Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,954
- 20,475
Walosimama kutoka kushoto: Kipa namba moja Madata Lubigisa, Rajabu Msoma , Beya Simba, Nteze John, Kitwana Selemani, Fumo Felician, Paschal Mayala na kipa Paul Rwechungura.
Walokaa kutoka kushoto ni : George Gole, Khalfan Ngasa, Ali Bushiri, David Mwkalebela, Maonwa Mkami, Alphonce Modesti, Juma Amiri Maftah na Nico Bambaga.
Hii ni timu iliwika kati ya mwaka 1980 na 1990 ingawa ilikuja timu ingine kati ta mwaka 1990 na 1995.
Hapa ndo Pamba ilikuwa haijampata kiungo mahiri Huseein Marsha na beki mshahara George Masatu.
Hiki ndicho kikosi kilichotikisa soka la Tanzania wakti ule Pamba FC au Tout Poisssant Lindanda.
Akiwepo Chilambo Domonic ameshika kipaza sauti kwenye mechi kati ya Simba na Yanga CCM Kirumba Mwanza, basi hauna mahitaji ya Charles Hirary, Salum Mbonde, na Sekione Kitojo, wao wabakia Dar-es-Salaam.
Kulikuwa na timu zingine pinzani kwenye ligi kuu ya Tanzania bara zikiwemo Pilsner ya Arusha, mecco ya Mbeya na Sigara ya Dar-es-Salaam.