My Son drink water
JF-Expert Member
- Nov 30, 2016
- 4,930
- 13,333
Mada hii imejikita ktk kushauri kizalendo nini kifanyike ili kuliokoa taifa lisizidi kutopea kwenye umasikini wa kutupwa unaolikabili taifa kwa sasa.
Idara ya usalama ina wataalamu wa nyanja zote wenye uwezo mkubwa kiakili pia, baadhi yao ni ma genius.
Idara hii iache kutumika kisiasa, bali itumike kulinda maslahi ya watanzania wote wenye vyama tofauti na dini tofauti.
Wanasiasa wakianza kuitumia Idara ya usalama kwa maslahi yao ya kisiasa na siyo nchi hatima yake huwa ni mbaya sana.
Kwa hiyo ni bora idara ikacheza mazingaombwe kuhakikisha nchi inakuwa na katiba nzuri kwa ajili ya watu wote na vizazi vyote vijavyo na siyo kulilinda genge la watu wachache kwa faida yao.
Hayati Baba wa taifa, Mwl Nyerere aliwahi kuonya endapo chama tawala kitaingiliwa na matajiri basi huo ndo ilikuwa mwisho wake ,watu wenye pesa walikimbilia chama tawala ili kulinda maslahi yao, siyo kwa sababu wanaipenda CCM, la hasha, bali kwa sababu wakienda upinzani biashara zao zipo hatarini.
Idara imeacha taifa liwe la watu wanaoimba mchana na usiku kusifia chama tawala na viongozi wake badala ya kuimba uzalendo juu ya nchi yao.
Wakenya waliokuwa wakiimba kusifia KANU badala ya Kenya zaidi ya miaka 32,leo KANU iko wapi? Lakini Kenya yao ipo.
Hata CCM inayotawala leo itapotea na kutoweka, na hata CHADEMA ikitawala nayo itakuja kupotea na kutoweka, Lakini Tanzania inadumu milele yote.
Idara ina watu wenye weledi mkubwa wanaojua jinsi ya kuifanya Tanzania isiwe ya makundi ya watu vichaa wanaoshinda mitandaoni kutukana na kukejeli kila anayekosoa Serikali bali wawe watu wamoja wenye uzalendo uliotukuka juu ya taifa lao.
Bado naendelea kuamini kuwa TISS ina uwezo wa kufanya kazi Kama MOSSAD au CIA ikitaka.
Kipi kinashindikana? ni TISS hii hii iliweza kuzuia hujuma kibao za Serikali ya kibaguzi ya makaburu dhidi ya Tanzania.
Ni TISS hii hii, iliendesha operesheni za ukombozi wa nchi za kusini mwa Africa.
Basi na sasa isimame juu ya ustawi bora wa Tanzania, maana kuna chuki kubwa mno za kisiasa miongoni mwetu.
Kuna mtu mmoja akaniuliza, "ulitaka TISS wajenge viwanda ?".
Lilikuwa swali zuri mno japo la kimbumbumbu.
Nilikaa kimya na sasa najibu hapa.
Tulikuwa na viwanda takribani 400,na moja ya viwanda hivyo kilikuwepo cha kusindika nyama ya ng'ombe, cha viatu, nguo, matairi na n.k.
65% ya viwanda vilivyokufa Tanzania vilikuja kufufukia Kenya, tafsiri yake ni kwamba, Usalama wa Taifa wa Kenya, KNIA walifanya yao huku TISS yetu ikiwa imelala, na Kiwanda cha mwisho kuhamia Kenya ni cha General Tyres, yaani ajira zinakufa Tanzania kisha zinawafufukia Wakenya.
Kenya imecheza sana ujasusi wa kiuchumi dhidi ya Tanzania, nashukuru Mungu tena dakika za mwisho TISS walistukia mchezo vinginevyo VodaCom nayo ilikuwa inakufa na ingekuja kufufukia Kenya
Inaendelea
www.jamiiforums.com
Idara ya usalama ina wataalamu wa nyanja zote wenye uwezo mkubwa kiakili pia, baadhi yao ni ma genius.
Idara hii iache kutumika kisiasa, bali itumike kulinda maslahi ya watanzania wote wenye vyama tofauti na dini tofauti.
Wanasiasa wakianza kuitumia Idara ya usalama kwa maslahi yao ya kisiasa na siyo nchi hatima yake huwa ni mbaya sana.
Kwa hiyo ni bora idara ikacheza mazingaombwe kuhakikisha nchi inakuwa na katiba nzuri kwa ajili ya watu wote na vizazi vyote vijavyo na siyo kulilinda genge la watu wachache kwa faida yao.
Hayati Baba wa taifa, Mwl Nyerere aliwahi kuonya endapo chama tawala kitaingiliwa na matajiri basi huo ndo ilikuwa mwisho wake ,watu wenye pesa walikimbilia chama tawala ili kulinda maslahi yao, siyo kwa sababu wanaipenda CCM, la hasha, bali kwa sababu wakienda upinzani biashara zao zipo hatarini.
Idara imeacha taifa liwe la watu wanaoimba mchana na usiku kusifia chama tawala na viongozi wake badala ya kuimba uzalendo juu ya nchi yao.
Wakenya waliokuwa wakiimba kusifia KANU badala ya Kenya zaidi ya miaka 32,leo KANU iko wapi? Lakini Kenya yao ipo.
Hata CCM inayotawala leo itapotea na kutoweka, na hata CHADEMA ikitawala nayo itakuja kupotea na kutoweka, Lakini Tanzania inadumu milele yote.
Idara ina watu wenye weledi mkubwa wanaojua jinsi ya kuifanya Tanzania isiwe ya makundi ya watu vichaa wanaoshinda mitandaoni kutukana na kukejeli kila anayekosoa Serikali bali wawe watu wamoja wenye uzalendo uliotukuka juu ya taifa lao.
Bado naendelea kuamini kuwa TISS ina uwezo wa kufanya kazi Kama MOSSAD au CIA ikitaka.
Kipi kinashindikana? ni TISS hii hii iliweza kuzuia hujuma kibao za Serikali ya kibaguzi ya makaburu dhidi ya Tanzania.
Ni TISS hii hii, iliendesha operesheni za ukombozi wa nchi za kusini mwa Africa.
Basi na sasa isimame juu ya ustawi bora wa Tanzania, maana kuna chuki kubwa mno za kisiasa miongoni mwetu.
Kuna mtu mmoja akaniuliza, "ulitaka TISS wajenge viwanda ?".
Lilikuwa swali zuri mno japo la kimbumbumbu.
Nilikaa kimya na sasa najibu hapa.
Tulikuwa na viwanda takribani 400,na moja ya viwanda hivyo kilikuwepo cha kusindika nyama ya ng'ombe, cha viatu, nguo, matairi na n.k.
65% ya viwanda vilivyokufa Tanzania vilikuja kufufukia Kenya, tafsiri yake ni kwamba, Usalama wa Taifa wa Kenya, KNIA walifanya yao huku TISS yetu ikiwa imelala, na Kiwanda cha mwisho kuhamia Kenya ni cha General Tyres, yaani ajira zinakufa Tanzania kisha zinawafufukia Wakenya.
Kenya imecheza sana ujasusi wa kiuchumi dhidi ya Tanzania, nashukuru Mungu tena dakika za mwisho TISS walistukia mchezo vinginevyo VodaCom nayo ilikuwa inakufa na ingekuja kufufukia Kenya
Inaendelea
Part 1: TISS bado safari ngumu
Kuna watu wanadhani kuondoka kwa mzee wangu wa Kanisa,TISS ndugu Kipilimba basi mambo yanaenda kubadilika na kuifanya idara hiyo ifanye kazi nzuri la hasha. TISS bado ina safari ndefu mno ili iwe idara bora Kama zingine, recruitment ya TISS imejaa viroja na maajabu, tofauti na mashirika mengi...
