Pesa ni makaratasi, literally.

Pesa ni makaratasi, literally.

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
10,884
Reaction score
18,824
Pesa ina historia ndefu sana lakini leo napenda tujadili status iliyonayo pesa leo.

1. Pesa kama pesa haina thamani yeyote, ni makaratasi tu. Thamani ya pesa inatokana na wananchi kuamini kuwa ina thamani na serikali kutunga sheria kuwalazimisha watu kukubali kuwa pesa ina thamani. Ndiyo maana kwenye pesa kuna maandishi 'fedha halali kwa malipo ya Shilingi.....' Fikiria mfano huu, Tanzania kuna watu 60m na wanaiamini na kuithamini Tsh. Rwanda wana watu 11m nao wanaiamini na kuithamini pesa yao. Kuna nchi zina watu 2m na zingine laki kadhaa na nchi nyingine zina watu elfu kadhaa. Shuka hivyo hadi upate kuwa kila familia ya watu kadhaa ni nchi. Sasa kila familia(nchi) itengeneze pesa yake. Familia A hawezi kwenda kwa familia B kununua mbuzi au ng'ombe kwa kutumia pesa yake sababu familia B hawaiamini, nao wana pesa yao, familia C nao wanayo yao na D nao wanayo yao. Imani ndiyo inaipa pesa thamani.

Kwa hiyo ukienda kwenye kiini kabisa, pesa tunazotumia sasa ni makaratasi matupu na ndiyo maana watu wakipoteza imani nazo huwa zinashuka thamani kwa kasi

2. Serikali huwa zinatengeneza pesa hizo kutoka hewani tu.

Kuna kipindi Iddi Amin(RIP) aliambiwa kuwa nchi imepigika haina hela za kulipa mishahara yeye akawajibu "kachapisheni muwalipe" zamani nilimuona mjinga lakini kumbe ndivyo mambo yalivyo. Serikali huchapisha pesa zinavyojisikia bila kuulizwa na yeyote. Pengine ili kuepuka hili ndiyo maana wanasema benki kuu ya Marekani haimilikiwi na serikali. Serikali haiwezi kuwa kwenye shida halafu inauwezo wa kuchapisha pesa na isichapishe. Kuchapisha kupita kiasi kunaweza leta inflation lakini mara nyingi serikali za kidemokrasia hazijali hayo.

3. Serikali zinatengeneza pesa kutoka hewani kisha zinatukopesha kwa riba.

Baada ya serikali kutengeneza pesa kutoka kwa hewa wanazikopesha benki. Benki nazo wanakopesha watu. Kwa hiyo kama benki kuu/ serikali inachaji riba ya 10% benki iliyokopeshwa bilioni moja itatakiwa kurudisha bilioni moja na milioni 100. Kama benki nao wanaenda kukopesha wananchi kwa asilimia 20 maana yake wananchi watatakiwa kurudisha Tsh bilioni 1.2. sasa jiulize hii milioni 200 imetoka wapi? Yaani unaingiza noti za elfu kumikumi laki moja halafu unataka zirudi laki moja na ishirini, hizi noti elfu ishirini zinatoka wapi? Hapa ndiyo maana watu hufirisika na dhamana zao kuuzwa, ni kama upatu mmoja mkubwa.

Tujadili.
 
mada fikirishi kwa kiasi chake. wachumi watufafanulie maana kwa upeo wangu mimi haya maelezo yoote yanazaa swali moja tu la msingi " nini au sababu zipi au viashiria vipi vinavyoamua pesa kiasi fulani zichapishwe ? Mchapishaji au mtoa ruhusa wa pesa kuchapishwa anazuiwa na nini au sheria zipi au mamlaka ipi ili asichapishe pesa nyingi kutatua matatizo yake yanayomkabili?
 
Walio leta ela wamechangia watu kuwa wavivu bora enzi za kubadilishana tu.
Ukisema wabadilishane vitu serikali ingekuwa maskini
Imagine ikikosekana 'sense of double coincidence'?
Hapa ndio pesa inazidi vingine vyote
 
Pesa ina historia ndefu sana lakini leo napenda tujadili status iliyonayo pesa leo.

1. Pesa kama pesa haina thamani yeyote, ni makaratasi tu. Thamani ya pesa inatokana na wananchi kuamini kuwa ina thamani na serikali kutunga sheria kuwalazimisha watu kukubali kuwa pesa ina thamani. Ndiyo maana kwenye pesa kuna maandishi 'fedha halali kwa malipo ya Shilingi.....' Fikiria mfano huu, Tanzania kuna watu 60m na wanaiamini na kuithamini Tsh. Rwanda wana watu 11m nao wanaiamini na kuithamini pesa yao. Kuna nchi zina watu 2m na zingine laki kadhaa na nchi nyingine zina watu elfu kadhaa. Shuka hivyo hadi upate kuwa kila familia ya watu kadhaa ni nchi. Sasa kila familia(nchi) itengeneze pesa yake. Familia A hawezi kwenda kwa familia B kununua mbuzi au ng'ombe kwa kutumia pesa yake sababu familia B hawaiamini, nao wana pesa yao, familia C nao wanayo yao na D nao wanayo yao. Imani ndiyo inaipa pesa thamani.

Kwa hiyo ukienda kwenye kiini kabisa, pesa tunazotumia sasa ni makaratasi matupu na ndiyo maana watu wakipoteza imani nazo huwa zinashuka thamani kwa kasi

2. Serikali huwa zinatengeneza pesa hizo kutoka hewani tu.

Kuna kipindi Iddi Amin(RIP) aliambiwa kuwa nchi imepigika haina hela za kulipa mishahara yeye akawajibu "kachapisheni muwalipe" zamani nilimuona mjinga lakini kumbe ndivyo mambo yalivyo. Serikali huchapisha pesa zinavyojisikia bila kuulizwa na yeyote. Pengine ili kuepuka hili ndiyo maana wanasema benki kuu ya Marekani haimilikiwi na serikali. Serikali haiwezi kuwa kwenye shida halafu inauwezo wa kuchapisha pesa na isichapishe. Kuchapisha kupita kiasi kunaweza leta inflation lakini mara nyingi serikali za kidemokrasia hazijali hayo.

3. Serikali zinatengeneza pesa kutoka hewani kisha zinatukopesha kwa riba.

Baada ya serikali kutengeneza pesa kutoka kwa hewa wanazikopesha benki. Benki nazo wanakopesha watu. Kwa hiyo kama benki kuu/ serikali inachaji riba ya 10% benki iliyokopeshwa bilioni moja itatakiwa kurudisha bilioni moja na milioni 100. Kama benki nao wanaenda kukopesha wananchi kwa asilimia 20 maana yake wananchi watatakiwa kurudisha Tsh bilioni 1.2. sasa jiulize hii milioni 200 imetoka wapi? Yaani unaingiza noti za elfu kumikumi laki moja halafu unataka zirudi laki moja na ishirini, hizi noti elfu ishirini zinatoka wapi? Hapa ndiyo maana watu hufirisika na dhamana zao kuuzwa, ni kama upatu mmoja mkubwa.

Tujadili.
Inaniuma sana. Kwa sababu hata ufanye kazi unatoa jasho la damu lakini kama hauna economic freedom ni kama kumpigia mbuzi zeze acheze. Tutafanya mamiradi yote tunayoyajua lakini kama pesa hatuimiliki bado kazi bure
 
Inaniuma sana. Kwa sababu hata ufanye kazi unatoa jasho la damu lakini kama hauna economic freedom ni kama kumpigia mbuzi zeze acheze. Tutafanya mamiradi yote tunayoyajua lakini kama pesa hatuimiliki bado kazi bure
Kwa maana pesa yetu iko controlled na mataifa makubwa
 
Lakini makaratasi ya marekani yana power zaidi kuliko ya tanzania. Unaweza elezea kwann
Kuna sababu nyingi sana zinazo sababisha pesa ya nchi fulani kuwa na thamani kuliko pesa ya nchi nyingine.

Moja ya sababu hizo ni, supply, demand, inflation, n.k
Sasa ili ujue ni kwanini US dollar ina thamani zaidi ya Tsh, kwanza ni lazima ujue economic history ya USA. Kwa kifupi ni kwamba baada ya uhuru wa Marekani, 1776, walifanya mageuzi makubwa sana kiuchumi kwa kuithamanisha dollar na Dhahabu. Hii ilipelekea pesa yao kuwa na nguvu na kuliteka kabisa soko la dunia.

Isitoshe wakati huo ndiyo kwanza kulikuwa na mapinduzi makubwa ya viwanda, Wamarekani wakawa na viwanda vingi sana na kuuza bidhaa nyingi adimu kwa mataifa mengine, yakiwepo magari, ndege, silaha za kijeshi, n.k.
Kwa kifupi ni kwamba uchumi wa Marekani ulikua kwa haraka sana na nchi kutajirika wakati sisi na mataifa mengine tulikuwa gizani.

Kuna kitu kinaitwa import and export, wakati wenzetu USA wao wana export bidhaa nyingi zenye thamani kubwa, kuliko zile wanazo import, sisi Tanzania tuna import bidhaa nyingi zenye thamani kubwa kuliko zile tunazo export. Hii hupelekea sisi pesa yetu au uchumi wetu kuwa dhaifu sababu tunanunua zaidi kuliko kuuza.

Na kitu kingine kilichochangia pesa yetu kuwa dhaifu ni aina ya mfumo wa kiuchumi tuliokuwa nao. Wakati USA wao walikuwa ni CAPITALISTS, sisi tulikuwa ni SOCIALISTS.

Hii ni mifumo miwili inayokinzana, mfumo wa Capitalism unaongozwa na kitu inaitwa "supply and demand", ni rahisi kufanya biashara kwa uhuru na faida kubwa kwenye mfumo huu kuliko mfumo wa "Socialism" ambapo Serikali humiliki kila kitu na kuamua kila kitu. Na hata kama tulikwisha achana na mfumo wa "Socialism" mwanzoni mwa miaka ya 90, lakini tayari tulikuwa tumechelewa sana tena sana, hasa ukilinganisha na jirani zetu Wakenya.

Hivyo basi kutokana na sababu hizo chache nilizozitaja, hiyo imepelekea sisi pesa yetu kuwa dhaifu ukilinganisha na dollar ya Marekani.
 
Kuchapisha pesa nigharama kubwa mkuu...
 
Pesa ina historia ndefu sana lakini leo napenda tujadili status iliyonayo pesa leo.

1. Pesa kama pesa haina thamani yeyote, ni makaratasi tu. Thamani ya pesa inatokana na wananchi kuamini kuwa ina thamani na serikali kutunga sheria kuwalazimisha watu kukubali kuwa pesa ina thamani. Ndiyo maana kwenye pesa kuna maandishi 'fedha halali kwa malipo ya Shilingi.....' Fikiria mfano huu, Tanzania kuna watu 60m na wanaiamini na kuithamini Tsh. Rwanda wana watu 11m nao wanaiamini na kuithamini pesa yao. Kuna nchi zina watu 2m na zingine laki kadhaa na nchi nyingine zina watu elfu kadhaa. Shuka hivyo hadi upate kuwa kila familia ya watu kadhaa ni nchi. Sasa kila familia(nchi) itengeneze pesa yake. Familia A hawezi kwenda kwa familia B kununua mbuzi au ng'ombe kwa kutumia pesa yake sababu familia B hawaiamini, nao wana pesa yao, familia C nao wanayo yao na D nao wanayo yao. Imani ndiyo inaipa pesa thamani.

Kwa hiyo ukienda kwenye kiini kabisa, pesa tunazotumia sasa ni makaratasi matupu na ndiyo maana watu wakipoteza imani nazo huwa zinashuka thamani kwa kasi

2. Serikali huwa zinatengeneza pesa hizo kutoka hewani tu.

Kuna kipindi Iddi Amin(RIP) aliambiwa kuwa nchi imepigika haina hela za kulipa mishahara yeye akawajibu "kachapisheni muwalipe" zamani nilimuona mjinga lakini kumbe ndivyo mambo yalivyo. Serikali huchapisha pesa zinavyojisikia bila kuulizwa na yeyote. Pengine ili kuepuka hili ndiyo maana wanasema benki kuu ya Marekani haimilikiwi na serikali. Serikali haiwezi kuwa kwenye shida halafu inauwezo wa kuchapisha pesa na isichapishe. Kuchapisha kupita kiasi kunaweza leta inflation lakini mara nyingi serikali za kidemokrasia hazijali hayo.

3. Serikali zinatengeneza pesa kutoka hewani kisha zinatukopesha kwa riba.

Baada ya serikali kutengeneza pesa kutoka kwa hewa wanazikopesha benki. Benki nazo wanakopesha watu. Kwa hiyo kama benki kuu/ serikali inachaji riba ya 10% benki iliyokopeshwa bilioni moja itatakiwa kurudisha bilioni moja na milioni 100. Kama benki nao wanaenda kukopesha wananchi kwa asilimia 20 maana yake wananchi watatakiwa kurudisha Tsh bilioni 1.2. sasa jiulize hii milioni 200 imetoka wapi? Yaani unaingiza noti za elfu kumikumi laki moja halafu unataka zirudi laki moja na ishirini, hizi noti elfu ishirini zinatoka wapi? Hapa ndiyo maana watu hufirisika na dhamana zao kuuzwa, ni kama upatu mmoja mkubwa.

Tujadili.
MOSI: Kuna tofauti kubwa sana kati ya "Worth" na "Value" ukiwa unaongelea socio-economics.

2. Pesa zote duniani zinakuwa regulated na Standard International Financial Acts. As long as nchi ina heshimu Regulations hizo, haiwezi chapisha pesa "HALALI" inavuojisikia.

3. Naunga hoja ila nahisi ume-simplify mno uhalisia wa mzunguko wa pesa Mkuu Lycaon.
Umeangalia pesa tu kuwa ndo chanzo cha kulipa madeni ukisahau factors zingine kama collateral assets.

 
Zinakua regulayed na na hao standard financial acts..... ni kwa kiasi gani tunawaamini wana regulate kwa haki. Maana swala limekaa kiimani
MOSI: Kuna tofauti kubwa sana kati ya "Worth" na "Value" ukiwa unaongelea socio-economics.

2. Pesa zote duniani zinakuwa regulated na Standard International Financial Acts. As long as nchi ina heshimu Regulations hizo, haiwezi chapisha pesa "HALALI" inavuojisikia.

3. Naunga hoja ila nahisi ume-simplify mno uhalisia wa mzunguko wa pesa Mkuu Lycaon.
Umeangalia pesa tu kuwa ndo chanzo cha kulipa madeni ukisahau factors zingine kama collateral assets.

 
Back
Top Bottom