PCB inanisumbua naombeni ushauri

Nakumbuka mtihani wa kwanza wa A level pale tosamaganga Biology wa kwanza alikua na 17,Chemistry atleast watu walipiga C zilikuwepo ila Physics huko siongei kabisa. Lakini hili halikutukatisha tamaa wala kuwachukia walimu sababu tuliwaza tunaendaje mbele tena kama group sio mtu mmoja mmoja. Tuligundua kilitutesa matokeo ya form four tukaanza Advance tukijua tunaanzia tulipoishia form 4,tukaelewa hii ni elimu mpya na tumeanza upya ile ya O level tukaiweka chini tukaanza vyema zaidi kwa kujifunza na kuelekezana zaidi. Tunaposema kwenye makundi tunashauriana na kueleweshana, weekend refreshment muhimu nazikumbuka safari za Ipamba,Iringa mjini,Ifunda etc.
Kikubwa soma kwa malengo na chagua marafiki zako vizuri,elewa hapo umeanza upya usidanganyike na maksi za Olevel.

Mwisho wa siku future sio udaktari pekee PCB ina fursa nyingi sana sana,nimesoma PCB ila nikaenda kusoma Horticulture leo ni Business Developer wa Tanzania wa kampuni binafsi. Kikubwa soma topic ielewe tafuta past papers pitia maswali yake tu ukiona umeelewa sogea mbele.
Ukiona topic kila unavyojitahidi uielew iache soma zingine utairudia mbeleni ukiwa umecover zingine,topic ni nyingi kuliko muda ukikomaa na moja muda utakuacha
 
Habari za muda huu ndugu zangu naombeni msaada wa mawazo.

Ngoja nianze kwa maelezo mafupi kwanza nilimaliza A level - PCB miaka miwili iliyo pita na matokeo yangu hayakuwa mazuri kijumla nilikuwa na two ya 12 ambapo CHEM - C BIOS - C na PHY - S.

Nilijaribu kuomba Degree ila nilipataga Ualimu wa CHEM na BIOS. Wakati naomba degree niliomba pia na diploma ya medicine napo pia nilipata.

Kwakuwa ndoto zangu zilikuwa ni Udaktar ikanibidi niende diploma. Mwaka jana nilifanya mtihani wa NACTE na nilipata sup mbili ya clinical skills na patient care.

Nikaendelea kusoma level 5 sem 1 huku nikisubiria mwez wa 2 nichomoe supp zangu. Nikafanya mitihani ya level 5 sem 1 na supp zangu.

Juzi matokeo yakatoka level 5 sem 1 nilipata pass ya GPA ya 3.6 Ila level 4 clinical skills ikanikamata tena kwa hiyo nimepata RM ya clinical skills.

Jana Sir ametwambia wale wote wenye RM matokeo yao ya Level 5 sem 1 yatafutwa hvyo watabidi wasome tena upya baada ya kufaulu somo walilopata RM.

Kumbe waliletewa utaratibu kwanzia mwaka jana mwez wa 9 kuwa wenye supp wasiendele na level inayofuata mpaka watakapo chomoa masomo yao. Ila chuo chetu hawakutuambia kabisa hili swala awali na ada zetu walichokuwa bila kutuambia wanakuja kutuambia jana tena baada ya matokeo.

Naombeni msaada kwa haya mambo mawili la kwanza
"Kuna mtu aliniambia kwa hayo matokeo ya a level ambayo ni chem c bios c na phy s naweza pata chuo uganda hata kampala na weza pata ila inabidi nimtafute connection ya kunisaidia. Swali je kwa hayo matokeo ya a level naweza pata chuo uganda kusomea md au naweza pata nchi gani ila uwezo wa wazaz wangu mwisho ni mil 4? La pili.

"Je nifanye utaratibu gani endapo chuo kikigoma kunirudishia hela zangu au hakuna utaratibu wowote? (namaanisha hela yangu ya ada ya level 5 sem 1 ambayo ni 1.7m)".

Kama unaushauri wowote naomba unisaidie kwa kweli maana sielewi hadi muda huu na kikubwa ni muda tu ndio tatizo.

Asante sana na samahani kama nitakuwa nimetumia lugha vibaya na rm maana yake ni repeat module na supp maana yake ni supplementary
Pole sana kiongozi kusoma nje kwa 4m tena MD aiwezekani ata kidogo pambana urudie sem tu io mzee tumepitia uko nakaribia tunamaliza saizi .ila sikuizi walivowawekea under Nacte mnapata tabu kwa kwer
 
Kama kichwa cha habari hapo juu kinavyoeleza

Jamani ndugu wanaJF nilikua naomba ushauri jinsi gani nitaweza kuovercome hi depression na hii combination mana hata nikisoma naona Mambo yanaenda tofauti hususani kwenye chemistry .naomba ushauri wenu Mimi nipo kidato Cha tano
Kemia rahisi pambana solve sana maliza ngaiza zote then uje huku muhimbili usome pharmacy
 
Back
Top Bottom