Tangu kitambo kidogo,umekuwa ukimnadi Edward Ngoyai Lowassa na kutuaminisha kuwa ndiye chaguo sahihi la CCM na nchi kwa ujumla kwa nafasi ya Urais 2015. Na hivi karibuni,hasa leo,umechomoza kama mpiga zumari wa Zitto Zuberi Kabwe kama chaguo sahihi la CHADEMA katika Urais 2015.
Hali ya kisiasa nchini Tanzania iliyopo na itakayofika 2015 inaonesha dhahiri kuwa mgombea wa ima CHADEMA au CCM ndiye atakayeibuka kidedea kama Rais wa tano wa Tanzania.
Ikiwa Lowassa atasimamishwa na CCM na Zitto atasimamishwa na CHADEMA,unadhani Tanzania itapata Rais inayomhitaji kuelekea mafanikio inayoyataka? Nini kinachokuaminisha kuwa hawa ni bora? Karibu Pasco,karibuni wana-JF wote tujadili
mara alitokea dereva wa zitto na kujumuika nao na ilipotimu saa sita za ucku aliondoka nao (PM7) kwa kauli hii unafikiri Zitto atafurukuta ndani ya chadema hadi kukabidhiwa kijiti cha kuwania nafac ya Urais
EL ndie the best that CCM has!. ZZK ndie the best that Chadema has na Jussa ndie the best tha CUF has for ZNZ.
Kuwa the best is one thing, kusimamishwa na chama is another thing!. Ili usimamishwe na chama, "you have to be the "choosen one", as of now, neither EL nor ZZK is the "choosen one".
2010, kwenye CCM, JK alisimama na Dr. Salim na Prof. Mwandosya. The best was Dr. Salim, akifuatiwa na Prof. Mwandosya, JK was the least na ndie aliyechaguliwa kusimama kwenye CCM simply because he was "the choosen one".
Na kati ya aliyosimama nao kuombea urais, JK was not the best ila ndie yeye aliyechaguliwa!.
Sio kweli kuwa siku zote "fast runners always win the race", or the brightest students win the exams!, Vivyo hivyo kwa EL na ZZK, they are the best but ...
Mkuu Pasco hivi kutakuwa na athari gani iwapo kwa EL na ZZK wasipoteuliwa na vyama vyao?
Kuhusu muundo wa serikali ijayo (2015) unapendekeza iweje? (hint.Make Katiba to remain constant or slighly change to happen).
Ni kigezo gani umetumia kwa Zito ili usemeanafa kama sio unataka kuingiza cdm mkenge.ZITTO mwenyewe yuko kimya kwenye kuimarisha chama wenzeke wanazunguka nchi nzima na M4C yeye anzunguka nje ya nchi kwa mambo.
Mkuu Ndalwa, kutoeleweka points zangu ni jambo moja na kutokuwa na msimamo ni jingine!.
Nkianzia na hili la kutoeleweka, tangu 4th Dec mpaka sasa 4th January, una kipindi cha mwezi mmoja tuu humu jukwaani, hivyo ni haki na halali yako kutonielewa, with time utakuja kunielewa tuu!.
Hili la msimamo nalo neno!, kila siku humu ninasema sina chama, sina upande, sina ushabiki, sina ufuasi, ila kuna watu nawaunga mkono!. Sasa kama na wewe ulitaraji au lazima niwe Chadema na kama mimi sio Chadema, then lazima ni CCM, endelea kuamini hivyo!. Mimi pasco wa jf naendelea kusimama kwenye kweli no matter what, CCM wakifanya mazuri, nawapongeza, wakichemsha nawabalasa, vivyo hivyo Chadema ikifanya mazuri ni pamoja sana ila mkichemsha ni bakora tuu kwa kwenda mbele, hata CUF or NCCR are not spared!.
Msimamo gani ambao wewe ungetaka niwe nao?!,
Pasco.
Hivi kuna tofauti gani kati Pasco na mimi kuwa na uhalali wakutoa maoni/msimamo nani anafaa kuwa Rais wa Tanzania? Je mimi pia mtanisikiliza nikitoa msimamo wangu kwamba anayefaa kuwa rais wa Tanzania 2015 ni Adrew Chenge? Kwa hiyo maoni ya Pasco kuhusu nani anweza kuwa rais wa Tanzania yanaweza kuwa sawasawa na ya mwendawazimu mwingine yeyote ambaye kulingana na uelewa au hata maslahi yake atamtaja Membe, Zitto au hata Lowassa kuwa anaweza kuwa rais wa Tanzania 2015.
KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ililazimika kujigeuza mahakama ili kusikiliza malalamiko dhidi ya wagombea nafasi ya uenyekiti wa baraza la vijana la chama hicho (BAVICHA).
Katika kusikiliza malalamiko hayo, Kamati Kuu iliwateua wanasheria wake mashuhuri, Mabere Marando na Profesa Abdallah Safari kuwa majaji wa kuendesha kesi ya Habibu Mchange aliyekuwa anawania nafasi ya mwenyekiti.
Mchange ambaye anajitambulisha kuwa ni mfuasi wa naibu katibu mkuu wa CHADEMA, Zitto Kabwe lilalamikiwa na mwenyekiti wa BAVICHA mkoani Mwanza, Liberatus Mlebele kukiuka maadili ya uchaguzi, ikiwamo kusafirisha wajumbe wa mkutano wa uchaguzi kutoka mikoani hadi Dar es Salaam.
Ndani ya CC, Mchange alilazimika kujibu tuhuma moja baada ya nyingine ikiwamo malalamiko ya kushindwa kuwajibika yaliyofunguliwa na katibu wa BAVICHA jimbo la Kigamboni.
Katibu huyo alimtuhumu Mchange kushindwa kutimiza wajibu wake kwa kile alichoeleza, Tangu achaguliwe kushika nafasi ya mwenyekiti wa BAVICHA wilayani humo hajahudhuria vikao.
Mjumbe mmoja wa CC amedokeza gazeti hili kuwa Mchange ambaye alionekana kuwa na wafuasi wengi, alikatwa kwa kuwa alishindwa kujitetea mbele ya mahakama ya CHADEMA.
Kwa mfano, kati ya 20 Mei na 25 mwaka huu, Mchange alituma zaidi ya Sh. 2, 561,000 kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa vijana kutoka katika mikoa mbalimbali nchini. Fedha hizo zilitumwa na Mchange mwenyewe kupitia mtandao wa M-Pesa na Tigo Pesa.
Namba ya Mchange iliyotumika kusambaza fedha hizo, ni 0658 178678. Alianza kutapakanya fedha kwa wajumbe 11 Mei 2011 saa 10:44.58 ambapo kiasi cha Sh. 28,500 zilitumwa kwa mmoja wa wajumbe wenye simu Na. 0659 374206.
Baadaye saa 11:04.24 alituma Sh. 15,500 kwenda Na. 0659 374206 na kisha 20 Mei 2011 saa 14:03.04 alituma Sh. 19,000 kwa mwenye Na. 0713 866650.
Tarehe 23 Mei 2011 saa 10:56.06, nyaraka zinaonyesa Mchange alituma Sh. 50,000 kwenda kwa mwenye Na. 0713 867745; tarehe 21Mei 2011 saa 11:54.47 alituma Sh. 40,000 kwenda kwa mwenye Na. 0717 268576 na saa 12:41.48 alituma Sh. 81,000 kwa mwenue Na. 0714 038536.
Wengine waliotumiwa fedha na Mchange; ni wenye Na. 0712 511508 aliyetumiwa Sh. 26,000 na mwenye Na. 0713 606169 aliyetumiwa Sh. 10,000 ambaye alitumiwa fedha hizo, saa 22:24.31.
Nyaraka za M-PESA zinamuonyesha Mchange akimtumia Peter Shiyo, mwenyekiti wa BAVICHA wilayani Maswa Sh. 50,000. Fedha hizo zilitumwa 23 Mei 2011 saa 16:39.
Tarehe hiyo 23 Mei 2011 saa 18:48, Mchange alituma kiasi cha Sh. 30,000 mwenyekiti wa vijana wilaya ya Singida Mjini, Wilfred Kitundu.
Aidha, siku hihiyo Mchange akitenda kama karani wa benki alituma Sh. 150,000 kwa mwenyekiti wa baraza hilo mkoani Mwanza, Liberatus Mlebele.
Mara baada ya kupokea fedha hizo, Mlebele aliwasilisha malalamiko kwa katibu mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa akimtuhumu Mchange kumshawishi kwa njia ya rushwa ili amchague kuwa mwenyekiti.
Katika barua yake hiyo, Mlebele pamoja na mambo mengine alisema, Ninakuandikia kwa nia njema kabisa ya kulinda hadhi ya chama chetu nikiomba maelekezo yako kama mtendaji mkuu wa chama.
Anasema, Tarehe 28 Mei 2011 Baraza la Vijana wa chama chetu litafanya uchaguzi wa viongozi wake wa kitaifa. Je, sisi wajumbe tumegharamiwa na chama ama wagombea kufika Dar es Salaam kwa ajili ya uchaguzi huu?
Alisema, Ninauliza hivi kwa sababu tayari mmoja wa wagombea ameshaniagiza kufika Dar es Salaam kwa gharama zake ili kukagua hoteli ambayo wajumbe wa mkoa wangu na kwingineko watafikia hali ambayo ninaihesabu kama rushwa.
Mlebele alisema katika barua yake, Niko tayari kutoa vielelezo sahihi juu ya kitendo hiki kama itabidi, ili kulinda hadhi ya chama chetu dhidi ya watu hatari kama hawa.
Alisema, Kwa kuwa mimi binafsi sipendi rushwa na siwezi kuvumilia vitendo vya rushwa na kwa kuwa natambua chama chetu kimekuwa kinara wa kupambana na rushwa nchini, ninaomba kamati kuu ichukue hatua stahiki dhidi ya mtu huyu ili kulinda hadhi ya baraza na chama chetu mbele ya wananchi.
Ni maelezo hayo ya Mlebele yaliyozika ndoto za Mchange kuwa mwenyekiti wa BAVICHA. Taarifa zinasema Dk. Slaa aliwasilisha malalamiko yote mbele ya wajumbe wa CC. Barua ya Mabele iliwasilishwa kwa Dk. Slaa, 26 Mei 2011.
Taarifa zinasema kabla ya CC kujigeuza mahakama ya kusikiliza shauri hilo, mjumbe mmoja alinukuliwa akimtetea Mchange. Hata hivyo, alizimwa na Dk. Slaa aliyesimama kidete kutaka chama chake kichunguze suala hilo na kichukue hatua.
Katika barua yake, Mlebele anasema alifikia katika hoteli ya Bondeni One iliyoko Magomeni. Anamtaja Mchange kuwa ndiye aliyelipa fedha hizo. Alitoa nakala ya kitabu cha wageni kuthibitisha kuwa fedha hizo zililipwa na aliyemteja.
Mchange alikiri mbele ya wajumbe wa CC kuwa ni kweli kwamba simu iliyotajwa kupeleka fedha ni yake; alimhonga Mlebele kiasi kilichotajwa, alilipia sehemu ya gharama za hoteli na alikiri kumuagiza akusanye wajumbe wa mkutano wa uchaguzi.
Kamati kuu ya CHADEMA ilipitisha majina ya wagombea tisa katika nafasi ya mwenyekiti na kisha kukasimu madaraka yake kwa kamati ya wazee kwa hatua nyingine inazoona zinafaa.
Ni kupitia kamati hiyo, ndiko wagombea wengine watatu walifyekwa. Waliopatwa na panga la kamati hiyo iliyokuwa chini ya Edwin Mtei, Bob Makani na mwanasheria wa chama hicho, Mabere Marando, ni Mtela Mwampamba, Bernard Saanane na Grayson Nyakarugu, huku John Heche akionywa na na kuelezwa ikibainika alifanya vitendo kinyume cha maandili, atavuliwa madaraka.
Wote waliokatwa walipatikana na makosa ya rushwa, kutoaminika, kupanga matokeo, makundi na kutumiwa na watu wa kutoka nje ya baraza la vijana.
Akifanya marejeo ya kilichofanyika Jumamosi katika uchaguzi huo uliofanyika ukumbi wa PTA Sabasaba, Temeke, jijini Dar es Salaam, Dk. Slaa alisema chama chake kimeweza kunasua mitego yote ya rushwa iliyopandikizwa na CCM
Ungekuwa unafuatilia misimamo ya Pasco wala usingepata shida. Pasco amekuwa very consistent about watu anaowaunga mkono. Hizi thread sasa inabidi tuzianzishie peer review process.
Very unfortunately mpaka sasa hapa nilipo, sina chama, yaani sio mwanachama wa chama chochote cha siasa!. Kwa vile uchaguzi ujao wa 2015, mgombea huru ni rukhsa, hilo linafikirika na nikiamua naweza kugombea popote!.
Pasco.
EL ndie the best that CCM has!. ZZK ndie the best that Chadema has na Jussa ndie the best tha CUF has for ZNZ.
Kuwa the best is one thing, kusimamishwa na chama is another thing!. Ili usimamishwe na chama, "you have to be the "choosen one", as of now, neither EL nor ZZK is the "choosen one".
2010, kwenye CCM, JK alisimama na Dr. Salim na Prof. Mwandosya. The best was Dr. Salim, akifuatiwa na Prof. Mwandosya, JK was the least na ndie aliyechaguliwa kusimama kwenye CCM simply because he was "the choosen one".
Na kati ya aliyosimama nao kuombea urais, JK was not the best ila ndie yeye aliyechaguliwa!.
Sio kweli kuwa siku zote "fast runners always win the race", or the brightest students win the exams!, Vivyo hivyo kwa EL na ZZK, they are the best but ...
Vyombo vya habari, wachambuzi na waandishi wengi katika masuala ya kijamii, kisiasa na kiuchumi nchini tumekuwa na kasumba ya:
Kuhabarisha
Kushawishi
Kushabikia
Badala ya kuchambua mbivu na mbichi na kuwaacha walaji wajue kipi ni bora kwa afya zao. Jukumu letu si kutoa hitimisho.
Hitimisho la nani anafaa na nani hafai ni kazi ya wananchi ambao wana dhamana ya kutumbukiza kura zao ndani ya ballot box. Hili la kwamba fulani na fulani ni chanda cha dhahabu, fulani na fulani hawana ubora kwa nafasi fulani bila kuleta mizani iliyotumika ni kutufikisha huko huko kwenye misingi ya wachambuzi kuhabarisha, kushabikia na kushawishi.
Pamoja na kwamba uhabarishaji ni jambo la msingi katika jamii, lakini vyombo vya habari pamoja na wachambuzi katika masuala ya uongozi nchini tunatakiwa kupanda ngazi moja juu zaidi katika kuchambua ngano na maguu shambani ili uvunaji unapowadia wavunaji wanakuwa na upeo wa kuelewa yapi magugu kuyatenga mbali na ngano itakayowekwa ghalani kwa ajili ya afya za watumiaji.
Narudia nilichokisema katika mada mbalimbali huko nyuma kwamba, uhariri katika vyombo mbalimbali vya habari nchini ni wa mantiki isiyo na kiwango kwa sababu ya uhariri wa kishabiki na kushawishi kuegemea upande fulani bila kuiangalia sarafu pande zote mbili. Hali kadhalika waandishi pamoja na ujuzi wa uchambuzi walio nao uandishi wao umeegemea zaidi kuhabarisha, kushabikia na kushawishi kitu ambacho ni kinyume cha taaluma ya ujuzi na uwajibika kwa jamii kwani ni uandishi ni chombo muhimu cha kuelimisha wananchi si kuwachagulia viongozi.
Hakuna mgombea uongozi anayekuwa perfect, kwani kila binadamu ana udhaifu wake. Pamoja na ukweli huo kuna mengi yanayotakiwa kuangaliwa katika maisha ya mtu katika kupima uwezo wake katika kuongoza nchi. Familia yake:
Muhimu kuangalia mtu uwezo anaokuwa nao katika kuongoza, kusetirika na ushirikiano anaokuwa nao katika familia yake kuanzia mume/mke na watoto wake, hali kadhalika mafanikio katika familia ni kipimo mojawapo, vinginevyo huwezi kujua uwezo wake kikamilifu.
Historia ya maisha yake:
Katika jamii wagombea wengi hujitahidi kuwa karibu na jamii wanazotaka kutumikia, isiwe kipindi cha papo kwa papo, kinachoangaliwa zaidi maisha yake tangu utotoni katika familia yake, shuleni, kazini, nk
Utumishi kwa umma:
Mambo kadhaa hutakiwa kuangaliwa utumishi wa mtu katika jamii kuangalia mafanikio yake katika shughuli alizofanikisha, uwezo wake wa kubuni mambo ya maendeleo kwa jamii, uwezo wa kusimamia miradi au kazi alizofanya au anazofanya, mahusiano yake na staff awapo katika shughuli hizo na jinsi anavyoweza kuwaunganisha wananchi na viongozi wenzake katika utumishi na uwajibikaji bila ubinafsi.
Alama za uongozi bora na udhaifu wake:
Katika nafasi hizo hapo juu, kwa kuangalia kwa undani mambo kadhaa yatajitokeza ikiwa ni pamoja na mafanikio yake. Hali kadhalika udhaifu wake utajitokeza kwa nafasi fulani fulani pamoja na kuonyesha mafanikio. Hayo yataweza kuleta picha ya uwezo wake kama kiongozi atakayefaa au la.
Kupima uwezo wake katika kushauri na kushaurika, busara katika maamuzi, uwezo wa kujali viongozi wenzake na wananchi, uwezo wa kupambanua udhaifu katika uongozi na kujitahidi kujenga taswira ya uwajibikaji kazini, pia muhimu zaidi kisaikolojia kujitambua udhaifu wake huweza kumjengea uwazi katika kushaurika.
Kama binadamu kwa vyo vyote kuna udhaifu kwani hakuna malaika, madhaifu yaanikwe ili kuwa na kipimo cha kuchagua unafuu katika wadhaifu kadhaa, ukifunikwa hatari yake majuto ni mjukuu, kwani akishakalia kiti cha Ikulu yuko juu na sheria inamlinda, pagumu kumnyoshea na kumkashifu.
Haya ndiyo tunayotakiwa kuyafanya badala ya mfumo wa propaganda uliozoeleka ambao hufanya tuwahimize wapiga kura wampigie kura fulani badala ya kuwafafanulia sifa na madhaifu ya viongozi hao wapiga kura watumia busara kutokana na ubora wa hawa wagombea. Wananchi wengi ambao ndio wenye ku-cast ballots kwenye ballot box hawawajui vizuri wagombea kwani kila mgombea anaeleza mazuri tu. Vyombo vya habari hupenya kila mahala na kisheria wana haki ya kupata kumbukumbu mbalimbali za wagombea kwa minajili ya kuelimisha jamii kwa kupima uwezo na udhaifu wao.
EL ndie the best that CCM has!. ZZK ndie the best that Chadema has na Jussa ndie the best tha CUF has for ZNZ.
Kuwa the best is one thing, kusimamishwa na chama is another thing!. Ili usimamishwe na chama, "you have to be the "choosen one", as of now, neither EL nor ZZK is the "choosen one".
2010, kwenye CCM, JK alisimama na Dr. Salim na Prof. Mwandosya. The best was Dr. Salim, akifuatiwa na Prof. Mwandosya, JK was the least na ndie aliyechaguliwa kusimama kwenye CCM simply because he was "the choosen one".
Na kati ya aliyosimama nao kuombea urais, JK was not the best ila ndie yeye aliyechaguliwa!.
Sio kweli kuwa siku zote "fast runners always win the race", or the brightest students win the exams!, Vivyo hivyo kwa EL na ZZK, they are the best but ...
Mkuu the leaned brother Petro E. Mselewa, naamini baada ya alichofanya Zitto jana mbele ya rais Mama Samia, kumuombea Mbowe aachiwe, utakuwa unakubaliana na mimi Zitto ni number nyingine, extra ordinary.
p
Tangu kitambo kidogo,umekuwa ukimnadi Na hivi karibuni,hasa leo,umechomoza kama mpiga zumari wa Zitto Zuberi Kabwe kama chaguo sahihi la CHADEMA katika Urais 2015.
Hali ya kisiasa nchini Tanzania iliyopo na itakayofika 2015 inaonesha dhahiri kuwa mgombea wa ima CHADEMA au CCM ndiye atakayeibuka kidedea kama Rais wa tano wa Tanzania.
Ikiwa Lowassa atasimamishwa na CCM na Zitto atasimamishwa na CHADEMA,unadhani Tanzania itapata Rais inayomhitaji kuelekea mafanikio inayoyataka? Nini kinachokuaminisha kuwa hawa ni bora? Karibu Pasco,karibuni wana-JF wote tujadili
Nime note Zitto anatajwa tajwa sana humu jukwaani, nikaona na mimi nijikumbushe niliwahi kuandika nini kumhusu mtu huyu.
All and all, huyu Zitto sio mtu wa mchezo mchezo, he is a man to watch very closely!, sio mtu wa kawaida!.
P
Nime note Zitto anatajwa tajwa sana humu jukwaani, nikaona na mimi nijikumbushe niliwahi kuandika nini kumhusu mtu huyu.
All and all, huyu Zitto sio mtu wa mchezo mchezo, he is a man to watch very closely!, sio mtu wa kawaida!.
P
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.