Picha: Dk Slaa azidi kuwabana CCM

Picha: Dk Slaa azidi kuwabana CCM

hoyce

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2010
Posts
1,117
Reaction score
298
attachment.php

attachment.php


Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa amewaambia wakazi hawa wa Karagwe kwamba hata viongozi wapya wa sekretarieti ya CCM wakizunguka nchi nzima, hawana cha kuwambia wananchi kwa sababu ndio waliosababisha matatizo makubwa yanayowasumbua wananchi.

Akizungumza katika Mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Kayanga, Karagwe Mkoani Kagera juzi, Dk. Slaa alisema CCM hawana majibu kwa Maswali Magumu yanayowakabili WATANZANIA.

Alisema Tanzania inahitaji Mabadiliko makubwa ya kimfumo na usimamizi makini wa raslimali zetu, na kwamba mambo haya hayawezi kufanyika chini ya utawala wa CCM.

Dk. Slaa alikuwa Mkoani Kagera kuhudhuria Mkutano wa Baraza la Mashauriano la Mkoa, ambalo pia lilialika viongozi wa mikoa yote ya Tanzania. Wakiwa Karagwe, viongozi hao walisajili wanachama wapya na kufungua Matawi katika Kila kijiji kwenye kata za Majimbo ya Karagwe na Kyerwa.
 

Attachments

  • nyomi.jpg
    nyomi.jpg
    84.4 KB · Views: 1,730
  • Kayanga.jpg
    Kayanga.jpg
    88.6 KB · Views: 1,743
Kinana, mangula,na secretariati yoote ya ccm wamekuwepo serikalini kwa zaidi ya miaka 30, je leo ndio wamepata akili ya kutatua kero za wananchi kwa kuzunguka nchi nzima??

Miaka 5i bado mnatoa ahadi??
Miaka 51 hata umeme mjini tu ni shida??
Miaka 51 hata huduma ya madawa hospitalini ni shida???
Nchi inaresource za kila aina, madini adimu yanayopatika tz pekee yake kama tanzanite yangefaa kusomesha watu wote bure mpaka chuo kikuu, achilia mbali gesi ya sasa, uraniumu

haohao viongozi wa ccm ndio wameua viwanda zaidi ya 80 nchi nzima vilivyokuwa vinatoa ajira kwa watz zaidi ya 500,000, viwanda vimekufa na hakuna aliyefungwa kwa uzembe,

i hate ccm kama navyo yahate majini (shetani)

ccm= mashetani:
 
Mkuu kuna uzushi kua rais wetu mtarajiwa kapata ajali kuna ukweli kuhus hilo?
 
Mkuu kuna uzushi kua rais wetu mtarajiwa kapata ajali kuna ukweli kuhus hilo?
Uongo mtupu. Soma alivyofafanua kwenye NIPASHE;
Akiongea na mwandishi wa habari hizi, Dk. Slaa alisema anamshukuru Mungu kuwa hao wanaomzushia kifo wanazidi kumuongezea maisha na kumpa nguvu na kuendelea na kazi zake.

"Hizo ni propaganda za watu wasionitakia mema, hivi ninavyoongea na wewe niko katika kijiji cha Nkwenda, Wilaya mpya ya Kyelwa, huku Bukoba ndio nimetoka kuteremka kwenye jukwaa kuongea na wananchi," alisema Dk. Slaa na kuongeza "Mimi ni mzima kabisa na nikitoka hapa nakwenda kwenye mkutano mwingine."
Alisema hiyo si mara ya kwanza yeye kuzushiwa kifo, lakini anamshukuru Mungu kuwa wabaya wake wanavyozidi kumzushia habari mbaya wanaendelea kumuongezea siku za kuishi.
 
Uongo mtupu. Soma alivyofafanua kwenye NIPASHE;
Akiongea na mwandishi wa habari hizi, Dk. Slaa alisema anamshukuru Mungu kuwa hao wanaomzushia kifo wanazidi kumuongezea maisha na kumpa nguvu na kuendelea na kazi zake.

Hizo ni propaganda za watu wasionitakia mema, hivi ninavyoongea na wewe niko katika kijiji cha Nkwenda, Wilaya mpya ya Kyelwa, huku Bukoba ndio nimetoka kuteremka kwenye jukwaa kuongea na wananchi, alisema Dk. Slaa na kuongeza Mimi ni mzima kabisa na nikitoka hapa nakwenda kwenye mkutano mwingine.
Alisema hiyo si mara ya kwanza yeye kuzushiwa kifo, lakini anamshukuru Mungu kuwa wabaya wake wanavyozidi kumzushia habari mbaya wanaendelea kumuongezea siku za kuishi.
nashukuru ndugu yangu kwa taarifa!
 
Mkuu hoyce CCM wanafanya Mikutano kwenye mikoa yenye mbuga za wanyama hii inashiria nini kwenye uongozi mpya wa jangili kinana?

Sasa ndo maliasili zetu zitauzwa mchana kweupe bila woga maana vinara wa uuzaji wa nyara hizo kwa sasa ni viongozi wakuu wa chama!
 
Last edited by a moderator:
Sasa ndo maliasili zetu zitauzwa mchana kweupe bila woga maana vinara wa uuzaji wa nyara hizo kwa sasa ni viongozi wakuu wa chama!
baada ya kuteuliwa kuwa katibu mkuu wasomali walikuwa wanapiga horn barabarani utafikiri simba au yanga imeshinda
 
Wanaomzushia kifo rais wetu wa moyoni nazani watakuwa TISS,kama sio zoka atakuwa rama.
 
Wanaomzushia kifo rais wetu wa moyoni watakuwa TISS kama sio zoka ni rama
 
Wanaomzushia kifo rais wetu wa moyoni watakuwa ni TISS! Hawa jamaa ovyo kabisa!
 
Nafikiri CCM wamemchagua KINANA ili awape mbinu mbadala ya kupata fedha kuelekea 2015 kwani wamegundua njia waliyotumia 2005 (kuchota kutoka BOT) haiwezekani tena kwa sasa.

Inaonekana njia pekee iliyobaki ni kupitia maliasili ya wanyama pori hususan TENBO na FARU na KINANA ni mahiri katika eneo hilo.
 
Back
Top Bottom