The introvert
JF-Expert Member
- Sep 15, 2023
- 1,118
- 2,230
Wakuu habari za muda huu.
Ni mwaka 2025, dunia inakimbia kwa kasi kwenye suala la teknolojia, lakini sisi bado tumekwama kwenye jambo dogo la huduma ya kifedha ya mtandaoni kama PayPal.
Watanzania — hasa vijana wa kidigitali, wabunifu, wasanii, freelancers, na wafanyabiashara mtandaoni — wamefungiwa milango ya kupata kipato halali kutoka nje kwa sababu tu huduma hii muhimu kuwa haipatikani nchini.
Cha na kushangaza na kusikitisha zaidi, serikali ipo kimya, hakuna juhudi za wazi wala majadiliano yanayofanyika hata na Wizara husika ni kama imelifumbia macho hili jambo.
Na hata katika kipindi hiki cha sera na kampeni za uchaguzi mkuu, hakuna mgombea yeyote anayeonesha kuipa kipaumbele hoja hii muhimu ya uchumi wa kidigitali kwa ajili ya vijana wa Tanzania.
Ukweli ni kwamba, kutokuwepo kwa PayPal Tanzania kunaua fursa za vijana.
Wakati wenzetu wanauza sanaa, huduma, na ubunifu wao duniani kupitia mitandao, sisi tunabaki kuwa watazamaji.Mfano halisi nenda katizame Kenya 🇰🇪 tu hapo kwa jirani.
Ni wakati wa viongozi kuamka na kuangalia dunia inavyokwenda.
Wizara husika naomba mtupambanie vijana katika hili
Ni mwaka 2025, dunia inakimbia kwa kasi kwenye suala la teknolojia, lakini sisi bado tumekwama kwenye jambo dogo la huduma ya kifedha ya mtandaoni kama PayPal.
Watanzania — hasa vijana wa kidigitali, wabunifu, wasanii, freelancers, na wafanyabiashara mtandaoni — wamefungiwa milango ya kupata kipato halali kutoka nje kwa sababu tu huduma hii muhimu kuwa haipatikani nchini.
Cha na kushangaza na kusikitisha zaidi, serikali ipo kimya, hakuna juhudi za wazi wala majadiliano yanayofanyika hata na Wizara husika ni kama imelifumbia macho hili jambo.
Na hata katika kipindi hiki cha sera na kampeni za uchaguzi mkuu, hakuna mgombea yeyote anayeonesha kuipa kipaumbele hoja hii muhimu ya uchumi wa kidigitali kwa ajili ya vijana wa Tanzania.
Ukweli ni kwamba, kutokuwepo kwa PayPal Tanzania kunaua fursa za vijana.
Wakati wenzetu wanauza sanaa, huduma, na ubunifu wao duniani kupitia mitandao, sisi tunabaki kuwa watazamaji.Mfano halisi nenda katizame Kenya 🇰🇪 tu hapo kwa jirani.
Ni wakati wa viongozi kuamka na kuangalia dunia inavyokwenda.
Wizara husika naomba mtupambanie vijana katika hili