sosoliso
JF-Expert Member
- May 6, 2009
- 8,539
- 9,462
Licha ya waziri mkuu, Mh. Mizengo Pinda kudai Serikali inatoa fedha za maendeleo bila ya ubaguzi wa itikadi, hali ni tofauti kwa Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kutokana na Madiwani wa CCM kutaka kata zinazoongozwa na upinzani zisipewe miradi mipya ya maendeleo..
Mh. Pinda alilazimika kutoa majibu hayo baada ya kuulizwa na kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, Mh. Freeman Mbowe kutokana na kauli zilizowahi kutolewa na Mawaziri waandamizi kama vitisho kwa wananchi kuwa wakiwachagua wapinzani hawatapata maendeleo..
Kamati ya Madiwani baada ya uchaguzi iliweka misimamo wa kutopitisha fedha za ujenzi huo, huku wanafunzi wakilazimika kukaa zaidi ya miezi saba nyumbani mpaka ujenzi ulipokamilika kwa michango ya wazazi na wadau wa elimu. Pia katika kikao cha bajeti cha Madiwani kilichoketi katikati ya wiki iliopita, Madiwani ambao wengi wanatoka CCM walipendekeza miradi ya ujenzi wa barabara kata za Nyansurura na Machochwe, zinazoongozwa na upinzani ziondolewe na badala yake zipelekwe kata za Madiwani wa CCM..
Madiwani wa CCM waliazimia kwenda kumuona Waziri wa elimu na ufundi na Katibu mkuu wa CCM, kuwashtaki wataalam waliopitisha ukarabati wa shule iliyo chini ya upinzani..
Source: Mwananchi
My Take:
Bado tuna safari ndefu sana kufikia demokrasia..
Mh. Pinda alilazimika kutoa majibu hayo baada ya kuulizwa na kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, Mh. Freeman Mbowe kutokana na kauli zilizowahi kutolewa na Mawaziri waandamizi kama vitisho kwa wananchi kuwa wakiwachagua wapinzani hawatapata maendeleo..
Kamati ya Madiwani baada ya uchaguzi iliweka misimamo wa kutopitisha fedha za ujenzi huo, huku wanafunzi wakilazimika kukaa zaidi ya miezi saba nyumbani mpaka ujenzi ulipokamilika kwa michango ya wazazi na wadau wa elimu. Pia katika kikao cha bajeti cha Madiwani kilichoketi katikati ya wiki iliopita, Madiwani ambao wengi wanatoka CCM walipendekeza miradi ya ujenzi wa barabara kata za Nyansurura na Machochwe, zinazoongozwa na upinzani ziondolewe na badala yake zipelekwe kata za Madiwani wa CCM..
Madiwani wa CCM waliazimia kwenda kumuona Waziri wa elimu na ufundi na Katibu mkuu wa CCM, kuwashtaki wataalam waliopitisha ukarabati wa shule iliyo chini ya upinzani..
Source: Mwananchi
My Take:
Bado tuna safari ndefu sana kufikia demokrasia..