Paul Makonda alitakiwa akabidhi Ofisi leo, zoezi limeahirishwa hadi Jumatatu. Je, Makonda atakanusha kugombea Kigamboni kupitia ACT-Wazalendo?

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,483
54,853
Salaam Mkuu,

Sasa Wiki mbili zimeisha baada ya aliyekuwa mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Dar kutenguliwa Cheo chake hicho baada ya yeye kuamua kugombea Ubunge wa Jimbo la Kigamboni ambapo kura zake hazikutosha.

Lakini tangu kipindi hicho hajakabidhi Funguo za Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa Mteule mpya.

Kabla ya Jumatatu anatakiwa awe amekabidhi ofisi kwa Mhe. Aboubakar Kunenge Mkuu mpya wa Mkoa wa Dar.

Kesho hakuna kazi. Je, leo atakabidhi Ofisi?

Kuna tetesi zinadai anataka ajiunge ACT-Wazalendo ili akagombee Kigamboni kama CCM hawatampitisha. Kuna Nzi amesema atamuuliza swali hilo siku ya kukabidhi Ofisi. Yajayo yanafurahisha.

Thread

=====

UPDATES; 1324HRS

Zoezi la kukabidhi Ofisi leo limeahirishwa kutokana na sababu zilizo njena uwezo wa Mkuu wa Mkoa Kunenge. Ratiba imebana sana hivyo itapangwa siku nyingine ikiwezezekana Jumatatu.

Zoezi la aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, kukabidhi ofisi rasmi kwa Mkuu wa Mkoa huo wa sasa Aboubakar Kunenge limesogezwa mbele, hadi siku ya Jumatatu baada ya ratiba hiyo kuingiliana na ratiba zingine.


Taarifa ya kuahirishwa kwa zoezi hilo, imetolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo, ambapo hii leo Agosti Mosi, Makonda alitarajiwa kukabidhi ofisi hiyo iliyopo maeneo ya Ilala, majira ya saa 7:00 mchana.

Makonda aliondolewa kwenye nafasi hiyo siku ya Julai 15, 2020, na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, na nafasi hiyo ilichukuliwa na aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa huo.

Machi 13, 2016, Rais Magufuli alimteua Makonda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, ambapo awali kabla ya uteuzi huo alikuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni na hivyo amehudumu kwenye nafasi ya Ukuu wa Mkoa kwa zaidi ya miaka mitatu.
 
Salaam Mkuu,

Sasa Wiki mbili zimeisha baada ya aliyekuwa mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Dar kutenguliwa Cheo chake hicho baada ya yeye kuamua kugombea Ubunge wa Jimbo la Kigamboni ambapo kura zake hazikutosha.

Lakini tangu kipindi hicho hajakabidhi Funguo za Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa Mteule mpya.

Kabla ya Jumatatu anatakiwa awe amekabidhi ofisi kwa Mhe. Aboubakar Kunenge Mkuu mpya wa Mkoa wa Dar.

Kesho hakuna kazi. Je, leo atakabidhi Ofisi?

Thread
Ina maana hajakabidhi mpaka leo?
 
Salaam Mkuu,

Sasa Wiki mbili zimeisha baada ya aliyekuwa mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Dar kutenguliwa Cheo chake hicho baada ya yeye kuamua kugombea Ubunge wa Jimbo la Kigamboni ambapo kura zake hazikutosha.

Lakini tangu kipindi hicho hajakabidhi Funguo za Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa Mteule mpya.

Kabla ya Jumatatu anatakiwa awe amekabidhi ofisi kwa Mhe. Aboubakar Kunenge Mkuu mpya wa Mkoa wa Dar.

Kesho hakuna kazi. Je, leo atakabidhi Ofisi?

Thread
kwa jinsi mambo yanavyoendeshwa kindugu-ndugu chini ya awamu hii, si ajabu kukuta kumbe Makonda bado ni RC while huyu wa sasa ni proxy tu.

there're all signs Bashite is still in control.
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom