Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Wiki hii kote ulimwenguni Wakristo watasherehekea Pasaka. Pasaka ni sikukuu kubwa kwa Wakristo kwa sababu ni siku ya kuadhimisha tukio muhimu sana katika imani ya Kikristo — kufufuka kwa Yesu Kristo kutoka kwa wafu. Bila Pasaka, hakuna Ukristo. Ndiyo sababu Wakristo huiona Pasaka kuwa ni siku kuu ya kipekee kuliko Krismasi.
Nchini Marekani, wiki hii inatambulika kuwa ni Wiki Takatifu(Holy Week). Mwaka jana Rais Mstaafu, Joe Biden aliiadhimisha wiki ya Pasaka kwa kutoa tangazo la kuwatambua watu waliobadili jinsia!! Rais Trump amepindua uchafu huo na kuipa heshima wiki hii kwa kuandaa matukio makubwa ya kuadhimisha Pasaka.
Wiki hii, Jumatano jioni, wafanyakazi wa Ikulu ya Marekani watakuwa na "Dinner" nzito ya Pasaka. Alhamisi itakuwa siku ya maombi na kumwabudu Mungu kwa wafanyakazi wote wa Ikulu ya Marekani. Siku hiyo wafanyakazi hao watapata pia nafasi ya kusikiliza Neno la Mungu kutoka kwa Wahubiri mbalimbali.
Jumapili iliyopita, Rais Trump aliahidi kuilinda imani ya Kikristo mashuleni, katika Jeshi na katika maeneo yote ya kazi. Alisisitiza pia kwamba ataendelea kulinda uhuru wa kuabudu katika nchi hiyo.
Rais Trump haoni aibu kumtangaza Yesu na yuko tayari kuujulisha ulimwengu wote kuhusu imani yake.
Baada ya kuanza muhula wake wa pili, Rais Trump alianzisha "White House Faith Office" kupitia agizo la kiutendaji tarehe 7 Februari 2025, akiwa na lengo la kuyasaidia mashirika ya kidini na ya kijamii katika juhudi za kuimarisha familia za Marekani na kulinda uhuru wa kidini. Ofisi hii ndiyo inayoandaa sherehe kubwa za Pasaka, Ikulu ya Marekani, mwaka huu.
Wewe je, umeandaa nini kusherehekea Pasaka? Karibu nyumbani kwetu ule vinono!
Grace and peace to you this Easter season. God bless you abundantly.
Nchini Marekani, wiki hii inatambulika kuwa ni Wiki Takatifu(Holy Week). Mwaka jana Rais Mstaafu, Joe Biden aliiadhimisha wiki ya Pasaka kwa kutoa tangazo la kuwatambua watu waliobadili jinsia!! Rais Trump amepindua uchafu huo na kuipa heshima wiki hii kwa kuandaa matukio makubwa ya kuadhimisha Pasaka.
Wiki hii, Jumatano jioni, wafanyakazi wa Ikulu ya Marekani watakuwa na "Dinner" nzito ya Pasaka. Alhamisi itakuwa siku ya maombi na kumwabudu Mungu kwa wafanyakazi wote wa Ikulu ya Marekani. Siku hiyo wafanyakazi hao watapata pia nafasi ya kusikiliza Neno la Mungu kutoka kwa Wahubiri mbalimbali.
Jumapili iliyopita, Rais Trump aliahidi kuilinda imani ya Kikristo mashuleni, katika Jeshi na katika maeneo yote ya kazi. Alisisitiza pia kwamba ataendelea kulinda uhuru wa kuabudu katika nchi hiyo.
Rais Trump haoni aibu kumtangaza Yesu na yuko tayari kuujulisha ulimwengu wote kuhusu imani yake.
Baada ya kuanza muhula wake wa pili, Rais Trump alianzisha "White House Faith Office" kupitia agizo la kiutendaji tarehe 7 Februari 2025, akiwa na lengo la kuyasaidia mashirika ya kidini na ya kijamii katika juhudi za kuimarisha familia za Marekani na kulinda uhuru wa kidini. Ofisi hii ndiyo inayoandaa sherehe kubwa za Pasaka, Ikulu ya Marekani, mwaka huu.
Wewe je, umeandaa nini kusherehekea Pasaka? Karibu nyumbani kwetu ule vinono!
Grace and peace to you this Easter season. God bless you abundantly.