ninaowafahamu mimi ndiyo walikuwa (na wengine bado) ni mihimili ya chama. Mkapa akiwa Mwenyekiti ndiye aliyetekeleza sera za ubinafsishaji. Kikwete akiwa Mwenyekiti ndiyo mikataba hadi ikasainiwa nje ya nchi! Hapa naongelea sekta ya madini tu! Siongelei sekta nyingine ambazo vigogo wa CCM ndiyo wanaifisadi nchi hii na kuisababishia matatizo tuliyonayo leo.


Maoni yangu naona hawa wapinzani ni weakest compared to CCM ya miaka yoyote ile.

Generalised response nyingine. Kwa kuwa tunajadiliana, tafadhali fafanua kwa kina unachokisema hapa. Pia zingatia mazingira ya kufanya siasa sasa hivi. Bila kusahau uchama dola wa CCM. Halafu urudie tena kusema ulivyosema. Kama ni weakest, kwanini Magufuli na serikali yake wanatumia nguvu nyingi sana (kwa mali na vyombo vya dola) kupambana na weak opposition?


Weakest sio kwa idadi au kifedha bali tukiangalia wanaweza kudeliver nini kwa kuangalia mfumo wa maisha yao hata matumizi ya kodi kidogo wanazopewa kama ruzuku..

Kama wanatumia ruzuku vibaya kwanini hawachukuliwi hatua? Serikali si ina vyombo vyake vya udhibiti wa fedha za umma, sasa kwanini wapinzani hawadhibitiwi katika hilo la ruzuku? Tena si wanakaguliwa mara kwa mara, serikali inafanya nini juu ya hili?

Yaani kila unachokiongea kinadhiirisha jinsi gani CCM ilivyoshindwa!

Ni maoni yangu sio lazima yawe sahihi kwa upande wako mkuu.[/QUOTE]

Najua. Ni vyema kutoa maoni yako. Lakini kwa majadiliano mazuri ni vyema uka-back up maoni yako ni particular/specific examples.
 
Pamoja na mauaji ya huyo mama.
bado hii scene ni ya kupongezwa na kusisitizwa na sisi tuna ya kujifunzwa kutoka kwenye tukio hilo
0fgjhs1sa066i2d97.942e3f91.jpg
Hapa kanamwambia na awamu hii nakupiga tena!! Uhuru au Kenya kwa ujumla demokrasia ipo juu kuliko upumbavu wa hapa kwetu!!
 
Tatizo lako ni moja tu: uwa haujibu maswali specifically kama ulivyouliza. Mimi nime-quote specific parts ya hoja zako na kukuuliza maswali. Wewe unakuja unatoa generalised responses.

Nilikuuliza kwamba unaweza kufafanua ni namna gani upinzani wanaongoza kwa kuendeleza ujinga

Sasa nakuomba unifafanulie namna ambavyo CCM inago evolution.

Na tatu, je CCM imeshawahi kukiri kusababisha hayo matatizo? Imetuomba watanzania msamaha? Imewachukulia hatua gani waliosababisha matatizo hayo?




Ulisoma kweli hili kabla ya kuliandika? Chama kinaundwa na watu! Bila watu hakuna chama! Hao wabinafsi wachache ninaowafahamu mimi ndiyo walikuwa (na wengine bado) ni mihimili ya chama. Mkapa akiwa Mwenyekiti ndiye aliyetekeleza sera za ubinafsishaji. Kikwete akiwa Mwenyekiti ndiyo mikataba hadi ikasainiwa nje ya nchi! Hapa naongelea sekta ya madini tu! Siongelei sekta nyingine ambazo vigogo wa CCM ndiyo wanaifisadi nchi hii na kuisababishia matatizo tuliyonayo leo.




Generalised response nyingine. Kwa kuwa tunajadiliana, tafadhali fafanua kwa kina unachokisema hapa. Pia zingatia mazingira ya kufanya siasa sasa hivi. Bila kusahau uchama dola wa CCM. Halafu urudie tena kusema ulivyosema. Kama ni weakest, kwanini Magufuli na serikali yake wanatumia nguvu nyingi sana (kwa mali na vyombo vya dola) kupambana na weak opposition?




Kama wanatumia ruzuku vibaya kwanini hawachukuliwi hatua? Serikali si ina vyombo vyake vya udhibiti wa fedha za umma, sasa kwanini wapinzani hawadhibitiwi katika hilo la ruzuku? Tena si wanakaguliwa mara kwa mara, serikali inafanya nini juu ya hili?

Yaani kila unachokiongea kinadhiirisha jinsi gani CCM ilivyoshindwa!

Ni maoni yangu sio lazima yawe sahihi kwa upande wako mkuu.

Najua. Ni vyema kutoa maoni yako. Lakini kwa majadiliano mazuri ni vyema uka-back up maoni yako ni particular/specific examples.[/QUOTE]
nakujibu hivi kutokana na mazingira niliyopo, ningekuwa na muda wa kutosha ningekujibu hatua moja baada ya nyingine kwa maoni yangu lakini ambayo yanaweza yasihabihiane unachodhani ni sahihi kichwani mwako.
 
Maneno haya yanaweza kusemwa na mtu mpumbavu tuu . .

Tulipopata Uhuru 1961, ni mtanzania gani alikua ameandaliwa kuwa Raisi, Waziri Mkuu, au hata Waziri . . ?!

Unasema wapinzani wana "capitalize" kwenye matatizo ya ccm . . , una maana gani . . ?!
Yaani ulitaka mtoe bure dhahabu yetu wapinzani wakae kimya . . ?!
Ulitaka wapinzani wazungumzie nini labda . . , au wazungumzie kutatua matatizo ya wananchi wa Kenya . . ?!
umeandika vitu vya kuchanganyikachanganyika sijui unataka nijibu nini.
Nyerere wakati anachukua nchi alikuwa na exposure kubwa na common sense kubwa kuliko wengi wanaothani ni mbadala wa watawala wa sasa.
Narudia wapinzani hawana uwezo huo unaodhani wanao. Huu ndio ukweli wangu japo kwako unaonekana ni upumbavu na uchwara
 
Kapitoa katiba ya chadema ipo humu jukwaanu ukishindwa ntaipaste hapa kursa yenye itikadi na sera kuu za chama..... zipo zinahubiriwa sana na mojawapo ilikuwa ni nguvu ya umma kwamba wananchi ndio wenye sauti kwenye uongozi wa serikali na uendeshwaji wa maliasili za taifa kwa itikadi hyo ikazaa ilani ambapo zinazaa sera mbalimbal za chama.

Zimehubiriwa majukwaani ndio hizo itikadi na ndio maana chadema ikakubalika mpaka kwa watoto wa shule sa msingi maana itikadi ya NGUVU YA UMMA imeaminisha watu kuwa chadema ni chama kinachojali maslahi ya wananchi wote na imejinasibu hivyo kupitia shughuli za kibunge kma mnavyoona sera zote za kinonyaji huwa zinapingwa na upinzani tu ssa majukwaa gani tena ulitaka tuhubiri itikadi yetu kuu ya PEOPLE'S POWER???

anyway kma hujasoma katiba ulikuwa huna haki ya kutoa povu humu maana unalalamika usichokijua....... ni vzuri upitie makabrasha kma za KUB, ilani ya uchaguzi na katiba ya chama kabla hujaanza kusema vyama havina itikadi zaidi ya rambirambi cjui bashite!!! Umenishangaza mkuuu
Hakuna itikadi iitwayo "nguvu ya umma " labda hiyo iwe ni sera au msimamo.
 
Hakuna itikadi iitwayo "nguvu ya umma " labda hiyo iwe ni sera au msimamo.
Soma hyo page nzima ndio uone kma NGUVU YA UMMA HAIONGELEWI chini ya kipengele cha itikadi ya chama...... au umekariri itikadi mpka iwe sijui far right sijui ??? Ndio maana nlisema kabla hujasoma usije kuleta mada zisizo na mashiko
 

Attachments

  • Screenshot_2017-06-04-18-22-21.png
    Screenshot_2017-06-04-18-22-21.png
    42.6 KB · Views: 22
Soma hyo page nzima ndio uone kma NGUVU YA UMMA HAIONGELEWI chini ya kipengele cha itikadi ya chama...... au umekariri itikadi mpka iwe sijui far right sijui ??? Ndio maana nlisema kabla hujasoma usije kuleta mada zisizo na mashiko
Nimekusoma, kila chama na nchi ina maandishi kama hayo, mfano katiba tuliyo nayo inasema Tz ni nchi ya kufuata itikadi za "ujamaa na kujitegemea" ccm ni chama cha kijamaa.
 
Back
Top Bottom