Pendekezo: Jecha Salimu Jecha ashitakiwe kuvunja katiba na sheria

Pendekezo: Jecha Salimu Jecha ashitakiwe kuvunja katiba na sheria

Joseph Mshinga

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2014
Posts
232
Reaction score
143
Na:Joseph Mshinga.

Msisitizo wangu uko palepale kuwa Mshindi halali atangazwe na si vinginevyo. Hakuna cha kutangazwa hali ya hatari, sijui habari za katiba mpya mara serikali ya umoja wa kitaifa . Hakuna sababu kwa yote haya. Mshindi atangazwe.

Jecha ashitakiwe.
1.Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na ile ya Zanzibar ya mwaka 1984 inaitaka tume ya uchaguzi ya Zanzibar(ZEC) kushauriana mara kwa Mara katika kutekeleza majukumu yake na tume ya uchaguzi ya Taifa(NEC)

Kitendo cha Jecha kufanya maamuzi ya kufuta uchaguzi bila takwa la kikatiba la kushauriana na tume ya Taifa ni dhahiri kuwa amekiuka na kuvunja katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katiba ya Zanzibar. Hivyo anapaswa kufunguliwa kesi ya kuvunja katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Zanzibar.

Ieleweke kuwa mashauriano yanayotakiwa kufanyika ni kati ya ZEC na NEC. isije kueleweka vibaya kuwa ni kati ya Jecha na NEC. hata kama Jecha alifanya mashauriano na NEC na mashauriano hayo hayajaripotiwa bado hayo si mashauriano ya ZEC na NEC bali ni mashauriano ya Jecha na NEC ambayo hayatambuliki kikatiba wala kisheria. Jecha ni mmoja ya wajumbe wa ZEC akiwa Mwenyekiti na ili ionekane kuwa ZEC imeshiriki basi uamuzi ule ulipaswa kuwa umejadiliwa kwanza ndani ya ZEC kitu ambacho hakikufanyika maana wajumbe walishakana tayari.

Hivyo Jecha kavunja katiba ya nchi na anapaswa kufunguliwa mshitaka.Hili ni kosa la kwanza.

Ieleweke pia kuwa Tume ya uchaguzi ya Zanzibar na NEC ya Taifa hazina kinga ya kutoshitakiwa. Vivyo hivyo hata Jecha hana kinga ya kutokushitakiwa juu ya uvunjaji wa katiba na sheria alioufanya. nasisitiza kuwa hana kinga ya kutoshitakiwa. Kisichoruhusiwa ni matokeo kuhojiwa mahakamani mara baada ya kutangazwa lakini si kushitakiwa kwa TUME yenyewe wala wajumbe na mwenyekiti wake.Hivyo sheria ichukue mkondo wake kwa Jecha.

2.Sheria ya uchaguzi ya Zanzibar namba 11 ya mwaka 1984 imeweka sharti kuwa uamuzi wowote wa tume ya Zanzibar ni sharti uwe umefanyika kwenye Kikao halali na tena kiwe na akidi inayotakiwa.

Kwa kuwa hakuna kikao cha Tume kilichofanyika kujadili na kuamua kufutwa kwa uchaguzi basi hili ni kosa la pili kufanywa na Jecha kwa kuvunja kifungu hiki cha sheria. Hivyo anapaswa kufunguliwa mashitaka kwa kuvunja kifungu hiki cha sheria ya uchaguzi.

3.Katika tamko lake la kufuta uchaguzi Jecha alikaririwa akisema kuwa kwa mamlaka aliyonayo basi anafuta uchaguzi wa Zanzibar.

Kwa kuwa Katiba ya Zanzibar na sheria ya uchaguzi Zanzibar hazimpi mamlaka mwenyekiti wa Tume kufuta uchaguzi basi atakuwa ametenda kosa kwa kukiuka sheria na kujipatia mamlaka ambayo hana.Anapaswa kufunguliwa mashitaka kwa kujipachika mamlaka ambayo hana kisheria wala kikatiba.

Mwisho naendelea kusistiza kuheshimiwa kwa maamuzi halali ya Wazanzibar.

Joseph Mshinga
12/11/2015.
 
Msimlaumu..Jecha alilazimishwa kufuta uchaguzi.. hayakuwa matakwa yake.. Huwezi kupinga amri ya amir jeshi mkuu
 
Ashitakiwe na nani?!, kwa kosa lipi wakati ndio kwanza ameinusuru serikali, yaani kesi ya nyani upeleke kwa ngedere?!.

Wenzako kila siku zisipotosha, zinatosheshwa!, this time pia hazikutosha, ila kabla ya zoezi la kutoshesha halijafanyika!, yule ambae kwake zilitosha, akatoa taarifa kuwa zimetosha hivyo juhudi za kutoshesha zikashindikana!.

Alichofanya ni kuliko kumtangaza, bora kuufuta wakose wote!.

Pasco
 
Msimlaumu..Jecha alilazimishwa kufuta uchaguzi.. hayakuwa matakwa yake.. Huwezi kupinga amri ya amir jeshi mkuu
kwanza yeye ashitakiwe kwa kuwa hakuna ushahidi kuwa alilazimishaa basi yeye aubebe mzigo wote. Kama akisema alilazimishwa basi litakuwa kosa jingine katenda na shitaka hilo liunganishwe kwa kuvunja kifungu kingine kinachokataza tume kupokea shinikizo toka kwa mtu yeyote.
 
Ashitakiwe na nani?!, kwa kosa lipi wakati ndio kwanza ameinusuru serikali, yaani kesi ya nyani upeleke kwa ngedere?!.

Wenzako kila siku zisipotosha, zinatosheshwa!, this time pia hazikutosha, ila kabla ya zoezi la kutoshesha halijafanyika!, yule ambae kwake zilitosha, akatoa taarifa kuwa zimetosha hivyo juhudi za kutoshesha zikashindikana!.

Alichofanya ni kuliko kumtangaza, bora kuufutaa wakose wote!.

Pasco

makosa nimeyasema.

kesi hiyo inaweza kufunguliwa na wagombea ama wapiga kura. Ila si kesi ya kushughulikia mtanziko wa kisiasa Zanzibar bali ni kesi ya kumwajibisha Jecha hata baada ya suluhu kuwa imepatikana ili kuwe na fundisho kwa wakati mwingine. Bora angebwaga manyanga.
 
Tume ya uchaguzi Zanzibar ni huru. Na uamuzi wao ni wa mwisho.

Huna kesi ya uvunjaji katiba hapo.
 
Huyu ajuza ni zaidi ya ukimwi namchukia kuliko killer yoyote ktk dunia hii.laaana za Allah ziwe juu ......
 
huyo Faiza hajitambui, kazoea vya kunyonga, vya kuchinja haviwezi,
ukiwa na akili timamu ukaunga mkono uchafu wa Jecha itabidi uchunguzwe akili yako.
 
Tume ya uchaguzi Zanzibar ni huru. Na uamuzi wao ni wa mwisho.

Huna kesi ya uvunjaji katiba hapo.
Tume huru mbona imeshindwa kutangaza mshindi au demokrasia ni ccm kushinda tuu?
 
huyo Faiza hajitambui, kazoea vya kunyonga, vya kuchinja haviwezi,
ukiwa na akili timamu ukaunga mkono uchafu wa Jecha itabidi uchunguzwe akili yako.

Ni wa kupuuza tuu huyo.
 
Mimi napendekeza jecha aajiliwe na bodi ya ligi kuu ya england ili afute matokeo yote ya Chelsea msimu huu......(ni mtazamo tu)
 
Ashitakiwe na nani?!, kwa kosa lipi wakati ndio kwanza ameinusuru serikali, yaani kesi ya nyani upeleke kwa ngedere?!.

Wenzako kila siku zisipotosha, zinatosheshwa!, this time pia hazikutosha, ila kabla ya zoezi la kutoshesha halijafanyika!, yule ambae kwake zilitosha, akatoa taarifa kuwa zimetosha hivyo juhudi za kutoshesha zikashindikana!.

Alichofanya ni kuliko kumtangaza, bora kuufuta wakose wote!.

Pasco
Mkuu Pasco uko sahihi huwezi kupeleka kesi ya ngedere kwa nyani hata mkienda mahakamani maamuzi yatakuwa ndo hayo lakini walichokifanya ZEC ni hujuma za wapi kama zile NEC tanzania lakini huu uonevu una mwisho wake.



HAKUNA AMANI BILA HAKI
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Pasco uko sahihi huwezi kupeleka kesi ya ngedere kwa nyani hata mkienda mahakamani maamuzi yatakuwa ndo hayo lakini walichokifanya ZEC ni hujuma za wapi kama zile NEC tanzania lakini huu uonevu una mwisho wake.



HAKUNA AMANI BILA HAKI


sijaeleweka? sipendekezi kutatua mgogoro wa matokeo kupitia kesi.

matokeo nimesema mshindi atangazwe na baada ya hapo Jecha si wa kuacha hivihivi lazima ashitakiwe kwa makosa aliyofanya yeye kama yeye. Hata kama kesi itaenda kwa ngedere lakini itatoa picha jinsi mahakama zetu zinavyofanya kazi,lakini lazima haki ya Jecha ikapiganiwa mahakamani kwa makosa aliyofanya na si kukata tamaa mapema.

Urais uamuliwe kwa njia ya kidiplomasia.
 
Last edited by a moderator:
ama kweli ccm ni noma. walipoona kule zenji hapasomeki wakaweka mpira kwapani kabla ya dakika 90 za mchezo, du. hii aibu ya karne. nawashauri wasiwe wanatumia kodi zetu kufanya uchaguzi ambao kiuhalisia hawana mpango wa kuheshimu maamzi ya wananchi.
 
Back
Top Bottom