tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
Tanzania tuna safari ndefu ya kwenda mpaka kufikia ukombozi kamili. Sasa hivi nimeanza kuelewa kwanini Mwalimu Julius Nyerere alikuwa anapambana sana Watanzania tuondokane na ujinga.
Ona leo hii kinachoendelea, kijana wa Kitanzania mwenye akili timamu ananunuliwa kwa boflo tano na maji na kukiri kabisa kwa kupatiwa vitu hivyo basi kiongozi anastahili kuendelea kutawala tena!
Hii inanipa picha kwamba Watanzania asilimia kubwa bado tunateseka na ujinga, hatujui haki zetu, hatujui nguvu yetu kwa viongozi wetu kama Watanzania, na wala hatuna uelewa wowote kuhusu utawala.
Jaribu kufikiria kwa akili za vijana kama hawa, hivi kweli wataelewa ukiwaambia kuhusu, DP World? wataelewa ukiwaambia kuhusu utakatishaji wa mabilioni ya mapesa unaoendelea nchini?
Utakuja kujua kuwa kiwango cha kufikiria kipo chini sana.
Akipata maarifa, Mjinga si mjinga tena.
Kama kweli haya ni mapokezi halali ya Samia Simiyu CCM inaogopa nini kuicha Tume ya uchaguzi kuwa huru?
Ona leo hii kinachoendelea, kijana wa Kitanzania mwenye akili timamu ananunuliwa kwa boflo tano na maji na kukiri kabisa kwa kupatiwa vitu hivyo basi kiongozi anastahili kuendelea kutawala tena!
Hii inanipa picha kwamba Watanzania asilimia kubwa bado tunateseka na ujinga, hatujui haki zetu, hatujui nguvu yetu kwa viongozi wetu kama Watanzania, na wala hatuna uelewa wowote kuhusu utawala.
Jaribu kufikiria kwa akili za vijana kama hawa, hivi kweli wataelewa ukiwaambia kuhusu, DP World? wataelewa ukiwaambia kuhusu utakatishaji wa mabilioni ya mapesa unaoendelea nchini?
Utakuja kujua kuwa kiwango cha kufikiria kipo chini sana.
Akipata maarifa, Mjinga si mjinga tena.
Kama kweli haya ni mapokezi halali ya Samia Simiyu CCM inaogopa nini kuicha Tume ya uchaguzi kuwa huru?