Nilisikitika sana kusikia Mkurugenzi mkuu wa TAKUKURU Dr Edward hosea akilamimika hasa kuhusu serikali kumfunga mikono, na kuisingizia ofisi yetu tukufu ya DPP kuwa inakalia majalada ya kesi ya ofisi yake hivyo kumkwamisha. mimi nikiwa mtumishi wa ofisi ya DPP ambaye nimefanya kazi hapa kwa muda wa miaka kumi (nimeanza kabla Hosea hajawa mkurugenzi mkuu wa TAKUKURU) watu wa nje ya mfumo wanamuona Dr Hoseah ni muadilifu sana lakini watu tuliyefanya naye kazi tunamjua kivingine, naomba nitoe mfano wa kesi ya Idd Simba na kama watu wengine wanabisha nitaweka mifano mingine halisi hapa janvini, natoa ukweli ambao mtu yeyyote anayetaka anaweza kuuchunguza, sisi tumechoka kushambuliwa kwenye vyombo vya habari wakati yeye mweyewe ndiye anayeharibu kesi zake.
Mashitaka waliyoyaleta PCCB ni pamoja na mashitaka ya matumizi mabaya ya madaraka kwa kuuza hisa za UDA bila kufuata utaratibu wa ushindani na bila kuihusisha serikali na halmashauri ya jiji. Shitaka la kwanza la kusababisha hasara lilihusu TSH 320,000,000/= zilizolipwa katika account ya ndugu Idd Mohamed Simba na ndugu ROBERT KISENA na kosa la pili ni kusababisha hasara ya TSH 8,422,000,000/= kama hisa hizo zingeuzwa kwa ushindani. Msingi wa shitaka la kusababisha hasara ya TSH 320,000,000/= lilitokana na maelezo ya ROBERT KISENA kuwa alilipa fedha hizo katika account ya ndg Idd Simba namba 0210001002 iliyopo BENK M kama sehemu ya malipo ya hisa.
Makosa waliyofanya PCCB chini ya Hosea kwa kukusudia
katika hati mojawapo ya malipo ya tsh 250,000,000/= kutoka katika kampuni ya robasika Agro Product Ltd kwenda kwenye account ya Idd Simba iliyoko benk m, NDG ROBERT KISENA aliandika uongo kuwa kilikuwa kinalipwa kwa gharama ya usafiri. Hii ilikuwa inamfanya Robert kisena ambaye TAKUKURU walitaka awe shahidi wao na yeye kuwa mtuhumiwa kwani kama alikuwa hausiki na wala hajui kuwa anafanya wizi kwa nini aandike sababu za uongo kwenye hati ya malipo?, lakini hata hivyo TAKUKURU waliiondoa hati hiyo na walipotakiwa wailete imbatanishwe katika jadala la kesi walikataa, hata walipotakiwa kuleta jalada halisi (original) la kesi ili ofisi ya DPP ikague yenyewe walikataa.
Ofisi yetu ya DPP ilikuja kugundua baadae kuwa Robert kisena hakuishia kuhusika tu katika malipo hayo ya rushwa kwa ndg Iddi Simba lakini baadaye ilibainika kuwa alishiriki kumpa rushwa mkaguzi Neema Kiule ambaye ukaguzi wake ulizipatia thamani ndogo hisa za UDA ili Robert Kisena atakapokuja kununua ainunue kwa bei ndogo.
Ofisi ya DPP ilipogundua hivyo iliiagiza TAKUKURU imuongeze ndg Robert katika orodha ya watuhumiwa ili na yeye ashitakiwe pamoja na wengine kwani katika issue hii yeye ndiye aliyekuwa king maker (mtoa rushwa na mnunuzi katika bei ya chini) na bila kumuunganisha yeye serikali ingeshindwa kesi kirahisi. Pamoja na maagizo hayo TAKUKURU ilikataa kata kata kumuongeza na wala kumuita mahakamani, mtuhumiwa huyu hakufikishwa mahakamani tarehe 04/06/2013 kesi ilipohairishwa na hata tarehe 19/06/2013 kesi ilipoondolewa mahakamani. PCCB imeelekezwa imuchukue maelezo mtuhumiwa huyo na ichunguze kuhusika kwake kikamilifu na maelezo yake yaambatanishwe katika hati za mashitaka katika kesi hii, ikulu, mwanasheria mkuu, waziri wa sharia, dci pamoja na usalama wa taifa viimeelezwa sababu za kutoa kesi hii mahakamani.
Nyuma ya pazia.
Taarifa za uhakika zinaeleza kuwa Dr Edward Hosea alishapewa tsh 300,000,000/= na ndugu Robert Kisena, na kumuhakikishia kwamba hatamujumuisha kwenye watuhumia na atamtumia kama shahidi, ndiyo maana anasita kufanya kitu amabacho kinaonekana dhahiri.
Kwa nini TAKUKURU inamlinda kingmaker wa deal hili ndg Robert Kisena kiasi cha kukataa kumjumuisha katika orodha ya watuhumiwa wa sakata hili? Hosea alijibu kwanza swali hili kabla hajaanza kulalamika hovyo na kusingizia taasisi nyingine kuwa ndio zinamzuia kufanya kazi vizuri.