Mdaiwa-Sugu
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 284
- 912
CHADEMA kina sera nzuri zenye kukosha na kukonga nyoyo za watanzania ingawa muda wa nusu saa anaotumia Tundu kujinadi ni mchache sana kiasi kwamba mambo mengi ya muhimu(sera) yaliyomo kwenye ilani hayagusii kutokana na kupanda jukwaani muda ukiwa umeenda halikadhalika kutumia muda mfupi kujinadi.
Hivyo basi niungane na watanzania wote wapenda mabadiliko kushauri au kupendekeza jambo moja, kuwa;
Mgombea wetu wa kiti cha Urais, bw. Tundu Antipas Lissu atumie muda wa kutosha angalau kati ya masaa mawili au moja na nusu kuchambua, kueleza na kunadi kinaga ubaga sera zinazobeba ilani ya chama.
kutumia muda mwingi kunadi sera za chama kutasaidia kujenga ushawishi na wananchi kuelewa kwa kina juu ya nini bw. Tundu Antipas amekusudia kuwafanyia endapo wakimpa ridhaa ya kuwaongoza 2020 - 2025.
Hivyo basi niungane na watanzania wote wapenda mabadiliko kushauri au kupendekeza jambo moja, kuwa;
Mgombea wetu wa kiti cha Urais, bw. Tundu Antipas Lissu atumie muda wa kutosha angalau kati ya masaa mawili au moja na nusu kuchambua, kueleza na kunadi kinaga ubaga sera zinazobeba ilani ya chama.
kutumia muda mwingi kunadi sera za chama kutasaidia kujenga ushawishi na wananchi kuelewa kwa kina juu ya nini bw. Tundu Antipas amekusudia kuwafanyia endapo wakimpa ridhaa ya kuwaongoza 2020 - 2025.