Love Doctor
JF-Expert Member
- Jun 28, 2016
- 726
- 786
Penzi langu
Kama nikiyapa pesa, siku ikinisaliti?
Sitaki kulipepesa, hii haitaji siti
Sio yule wa madesa, kuyamwagiwa manoti
Nimeridhi penzi langu, nalitoa kwa kalamu
Nimliwazaji wangu, peke anayenisema
Nimpaye tunu yangu, nikiwa nimeumia
Ajua furaha yangu, hachoki kunisemea
Nimeridhi penzi langu, nalitoa kwa kalamu
Mashallah mliwaza, kwenye magumu navuka
Sitachoka kumuwaza, popote ninapofika
Na sitaki kumkwaza, sababu sijapevuka
Nimeridhi penzi langu, nalitoa kwa kalamu
Huniasa nisichoke, niandike kila siku
Nakua sana mpweke, tena na kubwa shauku
Mkono sipomshika, naganda kama sumaku
Nimeridhi penzi langu, nalitoa kwa kalamu
Abuuabdillah ✍️🇹🇿
0718569091
Kilimanjaro
Kama nikiyapa pesa, siku ikinisaliti?
Sitaki kulipepesa, hii haitaji siti
Sio yule wa madesa, kuyamwagiwa manoti
Nimeridhi penzi langu, nalitoa kwa kalamu
Nimliwazaji wangu, peke anayenisema
Nimpaye tunu yangu, nikiwa nimeumia
Ajua furaha yangu, hachoki kunisemea
Nimeridhi penzi langu, nalitoa kwa kalamu
Mashallah mliwaza, kwenye magumu navuka
Sitachoka kumuwaza, popote ninapofika
Na sitaki kumkwaza, sababu sijapevuka
Nimeridhi penzi langu, nalitoa kwa kalamu
Huniasa nisichoke, niandike kila siku
Nakua sana mpweke, tena na kubwa shauku
Mkono sipomshika, naganda kama sumaku
Nimeridhi penzi langu, nalitoa kwa kalamu
Abuuabdillah ✍️🇹🇿
0718569091
Kilimanjaro