Silas Haki
JF-Expert Member
- Oct 18, 2010
- 368
- 39
Hapo kwenye RED. Kumbuka Jenerali Ulimwengu katika makala zake wakati wa uchaguzi alisema waandishi wengi unapofika wakati wa uchaguzi huwa wanachukua akili zao za kawaida wanaziweka kando, na kuvaa akili za kiuendawazimu hadi uchaguzi unapoisha. Kisha uchaguzi ukiisha wanazivua akili za kiuendawazimu na kuzirejesha akili zao za kawaida. Hao jamaa ndivyo walivyokuwa wakati wa uchaguzi kama unabii wa Jenerali Ulimwengu unavyoelezaPaul Mabuga,
I always respect your presentations on star tv's live programs, kuwa na utayari wa kurekebishika punde unapoteleza...kumbuka upo kwenye kioo cha jamii. Hali hii iliwatokea pia akina Yahya Mohamed & Baruan Muhuza kipindi cha 2010 national elections, lakini kwa sasa WAMEBADILIKA na kurejea kwenye ubora.
Hivyo Mabuga ipokee changamoto na ifanyie kazi, hopefully utafaulu na audience kukurejeshea heshima. UUNGWANA NI VITENDO, usichukie changamoto mkuu.
SHIME.
Nachoamini ni kuwa changamoto ni jambo la kawaida kwa binadamu! Kwangu mimi hakuna hoja ya kipuuzi. Lakini pia binadamu kutofautiana katika fikra ni jambo la kawaida, fikra zinajengwa na misingi minigi, baadhi ni pamoja na Imani, utashi na uelewa. Siwezi kuhukumu kipi kinawasukuma baadhi kutoa hoja na maoni waliyonayo, lakini ni mara chache misingi hii ikafanya katika hali ya usawa na kwa pamoja,lazima msingi mmoja utakuwa juu zaidi ya mingine. Kama binadamu pia kuna hatua za kujifunza katika jambo, kwanza naona, Napata uzoefu, maarifa mapya kama yapo na kisha napambanua, na hii ni lazima.
Kuibuka na fikra na kushtumu ama kulalamikia jambo ambalo una uewlewa nalo ama huna pia siyo dhambi, lakini uendeshaji na utayarishaji wa vipindi vya majadiliano una misingi na maadili yake. Unaweza kufanya kama wengine wanavyotaka uwafurahishe, nap engine fikiria ukifanya kuegemea upande mwingie kuwauzi hali itakuwaje. Lakini fikiria ukaendesha mjadala ambao wageni wako wengi wa upande mmoja, lakini unatakiwa kuwa na muungwana akilalamika kwa sababu umeuliza jambo ambalo yeye linamkirihisha.
Najua kwa nini zinakuwepo hoja kama zinazotolewa, lakini naziheshimu na nachukua kama changamoto.
Pengine ni nadra kwa mtu kujibu wazi malalamiko kama hivi, lakini nawapeni hongera mnaotoa malalamiko, wengine nawafahamu na wengine siwajui lakini Shukurani na Kwaresma njema.
Hivi kwa nini malalamiko haya yanatokea pale tu huyu jamaa anapoendesha kipindi ambacho kinaihusu CHADEMA sijasikia akilalamikiwa katika mada nyingine! Aanauwauzi nini Wana Nzengo na hasa wale ambao wanatarajia kugombe ubunge kwa tiketi ya CDM 2015?
Nimekiona kipindi, lakini , je usalama wa mtangazaji unakuwa wapi ikiwa mgeni anakaribia kuzunguza jambo ambalo linaweza kuwa kashfa ama tusi kwa namna fulani, lakini mbona nimeona wageni walikuwa wanapewa kauhoja za kuchokozwa ili waongee ... lakini bado licha ya kipindi kuegemea upande mmoja lakini bado tumepata hoja za upande mwingine... maanake vingine kingekuwa kipindi cha kwa ajili ya Cdm kama baadhi ya watu wanavyotaka.
Ufafanuzi ulikuwa mrefu, nafikiri kama hatujui kazi za watu tusijisemee kama vile tunabishana kwenye matapu tapu