Peter: Sihusiki P-Square kuvunjika

Donatila

JF-Expert Member
Oct 23, 2014
7,557
21,497
Peter-Okoye-300x294.jpg


NYOTA wa muziki nchini Nigeria ambaye alikuwa anaunda kundi la P-Square, Peter Okoye, ameweka wazi kuwa yeye si chanzo cha kundi hilo kuvunjika.

Kundi hilo kwa sasa limevunjika kwa madai kwamba kila mmoja alikuwa anafanya mambo kinyume na utaratibu na kila mmoja sasa anafanya kazi peke yake.

Mwishoni mwa wiki iliyopita, mapacha hao walikuwa wanasherehekea siku yao ya kuzaliwa, lakini kila mmoja alionesha kusherehekea kivyake japokuwa Paul aliposti picha yao ya utotoni.

Taarifa zilisambaa kwenye mitandao kwamba Peter ndio chanzo cha kuvunjika kwa kundi hilo, lakini ametumia ukurasa wake wa Instagram na kukanusha taarifa hiyo.

“Nashangaa kuonekana kuwa mimi ndio mwenye kosa, hakuna ukweli wowote nadhani kosa langu ni kuweka wazi tofauti zetu, ila mimi si chanzo kama watu wanavyosema kwenye mitandao ya kijamii, lakini nashukuru kila kitu kinakwenda kama kilivyopangwa,” aliandika Peter.


Mtanzania
 
Huwezi kushindana na nature....

Awali, originally, Peter and Paul walikuwa mbegu moja ya Mzee Okoye! Ilipofika makazi mapya, mbegu ikagawanyika pasu kwa pasu akatokea Peter na Paul

Peter na Paul nao wakaunganika kimuziki,

Na hivi sasa wamegawanyika tena kama ambavyo mbegu iliyowatoa wao ilivyokuwa imegawanyika hapo kabla.
 
Yeye alitaka kuwa recognized kama anaweza kutunga nyimbo na kuimba pia, sasa pacha wake na kaka yao wakakataa kwa kuwa hawakumuamini, akaona enough is enough kama haaminiwi kwa nn asifanye kazi akaonesha kipaji chake, na ndo alichofanya mpaka sasa anangoma mbili na zote ni hit songs town hapa
 
Yeye alitaka kuwa recognized kama anaweza kutunga nyimbo na kuimba pia, sasa pacha wake na kaka yao wakakataa kwa kuwa hawakumuamini, akaona enough is enough kama haaminiwi kwa nn asifanye kazi akaonesha kipaji chake, na ndo alichofanya mpaka sasa anangoma mbili na zote ni hit songs town hapa
umetumia kigezo kipi kwamba ni hit song?
 
Huwezi kushindana na nature....

Awali, originally, Peter and Paul walikuwa mbegu moja ya Mzee Okoye! Ilipofika makazi mapya, mbegu ikagawanyika pasu kwa pasu akatokea Peter na Paul

Peter na Paul nao wakaunganika kimuziki,

Na hivi sasa wamegawanyika tena kama ambavyo mbegu iliyowatoa wao ilivyokuwa imegawanyika hapo kabla.
dah
 
Yeye alitaka kuwa recognized kama anaweza kutunga nyimbo na kuimba pia, sasa pacha wake na kaka yao wakakataa kwa kuwa hawakumuamini, akaona enough is enough kama haaminiwi kwa nn asifanye kazi akaonesha kipaji chake, na ndo alichofanya mpaka sasa anangoma mbili na zote ni hit songs town hapa
Hivi nn maana ya hit song?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom