venister 98
Member
- Jun 11, 2022
- 9
- 9
Mara baada ya kutokuwa na maelewano mazuri na mpenzi wangu kwa muda mrefu usiopungua mwaka na miezi kadhaa nilijaribu kutafuta suluhu kadri ya uwezo wangu na haikufua dafu.
Nilipata msongo wa mawazo juu ya suala hilo kwani sikuwahi kufanya udanganyifu, hata kumjibu vibaya lakini amebadilika na hajali.
Kama mwanamke nilimpenda sana kiasi ambacho kilikuwa mtaji na fimbo ya kunijibu alivyotaka, hata mawasiliano alikuwa akinipigia simu mara moja kwa mwezi akijiskia wakati mwingine mwezi unaisha kabisa.
Kila niliyemuomba ushauri aliniambia huyo atakua yupo kwenye mahusiano na mwanamke mwingine, wewe kakufanya wa akiba.
Nilikaa chini nikawaza mengi ikiwemo kwa nini niendelee kuwa na mtu anayenipa msongo wa mawazo na chanzo sikujui ? Je, atabadilika lini? Naendelea kumng'ang'ania hadi lini? .
Waswahili wanasema "Uvumilivu aliachiwa mbuzi". Nilipata suluhisho la kumuacha kwa kukaa kimya, kwani nilijiona mwenye kulazimisha mawasiliano.
Baada ya kuona nimebadilika alituma ujumbe mfupi wa simu akitaka tuonane, tuzungumze, kitu ambacho kilishindikana ndani ya mwaka na miezi kadhaa hata hivyo moyo umeshakata tamaa, aliendelea kunisumbua baadaye alikaa ila baadaye alitulia.
Katika harakati za kutafuta maisha nikakutana na mwanaume mwingine ambaye tulianza urafiki. Na kwa kuwa koloni lilikuwa halina mbepari basi, yeye alijipatia mwanya wa kuanzisha mahusiano yasiyo rasmi. Tulidumu kwa muda wa miezi 5 ila tulitengana kwa sababu za kikazi.
Hata hivyo baada ya muda kupita nilimpata mpenzi mwingine, tunapendana na ananijali sana. Kwa kuwa yule rafiki yangu tulikuwa tumezoea uwazi nilimwambia mimi nimempata mpenzi, basi alinipongeza.
Mimi nampenda sana mpenzi wangu mpya ila kinachonichosha ni kwamba nimekua nikimuota yule mpenzi wa mpito / niliyeanzisha naye mahusiano yasiyo rasmi.
Hali hii inanifanya nijisikie vibaya na ninaona kama namkosea mpenzi niliye naye. Je, tatizo ni nini? naomba ushauri nifanyeje niache kumuota mpenzi wa mpito nikiwa kwenye penzi jipya?
Ahsante.
Nilipata msongo wa mawazo juu ya suala hilo kwani sikuwahi kufanya udanganyifu, hata kumjibu vibaya lakini amebadilika na hajali.
Kama mwanamke nilimpenda sana kiasi ambacho kilikuwa mtaji na fimbo ya kunijibu alivyotaka, hata mawasiliano alikuwa akinipigia simu mara moja kwa mwezi akijiskia wakati mwingine mwezi unaisha kabisa.
Kila niliyemuomba ushauri aliniambia huyo atakua yupo kwenye mahusiano na mwanamke mwingine, wewe kakufanya wa akiba.
Nilikaa chini nikawaza mengi ikiwemo kwa nini niendelee kuwa na mtu anayenipa msongo wa mawazo na chanzo sikujui ? Je, atabadilika lini? Naendelea kumng'ang'ania hadi lini? .
Waswahili wanasema "Uvumilivu aliachiwa mbuzi". Nilipata suluhisho la kumuacha kwa kukaa kimya, kwani nilijiona mwenye kulazimisha mawasiliano.
Baada ya kuona nimebadilika alituma ujumbe mfupi wa simu akitaka tuonane, tuzungumze, kitu ambacho kilishindikana ndani ya mwaka na miezi kadhaa hata hivyo moyo umeshakata tamaa, aliendelea kunisumbua baadaye alikaa ila baadaye alitulia.
Katika harakati za kutafuta maisha nikakutana na mwanaume mwingine ambaye tulianza urafiki. Na kwa kuwa koloni lilikuwa halina mbepari basi, yeye alijipatia mwanya wa kuanzisha mahusiano yasiyo rasmi. Tulidumu kwa muda wa miezi 5 ila tulitengana kwa sababu za kikazi.
Hata hivyo baada ya muda kupita nilimpata mpenzi mwingine, tunapendana na ananijali sana. Kwa kuwa yule rafiki yangu tulikuwa tumezoea uwazi nilimwambia mimi nimempata mpenzi, basi alinipongeza.
Mimi nampenda sana mpenzi wangu mpya ila kinachonichosha ni kwamba nimekua nikimuota yule mpenzi wa mpito / niliyeanzisha naye mahusiano yasiyo rasmi.
Hali hii inanifanya nijisikie vibaya na ninaona kama namkosea mpenzi niliye naye. Je, tatizo ni nini? naomba ushauri nifanyeje niache kumuota mpenzi wa mpito nikiwa kwenye penzi jipya?
Ahsante.