PENDEKEZO: Tuwe na VAR yetu ya kivyetu vyetu

kidi kudi

JF-Expert Member
May 17, 2011
2,419
1,981
Kwa muda mrefu vilabu vyetu, wadau na mashabiki wamekuwa wakilia na kulalamikia sana maamuzi yanayoamuliwa na waamuzi wetu kwenye mchezo pendwa wa soka ama kandanda au kabumbu kama linavyofahamika na wengi.

Nimekuwa nikijiuliza hili suala la wenzetu hasa wale wa nchi za Ulaya walivyofanikiwa kuleta hii teknolojia ya matumizi ya VAR katika kusaidia waamuzi kufanya maamuzi hasa yale yanayoonekana yana utata, kwamba kwa huku kwetu kwenye ligi yetu ya VPL hatuwezi na sisi kuja na VAR yetu kivyetu vyetu tukipata msaada toka picha za video za AZAM TV hasa kwa zile channel zinazorusha mubashara hizi mechi zetu?

Napendekeza msimu ujao viongezeke vitu viwili kama ifuatavyo;
1. Awepo refa mwingine wa ziada ndani ya gari la kurushia matangazo za AZAM ambae kazi yake itakuwa ni kuangalia tena video mgando ya tukio lenye utata na kisha kutoa taarifa hiyo haraka kwa mwamuzi wa nje mezani (fourth official) ili nae awasiliane na mwamuzi wa kati, kisha

2. Pawepo na ka flat screen hata ka 32" ambako katakua hapo nje kwa huyo 'fourth official' ambako katakuwa kanaonyesha mchezo husika live toka kwenye gari la matangazo la AZAM maalum kwa mwamuzi wa kati kwenda kujiridhisha na maamuzi aliyo/atakayo yafanya (kama vile ambavyo wenzetu wafanyavyo hukooooo majuuu).

Hebu tujaribu kuanzia hapo naamini kwa kiasi fulani malalamiko yapungua kwa kiasi fulani.

NINAPENDEKEZA!
 
VAR ni technology iliyoanzia Ulaya. Sasa hiyo ya Afrika iligunduliwa lini? Ni sawa na kusema "tunatengeneza Boeing za Afrika". Gharama ipo kwenye technology.
labda nikuulize swali dogo, ni kipi kiliwafanya mashabiki na kiongozi wa Yanga kusema refarii alikataa penati ya wazi wakati Yanga ikicheza na Mbeya city kule Mbeya?
 
Ni wazo zuri na kwa taarifa tu sisi ndo wa kwanza kutumia "VAR"(ya kikwetu kwetu) kabla wazungu hawajaja nayo. Sina kumbukumbu kamili lkn ilikuwa ni mechi ya simba na yanga kama sikosei mechi ilikuwa live na ile screen ya uwanjan ilikuwa inaonesha ikatokea mchezaji ameshika mpira refa hajaona wachezaji wakamwambia angalia kule kwenye screen azam walikuwa wanairudia refa alitumia ile video kufanya maamuzi
 
inawezekana sana tu naamini wakiamua litafanyiwa kazi tu.

wakati mwingine najiuliza ni kwanini tunakuwa na malumbano yasiyo ya lazima wakati tunaweza kufanya kitu tena kwa urahisi tu tukitumia teknolojia hii hii ndogo tuliyonayo
 
Wazo zuri sana,

ila hako ka-tv kanchi 32 katavunjiliwa mbali na wachezaji wa Uto maana wamekuwa ni wenye hasira sn siku za hv karibuni

Game na Mbeya City tu ilipoisha Kaseke alikuwa anataka kumtia vichwa refa, bahati nzuri Lamine Moro alimuwahi na kumdhibiti, sasa ndo waje waone kuwa kaTv kamewanyima ushindi si katapigwa funu moja na kuvunjika

Vinginevyo labda hio tv ilindwe na wale FFU muda wote
 
Ni wazo zuri na kwa taarifa tu sisi ndo wa kwanza kutumia "VAR"(ya kikwetu kwetu) kabla wazungu hawajaja nayo. Sina kumbukumbu kamili lkn ilikuwa ni mechi ya simba na yanga kama sikosei mechi ilikuwa live na ile screen ya uwanjan ilikuwa inaonesha ikatokea mchezaji ameshika mpira refa hajaona wachezaji wakamwambia angalia kule kwenye screen azam walikuwa wanairudia refa alitumia ile video kufanya maamuzi
Naikumbuka hii game, nilikuwepo uwanjani.
 
Wazo zuri sana,

ila hako ka-tv kanchi 32 katavunjiliwa mbali na wachezaji wa Uto maana wamekuwa ni wenye hasira sn siku za hv karibuni

Game na Mbeya City tu ilipoisha Kaseke alikuwa anataka kumtia vichwa refa, bahati nzuri Lamine Moro alimuwahi na kumdhibiti, sasa ndo waje waone kuwa kaTv kamewanyima ushindi si katapigwa funu moja na kuvunjika

Vinginevyo labda hio tv ilindwe na wale FFU muda wote
hapo lile rungu la kufungiwa maisha lifanye kazi kisawasawa....mpira ni burudani sio ugomvi
 
  • Thanks
Reactions: tyc
Wazk zuri, hata mimi nishawahi kuwaza hivyo, nikaleta na uzi humu

Ukisoma comments za wengi utagundua waafrika hatujiamini, hatuamini mawazo yetu,hatuamin kama tunaweza kutoka kikwetu kwetu.
 
Itabidi tuwapatie kandarasi misukule wa kule gamboshi & wale waganga wa TV asilia kuimplement VAR kwenye VPL
 
Wazk zuri, hata mimi nishawahi kuwaza hivyo, nikaleta na uzi humu

Ukisoma comments za wengi utagundua waafrika hatujiamini, hatuamini mawazo yetu,hatuamin kama tunaweza kutoka kikwetu kwetu.
kumbe ulishawahi kuwaza kitu kama hiki? nafikiri wakati umefika kuliangalia kwa mapana suala hili maana kelele ni nyingi na sioni mabadiliko kwa waamuzi wetu
 
Itabidi tuwapatie kandarasi misukule wa kule gamboshi & wale waganga wa TV asilia kuimplement VAR kwenye VPL
likifanyiwa kazi hili pendekezo nina hakika kuna klabu zitaongoza maandamano ya kuipinga maana janja janja kwao ndio mtaji
 
Sidhani kama itafanikiwa maana naliona tatizo kwa azam tv pia. Azam tv hawana kamera nyingi zitakazo fanikisha kurudia tukio na kuonekana kwa usahihi zaidi. Mfano tukio la goli la yanga dhidi ya mbeya city mpaka leo hii hakuna mwenye uhakika kama ule mpira ulivuka mstari au la maana marudio ya azam tv hakuna sehemu walipo onyesha kama mpira ulivuka mstari au la.

Matukio ni mengi tu azam tv wakirudia hayaonekani vizuri.Kwa hiyo ili angalau twende sawa Azam tv waongeze kwanza kamera.
 
kumbe ulishawahi kuwaza kitu kama hiki? nafikiri wakati umefika kuliangalia kwa mapana suala hili maana kelele ni nyingi na sioni mabadiliko kwa waamuzi wetu
Yes niliwaza, nikaweka bandiko hapo, nikahisi labda viongozi wetu bongolala wanaweza wakapita wakakopi, ikawa faida kwa soka letu.
 
Back
Top Bottom