Vugu-Vugu
JF-Expert Member
- Feb 24, 2017
- 1,109
- 1,265
Hiki ndicho alichokisema Baba Mtakatifu Francesco ambaye ndiye Kiongozi Mkuu wa Kanisa Takatifu Katoliki la Mitume Duniani,
Nimejipa muda wa kutosha nimeupitia waraka huu Mtakatifu nukta kwa nukta neno kwa neno mstari kwa mstari sijaona sehemu Ushoga na Usagaji vimeruhusiwa na kiongozi huyu wa juu kabisa wa Kanisa.
Katika waraka huu zaidi sana nimeona nafuu waliyopewa hawa mashoga wamepata neema kwa vitu vyao kubarikiwa mfano wa vitu hivyo ni kama kiwanja, Nyumba, gari au vinginevyo ila si ndoa Takatifu,
Tunakubaliana wote kuwa Gari la shoga haliwezi kuwa ni gari shoga au shule ya Shoga haiwezi kuwa ni shule shoga ila mmiliki,
Ushoga ni baina ya mtu na mtu mfano mwanaume na mwanaume au mwanamke na mwanamke na si kitu na kitu.
Kwakuwa tunaishi kwenye nyakati za mwisho watu wanatamani Kanisa liidhinishe dhambi zao mbele za Mungu.
Lazima tufahamu kuwa, Hata kama Kanisa au misikiti itaruhusu Ushoga dhambi hii bado iko palepale, na ni motoni moja kwa Moja bila mjadala.
Mungu lilinde na kuliinua Kanisa Katoliki Duniani, kote