Pascal Mayalla adai Waziri Mpango alitumia muda mwingi katika kusifu alipowasilisha bajeti. Asema yeye siyo MATAGA na hatafuti uteuzi!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,968
141,976
Ni katika mjadala wa waandishi kwenye kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari.

Pascal anasema bajeti ya nchi inatakiwa kuwasilishwa kitaaluma lakini juzi waziri wa fedha Dr Mpango ametumia muda mwingi katika kusifu ukilinganisha na kuifafanua bajeti.

Mwandishi Moses Methew alimpinga Pascal kwa madai kuwa Dr Mpango alizitumia vizuri dakika 60 za mwanzo hivyo hakuna ubaya wowote kutumia dakika 135 zilizobaki kusifiana.
Moses amesema hata Pascal Mayalla mwenyewe katika dakika 10 alizopewa kwenye mjadala huu ametumia dakika 7 katika kusifu na mgeni wake kamwachia dakika 3 tu.

Katika kujibu Pascal amedai yeye husifu kimantiki siyo kama wafanyavyo wale Mataga na wala hatafuti Uteuzi kama rafiki zake wa Jf wanavyomzushia.

Mwisho mwandishi Moses Methew amevilaumu vyombo vya habari na bunge kwa kutumia muda mwingi kujadili mambo binafsi na faragha za Mbowe.

Amesema inasikitisha kuona bunge zima linajadili " maisha binafsi " ya Mbowe kana kwamba Mbowe ndio bajeti ya serikali.

Chanzo: Star tv

Maendeleo hayana vyama!
 
Nimegundua bunge la Tz ni la hovyo Afrika mashariki na kati.Bajeti imesomwa badala ya kuchambua na kuishauri serikali nimeona 85% ya wabunge wanasifia mpk kinyaacunaona hyu ni empty set,wanatoa vijembe,wanashindana kijinga kasoro 25% ndio wanaongea kisomi

Tizameni bunge la kenya linavyojadili bajeti unafurahi mwenyewe
 
Kuna mbunge kujadili maisha binafsi ya Mbowe kama Mbowe. Na kuna maisha binafsi ya Mbowe kama KUB ambae ni kiongozi wa umma. Sasa kama kiongozi wa umma ndio anaruhusiwa kulewa chakari na kula bata na vimada, sijui kama inakubalika.
 
Waziri wa Fedha tena akiwasilisha bajeti ya nchi hapaswi kutoa sifa za kuhudhuria misiba, kuwaona wafungwa, kushiriki michezo, kwenda makanisani nk na kuonesha mh Rais ni kiumbe cha kipekee. Akikuwa amebakiza kidogo sana kuinama chini na kumsujudia Rais.

Tujifunze kupongeza vitu na kusonga mbele. Ni ajabu mpk sasa tunazungumzia bwawa la umeme, ndege, SGR, elimu bure, uhakiki wa wafanyakazi. Ilitosha kupongeza mambo hayo wakati yalipoanza. Tujifunze tunapoanza au kukamilisha jambo fulani, lingine hutokea au mahitaji huenda ngazi nyingine ya juu. Ni vema kusifia lakini si vema kutumia nguvu zote kusifia na kushindwa hata kuona mambo mengine.

Rais amefanya mambo mazuri, tumsifie kidogo na tumuoneshe mahitaji mengine hata kama itabidi kumkosoa kwa namna alivofanya aliyoyafanya tayari.

Ukimsifia sana mtu, unakosa uhalali wa kumwambia amekosea. Unaanza kumwogopa!! Huenda hizi sifa ni uoga!!
 
Ni katika mjadala wa waandishi kwenye kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari.

Pascal anasema bajeti ya nchi inatakiwa kuwasilishwa kitaaluma lakini juzi waziri wa fedha Dr Mpango ametumia muda mwingi katika kusifu ukilinganisha na kuifafanua bajeti.

Mwandishi Moses Methew alimpinga Pascal kwa madai kuwa Dr Mpango alizitumia vizuri dakika 60 za mwanzo hivyo hakuna ubaya wowote kutumia dakika 135 zilizobaki kusifiana.
Moses amesema hata Pascal Mayalla mwenyewe katika dakika 10 alizopewa kwenye mjadala huu ametumia dakika 7 katika kusifu na mgeni wake kamwachia dakika 3 tu.

Katika kujibu Pascal amedai yeye husifu kimantiki siyo kama wafanyavyo wale Mataga na wala hatafuti Uteuzi kama rafiki zake wa Jf wanavyomzushia.

Mwisho mwandishi Moses Methew amevilaumu vyombo vya habari na bunge kwa kutumia muda mwingi kujadili mambo binafsi na faragha za Mbowe.

Amesema inasikitisha kuona bunge zima linajadili " maisha binafsi " ya Mbowe kana kwamba Mbowe ndio bajeti ya serikali.

Source Star tv

Maendeleo hayana vyama!
Namuona Pascal Mayala anarudi katika maisha ya kawaida, Huyo Jmaa aliwahi kuishi katika maisha ya stress za kimapenzi kwa mda sana, kupenda ni kubaya.
 
Back
Top Bottom