Papa Mjesuit ana kasi sana

Jackwillpower

JF-Expert Member
Oct 4, 2017
2,301
3,414
Papa huyu mjesuit anawaumiza sana Wakatoliki waaminifu, hajui tu

Ingawa ndio injili ya wajesuit ya umoja katika tofauti. Mnamo karne ya 17, Wajesuit walifanya maridhiano na Wachina juu ya ibada zao za kuwaomba mababu zao waliokufa kama sehemu ya imani ya Katoliki.

Wajesuit wakakubali na ikawa hivyo, na mfalme wa China akawapenda sana kwa ustadi wao na kuupa utamaduni wa China heshima, kidogo tu abatizwe. Leo China ingekuwa ni taifa la Kikatoliki.

Lakini mvurugano ulitokea kati ya Wadominika na Wafranciskana dhidi ya injili ya Wajesuit ya maridhiano. Kesi ikafika hadi Vatican kwa Papa. Wajesuit wakajenga hoja lakini wakashindwa mbele ya Wadominika na Wafranciskana, ikaamulia injili yao ya maridhiano huko China ikomeshwe.

Mfalme wa China hakupendezwa na mvurugano huo. Papa akamuandikia barua mfalme Kang wa China dhidi ya injili hiyo na akimtaka ajisalimishe kwenye ukatoliki pasee aachane na wazo la Wajesuits. Mfalme alikerwa na barua hiyo na akaichana mbele ya baraza lake.

Maana aliona papa kavuka mpaka kuingilia uhuru wa China. Na toka siku hiyo akapiga marufuku mahubiri ya Wakristo na kuwafukuza Wadominika, Wafranciskana na akaamuru Wachina wasiwe Wakatoliki kwa amri ya kifo.

Wajesuit walipata kibali machoni pake sababu ya aina ya injili yao ya maridhiano, maana walivalia kama makasisi wa Confusian na mfalme aliwachukua kuwa washauri wake na wakaiboresha sayansi ya China. Lakini mnamo 1773 shirika la Jesuits lilivunjwa na papa Clement IV kwa shinikizo la wafalme wa Ulaya, hivyo mission yao ndani ya China ikakoma. Kwanini shirika lao lilivunjwa, hiyo ni mada nyingine....

Walirejeshwa rasmi mnamo 1814 na Papa Pius VII, na leo wanaye papa anayetokana na wao. Inasemekana walirudi Vatican kibabe na sasa ndio wanaoliendesha kanisa. Na mkuu (jenerali wao) amebatizwa jina la Papa mweusi (black pope) kuashiria yupo nyuma ya Papa mweupe (White Pope).

Hivyo tegemea injili ya maridhiano isiyotaka kuudhi watu bali kuridhisha matakwa ya umma. Ingawa kuna vuguvugu la upinzani ndani ya kanisa dhidi ya injili ya Papa huyu.

Hivyo wakatoliki waaminifu wajiandae kwa mambo ya kukera zaidi kutoka kwa Papa huyu.

FB_IMG_1704120241875.jpg
 
Hili nalo litapita naamini Mungu ana nafasi nzuri zaidi ya ku-deal nalo.

Walishakuwepo zaidi ya huyu still imani ikasimama nadhani ni era yetu kizazi hiki na sisi kupitia magumu.
 
Jesuit wana nguvu sana niliwahi pata hadithi kutoka kwa wajuvi ulichoongea kinafanana na nilichoambiwa safi sana...
 
Vibaya kuomba atuongezee ulinzi?
Kwa ulichoandika pale juu wewe siyo wa kuomba tena vitu vidogo kama ulinzi,hivi wewe umeshaijua siri ya Mungu kwamba fulani na fulani wao jehanam wewe mbinguni uombe ulinzi kweli?

Maombi yako ilibidi yawe ni akufunulie siku gani atakuchukua ili umuage kama ni mkeo au mumeo wanao na wote wa nyumba yako ili akupalize mbinguni ukale mema yake.
 
Papa huyu mjesuit anawaumiza sana Wakatoliki waaminifu, hajui tu

Ingawa ndio injili ya wajesuit ya umoja katika tofauti. Mnamo karne ya 17, Wajesuit walifanya maridhiano na Wachina juu ya ibada zao za kuwaomba mababu zao waliokufa kama sehemu ya imani ya Katoliki.

Wajesuit wakakubali na ikawa hivyo, na mfalme wa China akawapenda sana kwa ustadi wao na kuupa utamaduni wa China heshima, kidogo tu abatizwe. Leo China ingekuwa ni taifa la Kikatoliki.

Lakini mvurugano ulitokea kati ya Wadominika na Wafranciskana dhidi ya injili ya Wajesuit ya maridhiano. Kesi ikafika hadi Vatican kwa Papa. Wajesuit wakajenga hoja lakini wakashindwa mbele ya Wadominika na Wafranciskana, ikaamulia injili yao ya maridhiano huko China ikomeshwe.

Mfalme wa China hakupendezwa na mvurugano huo. Papa akamuandikia barua mfalme Kang wa China dhidi ya injili hiyo na akimtaka ajisalimishe kwenye ukatoliki pasee aachane na wazo la Wajesuits. Mfalme alikerwa na barua hiyo na akaichana mbele ya baraza lake.

Maana aliona papa kavuka mpaka kuingilia uhuru wa China. Na toka siku hiyo akapiga marufuku mahubiri ya Wakristo na kuwafukuza Wadominika, Wafranciskana na akaamuru Wachina wasiwe Wakatoliki kwa amri ya kifo.

Wajesuit walipata kibali machoni pake sababu ya aina ya injili yao ya maridhiano, maana walivalia kama makasisi wa Confusian na mfalme aliwachukua kuwa washauri wake na wakaiboresha sayansi ya China. Lakini mnamo 1773 shirika la Jesuits lilivunjwa na papa Clement IV kwa shinikizo la wafalme wa Ulaya, hivyo mission yao ndani ya China ikakoma. Kwanini shirika lao lilivunjwa, hiyo ni mada nyingine....

Walirejeshwa rasmi mnamo 1814 na Papa Pius VII, na leo wanaye papa anayetokana na wao. Inasemekana walirudi Vatican kibabe na sasa ndio wanaoliendesha kanisa. Na mkuu (jenerali wao) amebatizwa jina la Papa mweusi (black pope) kuashiria yupo nyuma ya Papa mweupe (White Pope).

Hivyo tegemea injili ya maridhiano isiyotaka kuudhi watu bali kuridhisha matakwa ya umma. Ingawa kuna vuguvugu la upinzani ndani ya kanisa dhidi ya injili ya Papa huyu.

Hivyo wakatoliki waaminifu wajiandae kwa mambo ya kukera zaidi kutoka kwa Papa huyu.

View attachment 2859403
Asante mleta mada , lakini inadhaniwa papa hawezi kutoa hitimisho lolote wala shinikizo lolote ndani ya kanisa bila ya mabaraza au watu waandamizi ndio waamue kwa umoja wao kisha yeye kama papa ndie anatoa kama tamko.
Kwa hiyo haiwezi kuwa kinachoendelea sasa ni kwa utashi wa Fransins kama mjesuit bali ni vatikani kwa ujumla wake, izingatiwe pia ni mzee mwenye zaidi ya miaka 80 hivyo haidhaniki kama mawazo na utashi wake ni wa kutegemewa.
 
Unazijua KAZI ya hizi six codes duniani kwenye ulimwengu wa giza.
111,333,555,666,999.
666 sio Nero Bali ni mfumo wa uchumi duniani.
Codes zingine hizo ni sayansi,siasa,dini,nk
Hujui lolote, kitabu cha ufunuo wa Yohana hakuna mjinga yeyote anayeweza kukielewa.

Ndio mnyama 666 ametajwa ni hesabu ya kibinadamu.

Viongozi wanaongoza Kwa mkono wa chuma huwa hawatajwi Kwa majina Yao, hata Magufuli hapa aliitwa Kayafa.
 
Kwa ulichoandika pale juu wewe siyo wa kuomba tena vitu vidogo kama ulinzi,hivi wewe umeshaijua siri ya Mungu kwamba fulani na fulani wao jehanam wewe mbinguni uombe ulinzi kweli?

Maombi yako ilibidi yawe ni akufunulie siku gani atakuchukua ili umuage kama ni mkeo au mumeo wanao na wote wa nyumba yako ili akupalize mbinguni ukale mema yake.
Una upeo mkubwa kuliko mleta maada, mleta maada kakalili mafundisho,akirudi kwenye utashi wake halisi anasahau amekalili Nini,anatoa maono aliyooneshwa na sehemu yake kwenye maono,akili zake zikimrudi anaomba apewe Tena sehemu ambayo kwenye maono tayari anayo,,, ,
 
Asante mleta mada , lakini inadhaniwa papa hawezi kutoa hitimisho lolote wala shinikizo lolote ndani ya kanisa bila ya mabaraza au watu waandamizi ndio waamue kwa umoja wao kisha yeye kama papa ndie anatoa kama tamko.
Kwa hiyo haiwezi kuwa kinachoendelea sasa ni kwa utashi wa Fransins kama mjesuit bali ni vatikani kwa ujumla wake, izingatiwe pia ni mzee mwenye zaidi ya miaka 80 hivyo haidhaniki kama mawazo na utashi wake ni wa kutegemewa.
Na mimi nafikiri hilo, papa hawezi kufikia hitimisho bila makadinali na maafisa waandamizi wa vatican kushirikishwa.....labda tuseme kwamba wale wanao influence maamuzi na mwelekeo wa kanisa ndo wengi wao globalists kama alivyosema Jesuits, huenda wame infiltarate mfumo na kuweza kuwa na nguvu kubwa ya kimaamuzi na kuwazidi kete wale fundamentalists ambao wamejikita kwenye mafundisho asili ya kanisa.

Lakini kimantiki utawezaje kuwazuia watu wa aina hiyo kubatizwa au kupata huduma nyingine za kikanisa, inaweza kutafsiriwa kama unawahukumu, ndiyo maana Papa aliwahi kunukuliwa akisema yeye ni nani hata ahukumu? Tatizo linaweza kuja kwa watu kutaka kutambuliwa kanisani kwa dhambi au maovu wao, kwamba wanataka kutambuliwa kanisani kama mashoga, wasagaji, wezi, majambazi, mafisadi nk.​
 
Back
Top Bottom