Nafikiri ni makubaliano. Kama kampuni ipo Uswiswi na inataka uilipe kwa US au pesa ya Uswiswi, utailipa kwa hiyo. Kama ni kampuni ya Ujerumani na wanataka uwalipe kwa Euro basi utafanya hivyo.
Dhahabu ilitumika dunia ilipokuwa inatumia gold standard. Yaani nchi inachapisha pesa kulingana na kiasi cha dhahabu ilichonacho. Wakaona hilo linacheleweshs uchumi kukuwa. Wakaweka ratio. Kama una dhahabu 10 basi uweze kuchapisha pesa 20, baadaye wakaongeza tena, kama una dhahabu kumi basi uweze chapisha pesa 50. Kisha wakaja, kama una dhahabu kumi basi uchapishe pesa 100.
Kabisakabisa, pesa ilikuwa ni risiti(stakabadhi ) ya kuonyesha kiasi cha dhahabu ulicho nacho.
Mwisho wakaja na kusema, unaweza chapisha pesa bila dhahabu. Hivyo ndivyo gold standard ilivyokufa na pesa kugeuka makaratasi yanayotegemea matamko ya serikali na imani ya watu kuipa thamani.
matumizi ya gold standard yana historia ndefu sana.
Hata benki za biashara hukopeshwa na benki kuu kwa mtindo huo. Mfano kama benki inaakiba ya bilioni 10 basi benki kuu wanaweza ikopesha Bilioni 20, 30 50 au yoyote kulingana na ratio iliwekwa na baenki kuu. So mara nyingi utakuta benki nazo ni madalali tu, pesa wanazokopesha na mtaji wao ni tofauti kabisa.