figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,895
Zoezi la aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, kukabidhi ofisi rasmi kwa Mkuu wa Mkoa huo wa sasa Aboubakar Kunenge limesogezwa mbele, hadi siku ya Jumatatu baada ya ratiba hiyo kuingiliana na ratiba zingine.
Taarifa ya kuahirishwa kwa zoezi hilo, imetolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo, ambapo hii leo Agosti Mosi, Makonda alitarajiwa kukabidhi ofisi hiyo iliyopo maeneo ya Ilala, majira ya saa 7:00 mchana.
Makonda aliondolewa kwenye nafasi hiyo siku ya Julai 15, 2020, na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, na nafasi hiyo ilichukuliwa na aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa huo.
Machi 13, 2016, Rais Magufuli alimteua Makonda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, ambapo awali kabla ya uteuzi huo alikuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni na hivyo amehudumu kwenye nafasi ya Ukuu wa Mkoa kwa zaidi ya miaka mitatu.
Kama T bag alivyomeza funguoNakumbuka alivyoteuliwa ukuu wa mkoa inasemekana gsm waliikarabati kwa takribani milioni 400. Akifikiria hilo anatamani ameze funguo.
ha ha haKama T bag alivyomeza funguo
Ina maana hajakabidhi mpaka leo?Salaam Mkuu,
Sasa Wiki mbili zimeisha baada ya aliyekuwa mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Dar kutenguliwa Cheo chake hicho baada ya yeye kuamua kugombea Ubunge wa Jimbo la Kigamboni ambapo kura zake hazikutosha.
Lakini tangu kipindi hicho hajakabidhi Funguo za Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa Mteule mpya.
Kabla ya Jumatatu anatakiwa awe amekabidhi ofisi kwa Mhe. Aboubakar Kunenge Mkuu mpya wa Mkoa wa Dar.
Kesho hakuna kazi. Je, leo atakabidhi Ofisi?
Thread
Ataanza kulia maana hachelewagi๐๐๐๐๐๐๐Nakumbuka alivyoteuliwa ukuu wa mkoa inasemekana gsm waliikarabati kwa takribani milioni 400
Akifikiria hilo anatamani ameze funguo.
Angekuwa ni mwingine, angekuwa SegereaMwana wa mfalmeBado anazo mfukonii
kwa jinsi mambo yanavyoendeshwa kindugu-ndugu chini ya awamu hii, si ajabu kukuta kumbe Makonda bado ni RC while huyu wa sasa ni proxy tu.Salaam Mkuu,
Sasa Wiki mbili zimeisha baada ya aliyekuwa mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Dar kutenguliwa Cheo chake hicho baada ya yeye kuamua kugombea Ubunge wa Jimbo la Kigamboni ambapo kura zake hazikutosha.
Lakini tangu kipindi hicho hajakabidhi Funguo za Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa Mteule mpya.
Kabla ya Jumatatu anatakiwa awe amekabidhi ofisi kwa Mhe. Aboubakar Kunenge Mkuu mpya wa Mkoa wa Dar.
Kesho hakuna kazi. Je, leo atakabidhi Ofisi?
Thread
Hiyo ofisi ni mali ya wananchi sio nyumba binafsi hivyo lazima waambiwe kila hatua kwa kinachoendelea ni sheria.Kwani haiwezekani kukabidhi kimya kimya?