DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari imewaagiza Waajiri wa Vyombo vya Habari kuhakikisha kuwa Waandishi wa Habari wanaogombea nafasi za kisiasa wanasitisha utekelezaji wa majukumu yao ya kihabari kwa kipindi chote cha mchakato wa uchaguzi.
Taarifa iliyotolewa leo June 21,2025 na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi hiyo, Patrick Kipangula imesema “Kwa kwa kuzingatia uwepo wa Uchaguzi Mkuu mwaka huu, na kwa mujibu wa masharti ya Kanuni ya 12(g) ya Kanuni za Utangazaji wa Uchaguzi kwa Vyama vya Siasa (Tangazo la Serikali Na. 775 la tarehe 18 Septemba, 2020).
Aidha, Waandishi wa Habari ambao ni Wagombea wa nafasi za kisiasa wanapaswa kuzingatia kwamba hawajihusishi katika shughuli au majukumu yoyote ya kihabari katika Vyombo vya Habari walivyoajiriwa kwa muda wote wa mchakato wa uchaguzi” “Hatua hii inalenga kuzuia mgongano wa maslahi na kulinda uaminifu wa Vyombo vya Habari mbele ya umma, hususan katika kipindi cha uchaguzi”
Chanzo: Millard Ayo
Taarifa iliyotolewa leo June 21,2025 na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi hiyo, Patrick Kipangula imesema “Kwa kwa kuzingatia uwepo wa Uchaguzi Mkuu mwaka huu, na kwa mujibu wa masharti ya Kanuni ya 12(g) ya Kanuni za Utangazaji wa Uchaguzi kwa Vyama vya Siasa (Tangazo la Serikali Na. 775 la tarehe 18 Septemba, 2020).
Aidha, Waandishi wa Habari ambao ni Wagombea wa nafasi za kisiasa wanapaswa kuzingatia kwamba hawajihusishi katika shughuli au majukumu yoyote ya kihabari katika Vyombo vya Habari walivyoajiriwa kwa muda wote wa mchakato wa uchaguzi” “Hatua hii inalenga kuzuia mgongano wa maslahi na kulinda uaminifu wa Vyombo vya Habari mbele ya umma, hususan katika kipindi cha uchaguzi”
Chanzo: Millard Ayo