AUGUSTINO CHIWINGA
JF-Expert Member
- Apr 23, 2017
- 220
- 689
Kipimo cha uwezo wa sehemu ya kazi hupimwa kwa kitu kinachoitwa Perfomance appraisal. Tangu ashike madaraka Rais wa Tanzania wa awamu ya sita ni wazi amescore credit zote 100.
Mosi kuweza kumaintain uendelezwaji wa miradi mikubwa ya kimkakati kama vile SGR na Bwawa la Nyerere huku makusanyo ya kodi yakipaa mpaka kufikia Trilioni 5 ni uwezo mkubwa sana alionao.Trilioni Tanio hizo ndizo zinaletwa huku vijijijni na mitaani kuja kutatua changamoto mbalimbali za wananchi.
Uwezo mwingine mkubwa alionesha ni ule wa kumwaga ajira kwenye sekta mbalimbali za umma kama vile polisi, ,magereza na zimamoto. Sasa kile kilio cha ukosefu wa ajira Rais Samiah amekipatia mwarobaini wake. Jambo hili linaenda sambamba na uimarishaji wa sekta binafsi ambapo ndani ya miezi mitano tu jumla ya biashara zenye thamani ya Bilion 3 zimeweza kusajili jambo ambalo limeongeza ajira kwa vijana wengi.
Achilia mbali miradi mingi midogomidogo na ya kati inayoendelea kote nchini kama vile barabara za majimbo ambazo kupitia TARURA zimeingizwa shillingi milioni 500 mpaka Bilioni moja kote nchini.Nchi inanawiri na kustawi maendeleo yanazidi kupatikana tena kwa kasi kubwa bila ya kusahau bei nzuri za mazao yao waliyoyapata wakulima mwaka huu.
Rais wetu ni mchapakazi hodari makini mwenye huruma mpole lakini mkali kwenye mambo ya hovyo . Watanzania wana imani nae, mama atatuvusha.
Mosi kuweza kumaintain uendelezwaji wa miradi mikubwa ya kimkakati kama vile SGR na Bwawa la Nyerere huku makusanyo ya kodi yakipaa mpaka kufikia Trilioni 5 ni uwezo mkubwa sana alionao.Trilioni Tanio hizo ndizo zinaletwa huku vijijijni na mitaani kuja kutatua changamoto mbalimbali za wananchi.
Uwezo mwingine mkubwa alionesha ni ule wa kumwaga ajira kwenye sekta mbalimbali za umma kama vile polisi, ,magereza na zimamoto. Sasa kile kilio cha ukosefu wa ajira Rais Samiah amekipatia mwarobaini wake. Jambo hili linaenda sambamba na uimarishaji wa sekta binafsi ambapo ndani ya miezi mitano tu jumla ya biashara zenye thamani ya Bilion 3 zimeweza kusajili jambo ambalo limeongeza ajira kwa vijana wengi.
Achilia mbali miradi mingi midogomidogo na ya kati inayoendelea kote nchini kama vile barabara za majimbo ambazo kupitia TARURA zimeingizwa shillingi milioni 500 mpaka Bilioni moja kote nchini.Nchi inanawiri na kustawi maendeleo yanazidi kupatikana tena kwa kasi kubwa bila ya kusahau bei nzuri za mazao yao waliyoyapata wakulima mwaka huu.
Rais wetu ni mchapakazi hodari makini mwenye huruma mpole lakini mkali kwenye mambo ya hovyo . Watanzania wana imani nae, mama atatuvusha.