EINSTEIN112
JF-Expert Member
- Oct 26, 2018
- 21,709
- 35,702
Sisi tunaotoka Kiluvya kuja mjini hakuna vituo vya mafuta njiani, wajenzi wa barabara wameziba njia zote za kuingilia vituoni.
Mfano kituo cha Henry Filling Station kilichopo Chuo cha St. Joseph kuingia hadi upite Luguruni utembee rough road kama 1km to & from ndio uendelee na safari.
Oilcom Mbezi Kwa Yusufu wamefunga njia ya kuingia hadi uzunguke nyuma ya sheli.
Ukija Temboni sasa, kuingia hadi uzungukie kile kibarabara cha vumbi kama unarudi Msuguri ndio uingie sheli.
Yaani kama unaelekea mjini sheli isiyo na kizuizi ni Puma iliyopo Baruti.
Huu ni usumbufu usio na ulazima, wangeweza kuacha nafasi kidogo ili huduma ya upatikanaki wa mafuta kwa watumiaji wa vyombo vya moto uwe rahisi.
Tunajua sheli zipo kwenye hifadhi wa barabara inayomilikiwa na Serikali ila kwa wakati huu wakati mkiweka mambo sawa na wamiliki wa sheli sisi wananchi tusipate huu usumbufu.
Nawasilisha!
Mfano kituo cha Henry Filling Station kilichopo Chuo cha St. Joseph kuingia hadi upite Luguruni utembee rough road kama 1km to & from ndio uendelee na safari.
Oilcom Mbezi Kwa Yusufu wamefunga njia ya kuingia hadi uzunguke nyuma ya sheli.
Ukija Temboni sasa, kuingia hadi uzungukie kile kibarabara cha vumbi kama unarudi Msuguri ndio uingie sheli.
Yaani kama unaelekea mjini sheli isiyo na kizuizi ni Puma iliyopo Baruti.
Huu ni usumbufu usio na ulazima, wangeweza kuacha nafasi kidogo ili huduma ya upatikanaki wa mafuta kwa watumiaji wa vyombo vya moto uwe rahisi.
Tunajua sheli zipo kwenye hifadhi wa barabara inayomilikiwa na Serikali ila kwa wakati huu wakati mkiweka mambo sawa na wamiliki wa sheli sisi wananchi tusipate huu usumbufu.
Nawasilisha!