Watu wamechoka, kinachohitajika ni Elimu makini na sahihi, kuwaeleza ukweli na udhaifu unaowaumiza kila siku maishani mwao. Pasipo elimu bayana na makini bado kazi itakuwa kubwa, wanaweza shangilia ila wasichukue hatua muhimu ya kuondoa waliochoka CCM na kuweka wenye hamu ya kuleta mabadiliko CDM. Tuwaelekeze bila kuchoka, tuwaamshe waliolala, tuwapandishe hasira kwa kuwaonesha ukweli, tofauti na wanavyotumiwa na wachache kwa manufaa binafsi. Hongera sana kwa kazi hii kubwa iliyofanywa na wapiganaji hawa, songeni mbele maana wakati wa mavuno umekaribia. We shall overcome... very soon we will be there.