Yeah inawezekana ikawa kweli kuna tofauti kubwa hapo lakini tambua ya kwamba scientifically huwezi ukahitimisha mtu fulani kupendwa kutokana tu na kuwa na umati mkubwa. Kuna factors nyingi ambazo pengine zinaweza kusababisha kuwepo kwa huo umati mkubwa na usishangae kukuta hao walio wachache kimwonekano ndiyo wakawa wakweli kutoka moyoni huku hao wengi unaowaona hapo wakawa ni wanafiki tu na wapo hapo kama ni sehemu tu ya kupotezea muda kama siyo kuondoa tu stress ya ugumu wa maisha pengine uliosababishwa na huyo huyo wanayemshangilia hapo. Sasa hivi kadri siku zinavyoenda ndiyo uwezo wa kufikiri na wa kuona mambo ya tija ya watanzania unaonekana.