Pata siri jaribio la kumuua Lissu

Pata siri jaribio la kumuua Lissu

The genius62 tuamini hizo dhana za nani mhusikana shambulizi ni za afisa usalama mstaafu na siyo zako. Kwamba tuwaachie Polisi kuwanasa ndo jambo la msingi.

Pmoja na hizo dhana, mkanganyiko wa mitazamo ya Serikali na Upinzani kuhusu vita ya kiuchumi, ufisadi na madawa ya kulevya nalo ni la kutilia maanani.
Nimekupata bt kumbuka cjafuta jina lake pale
 
Umeeleza vyema mkuu. Inawezekana serikali haijahusika na hili tukio ila matendo yanatufanya tuamini. Swali la msingi je, kuna Serikali inayopenda kuchafuliwa image yake? Nafhani haipo. Sasa kwanini huwa hawafanyi bidii kuwatia mbaroni wahusika halisi?

Em tujikumbushe haya matukio baadhi :

1. Ben Saanane kutoweka, vidole vimeelekezwa serikalini. Hajapatikana.

2. Nape Nnauye kutishwa bastola mubashara kabisa mbele ya halaiki ya waandishi wa habari. Muhusika alionekana kabisa. Kuna kilichoendelea?

3. Ofisi za IMMA kulipuliwa. Upelelezi bado unaendelea na Utazidi kuendelea...

4. Roma na wenzake kutekwa. Upelelezi bado unaendelea na utazidi kuendelea.

Sasa ukifikiria hayo matukio unajikuta kichwa kinashika moto, na kumbuka tulikubaliana kwamba hakuna Serikali inayopenda kuchafuliwa. Na njia nzuri ya kupambana na wanakuchafua ni kuwatia mbaroni.
Naaamn ipo cku watu wasiojikana watajulikana kila jambo lina mwsho wake
 
Km huu ndio usalama wa Taifa basi bora tusiwe nao kabisa

Hizi akili za kuuzia genge sio usalama wa Taifa

mchana toch ,usiku magogo tufanyaje?
 
Umeeleza vyema mkuu. Inawezekana serikali haijahusika na hili tukio ila matendo yanatufanya tuamini. Swali la msingi je, kuna Serikali inayopenda kuchafuliwa image yake? Nafhani haipo. Sasa kwanini huwa hawafanyi bidii kuwatia mbaroni wahusika halisi?

Em tujikumbushe haya matukio baadhi :

1. Ben Saanane kutoweka, vidole vimeelekezwa serikalini. Hajapatikana.

2. Nape Nnauye kutishwa bastola mubashara kabisa mbele ya halaiki ya waandishi wa habari. Muhusika alionekana kabisa. Kuna kilichoendelea?

3. Ofisi za IMMA kulipuliwa. Upelelezi bado unaendelea na Utazidi kuendelea...

4. Roma na wenzake kutekwa. Upelelezi bado unaendelea na utazidi kuendelea.

Sasa ukifikiria hayo matukio unajikuta kichwa kinashika moto, na kumbuka tulikubaliana kwamba hakuna Serikali inayopenda kuchafuliwa. Na njia nzuri ya kupambana na wanakuchafua ni kuwatia mbaroni.
Kuna matukio yaliyoumiza serikali vichwa zaidi ya mauaji ya askari na viongozi wa CCM kule kibiti? Je, unakumbuka ilichukua mudagani kumaliza hilo tatizo? Au unataka kutuaminisha kuwa na mauaji ya Kibiti yalikuwa orchastrated na serikali pia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Evarist Chahali, Afisa usalama wa taifa mstaafu

Wahusika Kina Nani ?: Jana, Septemba 07, 2017, majira ya mchana, zilipatikana taarifa kwamba Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Mbunge wa Singida Mashariki, Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani, na Rais wa Chama cha Wanasheria (TLS), amepigwa risasi kadhaa na kujeruhiwa vibaya.

Tukio hilo la kutisha lilitokea jijini Dodoma, wakati Mbunge huyo aliposhuka nyumbani kwake eneo la Area D, inakoelezwa alienda kwa ajili ya kujipatia mlo wa mchana.

Kabla ya kuingia kiundani kwenye makala hii, nitumie fursa hii kutoa salamu za pole kwa Lissu, na kumwombea apone haraka. Salamu za pole pia kwa viongozi, wanachama na wafuasi wa Chadema, chama ambacho Lissu amekuwa akikiwakilisha kwa ufanisi mkubwa.

Pia ni vema nitahadharishe mapema kwamba intelijensia sio sayansi timilifu kwa asilimia 100, kwa kimombo wanasema “intelligence is not an exact science.”

Okey, sasa tuingie mtamboni. Hadi muda huu kuna dhana za msingi tatu ambazo zinatokana na‘mchujo’ wa dhana mbalimbali.
Dhana ya kwanza na ambayo pengine ni maarufu zaidi ya zote ni kwamba jaribio hilo la mauaji ya Lissu lina mkono wa dola. Kwamba sio siri kuwa Lissu amekuwa ‘akiisumbua mno’ serikali, ambapo wafuasi wake wanamwona kama jasiri asiye na uoga wa kusema ukweli, ilhali wapinzani wake wakimwona kama mchochezi.

Yayumkinika kuhitimisha kwamba kama kuna mwanasiasa wa upinzani ambaye amekuwa ‘mwiba mchungu’ kwa serikali ya Rais John Magufuli basi si mwingine bali Lissu.
Na pengine kinachoongeza uzito kwenye dhana hii ni ukweli kwamba Agosti 18 mwaka huu, Lissu aliwaeleza wananchi kwamba anafuatiliwa.

Namnukuu "Naomba kabla sijaanza Mazungumzo yangu nimuombe Mkuu wa idara ya Usalama wa Taifa anaitwa Kipilimba au Inspekta Generali wa Polisi Simon Sirro, wale vijana ambao wamewatuma na kwa wiki tatu mfululizo wananifuata kila nilipo wanaotembea na gari ya Toyota premio namba T460CQV, jana niliwakaba Kanisani St. Peter's.”

Kwa upande mwingine serikali ya Magufuli ni kama ilikuwa inatafuta ‘kulaumiwa bure.’ Kwa sababu, Hadi muda huu hakuna sababu moja ya msingi kwa serikali hiyo kuyafanya maisha ya wanasiasa wa upinzani yawe magumu kiasi hiki. Magumu kwa maana ya kuwanyima kila aina ya fursa ya kufanya siasa (political space).

Kwa mujibu wa takwimu zilizopo, zaidi ya viongozi na wafuasi 400 wa Chadema wameshakamatwa tangu Magufuli aingie madarakani. Mtu atayedai kuwa kiongozi huyo ‘anawachukia wapinzani’ hatoonekana mtu wa ajabu japo huenda akatupwa jela.

Katika hotuba zake mbalimbali, Rais Magufuli ameshindwa kuficha hisia zake dhidi ya upinzani na wapinzani. Juni 12 mwaka huu, Rais Magufuli alimweleza Spika Job Ndugai maneno yafuatayo

“Tumia mbinu hiyohiyo ya kuwafanya wasiropokee Bungeni, waropokee nje na kule tutadili nao vizuri kwasababu wanapokua kule ndani wana kinga wanaweza wakatukana chochote, sasa kinga wanayoitumia vibaya bungeni kainyooshe wewe. Wawe wanatoka kule bungeni, ukishamfukuza hata mwezi mzima… atakuja aropokee huku, na mimi nakueleza waache waropokee huku nitadili nao, wala siwatishi lakini hatuwezi kuwa kwenye vita wewe unaanza kugeuka kupiga wale wanaokwenda mbele…. ni nafuu unyamaze ukalale.”

Kwa kuangalia jinsi watendaji wa serikali ngazi za mkoa na wilaya wanavyochuana na polisi kuwanyanyasa wapinzani, hususan wa Chadema, dhana kuwa serikali ina mkono katika jaribio la mauaji ya Lissu ni kama ‘ready-made.’

Hata hivyo, pamoja na ‘dalili zote’ kuashiria uwezekano wa mkono wa serikali katika jaribio la kumuua Lissu, dhana hii inakosa mantiki kiuhalisia. Ni kwamba hakuna tija kwa serikali kumuua Lissu. Sawa, sio siri kuwa uhusiano kati ya serikali na Lissu/ wapinzani sio mzuri, lakini haitokuwa na tija yoyote kwa serikali ya Magufuli kumuua Lissu.

Na hata kama ingekuwa lazima ‘aondoke,’ basi kuna ‘njia mwafaka zaidi’ za mauaji ya watu maarufu (assassination), huku 'kifo cha ajali' ikiwa maarufu na rahisi zaidi.

Halafu kinachotatiza katika tukio la jana, na kinachopunguza zaidi nguvu ya dhana kwamba ‘kuna mkono wa serikali,’ ni jinsi waliofanya shambulio hilo walivyoonekana kama wanahitaji publicity ya kutosha. Kwanini? Jibu lipo kwenye uchambuzi wa dhana ya tatu.

Dhana ya pili ni dhaifu kuliko nyingine mbili. Hii inahusisha mbio za urais mwaka 2020. Kwamba kila siku Lissu amekuwa akijitengenezea mazingira ya mgombea mwafaka wa Chadema/Upinzani katika uchaguzi mkuu ujao, wala halina mjadala. Sio kwamba Lissu amekuwa hodari katika masuala mbalimbali kwa vile anataka urais (hajawahi kutamka nia ya kugombea nafasi hiyo) lakini umahiri wake bungeni na katika masuala ya kisheria na kitaifa kwa ujumla, unamfanya kuwa kipenzi cha takriban kila mfuasi wa Chadema.

Dhana hii dhaifu inasema kuwa jaribio hilo la mauaji ni kazi ya wapinzani wa kisiasa wa Lissu, hususan ndani ya chama chake.
Udhaifu wa dhana hii ni kwamba, kama ambavyo kwenye dhana ya kwanza, hakuna tija katika kumdhuru Lissu hadharani. Kwamba hata kama kungekuwa na lundo la wapinzani wa kisiasa wa Lissu huko kwenye chama chake, kwanini wafanye ‘operesheni’ hiyo waziwazi badala ya kuandaa mkakati wa siri?
Na kama ilivyokuwa kwenye dhana ya kwanza, hata kama wapinzani wa kisiasa wa Lissu ndani ya chama chake wangekuwa wahusika, kwanini basi tukio hilo lifanyike katika mazingira ya ‘kusaka publicity kwa nguvu’?

Hiyo inatuacha na dhana moja, ya tatu, na ya mwisho. Ya mwisho lakini sio haba katika mantiki. Dhana hii inaeleza kwamba jaribio hilo la mauaji limefanywa makusudi na kile wajuzi wa mambo wanaita ‘rogue elements.’ Hizi zilitusumbua sana katika utawala wa Awamu ya Nne wa Rais Jakaya Kikwete. Rogue elements hizi zinajumuisha watumishi halali wa vyombo vya dola wanaofanya shughuli zisizo halali. Nani anawatuma? Hiyo ni habari nyingine.
Kuna kitu kinachofahuamika kama ‘Deep state.’ Kila nchi ina tafsiri yake kuhusu ‘deep state’ lakini tafsiri nyepesi kwa mazingira yetu ni ushirika wa watu wenye nguvu katika serikali na jamii – mfano vigogo (hususan wa zamani) wa vyombo vya dola, wafanyabiashara wenye uwezo mkubwa na wanasiasa kutoka upande wowote ule, lakini zaidi chama kilichopo madarakani.

Dhana hii inaliona tukio la kujaribu kumuua Lissu kama njia rahisi ya kuichafua serikali ya Rais Magufuli, ambayo kwa bahati mbaya/makusudi ilishajitengenezea mazingira ya kulaumiwa pindi la kutokea likimtokea mwanasiasa wa upinzani kama Lissu. Rais anaposhindwa kudhibiti ‘chuki zake’ dhidi ya wapinzani, anawapa nafasi nzuri ‘wabaya wake’ kutenda kitu kisha ikawa rahisi tu lawama kuelekezwa kwake.

Ndio maana dhana ya kwanza – kwamba kuna mkono wa serikali ya Magufuli kwenye jaribio la kumuua Lissu – inaonekana kama yenye uzito kwa vile "kuna sababu ready-made.”

Dhana hii inapata uzito kutokana na ukweli kwamba Magufuli amejitengenezea maadui wengi, wenye nguvu, na baadhi yao wakiwa viumbe hatari. Kuna watu waliozowea kuishi maisha ya kifalme ambao sasa wanalazimishwa kuishi maisha ya kawaida. Hawa watu wakipata upenyo wa kumdhuru Magufuli, hawatosita kufanya hivyo.

Lakini kwa vile ni ‘vigumu mno’ (angalau kwa wakati huu) kufanikisha jaribio la kumdhuru kiongozi huyo, njia nyepesi inaweza kuwa katika ‘kuua character yake,’ ambayo bahati nzuri kwa ‘wabaya wake,’ sio nzuri sana.

Kumekuwa na malalamiko kadhaa hasa kutoka upande wa upinzani kumtuhumu Magufuli kuwa ni dikteta. Na ukifuatilia mwenendo wa siasa zetu kwa muda huu, sio siri kwamba kuna chembe chembe za udikteta. Kwahiyo, ni rahisi kwa ‘wabaya wa Magufuli’ kutumia mwanya huo kujenga picha ya “serikali ya dikteta yamuua mpinzani wake mkubwa.”

Na hilo linatuleta kwenye suala la publicity. Kwamba jaribio la mauaji hayo liwe na mwangwi wa kutosha ndani na nje ya Tanzania. Mwangwi huo ni wa makusudi ili uakisi taswira inayojengeka kuwa ‘Magufuli ni dikteta. Na madikteta hunyanyasa wapinzani wao, na ikibidi hata kuwaua.’

Kwahiyo, kama kuna funzo kubwa kwa Magufuli katika tukio hili ni kuepuka mazingira yaliyopo ya uhasama mkubwa dhidi ya upinzani hususan Chadema. Kiongozi huyo anatambua fika kwamba kuna watu wapo radhi kufanya lolote lile kumng’oa, na kwa vile ‘njia za kawaida’ sio rahisi, basi inakuwa ‘anything goes,’ liwalo na liwe.

Na dhana hii ya tatu inaleta uhusiano kati ya tukio la jana la jaribio la kumuua Lissu na lile la hivi karibuni la kuchomwa moto kwa ofisi za kampuni ya uwakili wa IMMA. Kama hili la Lissu, tukio la moto nalo lilifanyika katika mazingira ya kuvutia publicity, yaani kama kulikuwa na jitihada za makusudi za kuushawishi umma kwamba “mnaona huyu dikteta Magufuli anakoelekea? Sasa anachoma hadi ofisi wa ‘wabaya’ wake.”

Nihitimishe uchambuzi huu kwa kueleza bayana masuala mawili matatu. Kwanza, lengo la uchambuzi huu mfupi sio kuingilia kazi za vyombo vya dola vinavyoendelea na uchunguzi kuhusu jaribio la kumuua Lissu. Nimefanya uchambuzi huu kama mtu mwenye uelewa wa masuala ya intelijensia na siasa za Tanzania yetu, ikiwa ni pamoja na “yanayojiri nyuma ya pazia.”

Pili, lengo la uchambuzi huu sio kumshawishi mtu yeyote abadili mtazamo wake kuhusu “nani ana/wanahusika.”
Mwisho, kama nilivyotanabaisha awali, tasnia ya intelijensia sio sayansi kamilifu kwa asilimia 100 (intelligence is not an exact science). Kwa maana hiyo, japo uchambuzi huu ni karibu kabisa na hali halisi, sio rahisi sana kufikia hali halisi yenye uhakika wa asilimia 100.

Nimalizie kwa kumtakia afya njema Bwana Lissu huku nikiamini kuwa malaka husika zitafanya kila jitihada kuwanasa wahusika, sio tu kwa minajili ya serikali kujinasua bali ili Bwana Lissu atendewe haki.
"Evarist Chahali, Afisa usalama wa taifa mstaafu". Nimeipenda hii na sikuona sababu ya kuendelea kusoma ngonjera

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chacha Wangwe ni serikali?
Madame Mbatia car accident ni serikali?
Zzk kuwekewa sumu bagamoyo ni serikali
Rev Mtikila car accident ni govt
Dr Mwakyembe na Prof Mark ni serikali?
Kwahiyo unathibitisha kuwa hayo matukio ambayo jamaa ameyaorodhesha yana mkono wa serikali?


Bless I
 
Naona mkuu umetuingiza darasani kidogo..btw muda ni mwalimu mzuri.miluzi mingi ilimpoteza mbwa.
 
First theory applies.

....it might be....
The third one might be! Along with it, the second theory is juxtaposited. It sounds that opposition have taken it to their advantage. Refer to Mr Mbowe interview with VoA about the incident. In that interview he said that over 21 bullets hit Lissu instead of 5 bullets that had been mentioned in statements issued earlier. To me that seemed intentional exageration. Finally, he concluded that he wanted the international community to be aware that Magufuli is using sledgehammer tactics against opposition. Such statements indicate that opposition are schadenfreude over the incident.
 
Siku zote ukitaka usafi hutapenda uchafu

Ukitaka unadhifu hutashiriki uchafu na kulazimisha wengine wachafuke

Mtu smart ni yule anatembea kwenye mstari wa:-

1. Katiba ya nchi

2. Sheria za nchi

3. Kanuni na taratibu

4. Mila na desturi za nchi

1. Katiba ya nchi
a) Siasa
-Vyama vya siasa vinapewa haki yao kufanya siasa kama ilivyoainishwa na katiba?

-Wanasiasa hususani wabunge hasa wa upinzani wanapewa haki ya kikatiba kufanya siasa katika maeneo ya Taifa la Tanzania?

-Bunge na wabunge, kuna uhuru wa wabunge kuishauri serikali, kuikosoa na kuisimamia kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni.....

Fukuzafukuza ya wabunge inafuata misingi ya bunge sheria na kanuni?

-Wakuu wa mikowa na wilaya nani zaidi ukilinganisha na wabunge ambao wanawakilisha maelf ya wapigakura? Je kuna uhusiano mzuri wa kisiasa na kiutendaji? Kamatakamata bila makosa

2. Sheria za nchi..
Ulinzi na usalama nijukum la serikali kwa raia wake na mali zao.
- Mawazo aliuwawa mchana kweupe
-Dr Mnvungi...mtaalam wa sheria kauliwa
-Beni saa nane kapotea
-Mateso akina mkatoriki
Nk

-Haki ya kukusanyika kupashana habari nk kama ilivyo ainashwa na katiba ya nchi ipo?...

Sintaandika kila kitu, hatahivyo endapo hayo mambo manne yamewekwa kapuni na kuwafanya watanzania kukosa kujuwa kama kuna manufaa ya kuwepo katiba au laaa basi tatizo linaanzia hapo....tusipindishe hoja kwa vioja.

Je serikali yetu inayafuata hayo? Inawapa watu haki zakisheria kwa mujibu wa katiba?

Je wale woote wanaoikosoa serikali wanatendewaje?
A) mpaka sasa Lisu anakesi ngapi mahakamani...? anashitakiwa na nani kwanini?

B) Mbowe anakesi ngapi mahakamani...? anashitakiwa na nani kwanini?

C) Mzee Hashim Rungwe anakesi ngapi mahakamani...? anashitakiwa na nani kwanini?

D) Halima mdee anakesi ngapi mahakamani...? anashitakiwa na nani kwanini?

Niwapinzani wangapi wanakesi ngapi mahakamani kwa makosagani kwanini sio wachama tawala?

Je kufanya siasa nikosa kikatiba.....kunakifungu chochote kinachosema siasa mpaka 2020?

Dhana zipo nyingi lakini serikali za kiafrika zina namna zao kushughurika na wapinzani nje ya katiba

Kagame wa Rwanda
Musseveni wa Uganda
Nkrunzinza wa Burundi
Kabira wa DRC
Omar Allybashir wa N. Sudani
Tatizo kubwa kuwaona maadui wakubwa wafuatao
-wapinzani wa kisiasa
-vyama pinzani vya siasa
-Wafuasi wa vyama pinzani vya siasa

Dhana hii kubwa nayamsingi kwenye serikali zetu inapelekea kwa wapinzani
Mateso
Manyanyaso
Kushikwashikwa hovyohovyo bila makosa yoyote
Mauwaji nk

Dhana kuu yakuona wapinzani maadui ndiyo tatizo kubwa na chanzo cha migogoro, mauwaji na mateso kwa viongozi wa kisiasa upinzani, wanachama wa upinzani kisiasa nk
 
Kuna matukio yaliyoumiza serikali vichwa zaidi ya mauaji ya askari na viongozi wa CCM kule kibiti? Je, unakumbuka ilichukua mudagani kumaliza hilo tatizo? Au unataka kutuaminisha kuwa na mauaji ya Kibiti yalikuwa orchastrated na serikali pia?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi mkuu point yangu umeipata kweli? Relax nisome tena utanielewa. Hapo unadhani unaitetea serikali lakini sio, unazidi kutuamisha kwa serikali ndio muhusika mkuu. Kwanini?

Hapo umekubali kabisa yalipotokea mauaji ya viongozi wa CCM ilichukua muda mpaka wahusika kupatikana. Sawa, lakini ishu ya Ben Saanane ina muda gani mpaka sasa? Je unajaribu kuniaminisha ninachokiwaza saa hizi baada ya hii post yako?
 
Chacha Wangwe ni serikali?
Madame Mbatia car accident ni serikali?
Zzk kuwekewa sumu bagamoyo ni serikali
Rev Mtikila car accident ni govt
Dr Mwakyembe na Prof Mark ni serikali?
Jibu ni ndioooooo. Ni serikali vinginevyo uniambie kuwa kati ya hao wote ni kwanini serikali haikufanya uchunguzi!?

Kama serikali ilifanya uchunguzi je, ilibaini mhusika /wahusika ni kina nani na walichukuliwa hatua gani!?

Huwezi, kuniambia kuwa kwenye matukio yote hayo eti serikali ilishindwa kuwabaini wahusika. Labda mliogopa kujichunguza wenyewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom