Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Patashika ya Michuano ya Kombe la Azam Sports Federation Cup kuendelea kupigwa leo Mei 14, 2022 ambapo Mnyama Mkali Mwituni Simba SC, anakipiga na TP Lindanda Wana Kawekamo Pamba FC, katika hatua ya robo fainali kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa.
Mchezo unatarajiwa kuwa mkali hasa baada ya Pamba FC kutaka kuwavuruga Simba SC katika mipango yao ya kutetea ubingwa huu wa Kombe la Azam Sports Federation Cup.
Kocha wa Simba SC Pablo Franco Martin amesema kuwa anahitaji ushindi hivyo atapanga kikosi kamili kulingana na umuhimu wa mchezo huu.
"Michuano hii hakuna timu rahisi, huu ni mchezo muhimu kwetu tunahitaji kushinda ili kusonga mbele tutapanga kikosi kamili kwa wachezaji wote walio tayari kwa mchezo" amesema Kocha Pablo
Naye Kocha wa Pamba FC Athuman Kairo amesema kuwa wamakuja kupambana kupata matokeo ya ushindi.
"Tumekuja kupambana na Simba SC, tuajua kuwa ni timu kubwa, ngumu, nzuri, lakini sisi kama Pamba FC tunawaheshimu na tutacheza kwa nidhamu ili mwisho wa siku tupate ushindi na kuweza kusonga mbele kwenye nusu fainali" amesema Kocha Kairo.
Yote kwa yote ni dakika 90 za jasho na damu kuamua..Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 1: 00 Usiku.. Usikose Ukaambiwa.
Kulipewa Mwana Kulitaka Mwana
..... Ghazwat.....
======================
Wakati wowote mpira utaanza Uwanja wa Mkapa | Simba SC Vs Pamba FC
00' Naaam mpiraaaaaaa umeanza
03' Peter Banda anashindwa kuweka mpira kambani baada ya kutokea Krosi ya Kibu, ilikuwa hatari lango la Pamba FC.
05' Nafasi nyingine tena kwa simba kushindwa kuandika bao, Mhilu anakosaaaaaa.
07' Bocco na Kibu wanashindwa kutumia nafasi nzuri ya kufunga, Simba hizi nafasi watajutia kama hawatapata ushindi.
10' Yusuf Mhilu tena anashindwa kuunganisha Krosi bomba ya Banda
Pamba FC hawajapata nafasi ya kumfikia golikipa wa Simba, Beno kutokana na mashambulizi yao kuishia kwa mabeki wa Simba SC
18' Jaribio la kwanza kwa Pamba FC kwa shuti kali, lakini golikipa Beno anarukaaaa na kuokoa hatari ile na kuwa Kona ambayo haikuzaa matunda
20' Simba SC 0-0 Pamba FC
Free Kick inapigwa kuelekea Simba SC lakini golikipa Beno, anadaka bila wasiwasi, Pamba FC wameamka sasa.
23' Nafasi nyingine kwa Simba, Bocco, anakosaaaaaa kichwa cha John Bocco kinashindwa kulenga lango, ilikuwa nafasi nzuri ya kufunga.
28' Simba SC wamepata Kona tatu mfululizo bila mafaniko ya kufunga.
33' Salum Sheshe wa Pamba FC anaonyeshwa KADI ya Njano kwa kumvuta Jezi Hussein
37' Robert Makidala anakosa nafasi nzuri ya kufunga, ilikuwa Shambulizi kali kuelekea Simba | wakati huo huo Mohamed Said ameoneshwa Kadi ya Njano kwa kumchezea madhambi Kibu
43' Pascal Wawa anaonyeshwa KADI ya Njano kwa mchezo mbaya, Pamba wanacheza eneo lao la nyuma kuwavuta Simba
45' Goooooooooooooaaal gooal
Peter Banda anaipatia Simba bao la kwanza | Simba SC 1-0 Pamba FC
45' Mwamuzi anakamilisha kipindi cha kwanza
Timu zinaingia kwa ajili ya kipindi cha pili
46' Simba wanafanya mabadiliko, anatoka John Bocco anaingia Meddie Kagere
48' GOOOOOOOOOOOOOOOOOOO
Kibu Denis anafunga bao la pili kwa Simba kwa kichwa, akimalizia mpira uliotoka kwa Mohamed Hussein 'Zimbwe Jr'
50' Simba wanaendelea kumiliki mchezo.
52' GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO
Yusuph Mhilu anaipatia Simba bao la tatu kwa kichwa, amemalizia mpira kutoka kwa Kagere
Ametoka Mzamiru na ameingia Lwanga upande wa Simba SC
74' Mchezaji Mbaruku anaonyeshwa KADI ya Njano kwa kumchezea madhambi Peter Banda
76' Wawa yupo chini akipatiwa matibabu baada ya kugongana na mchezaji wa Pamba FC
78' Yusuf Mhilu anapiga shutii lakini golikipa wa Pamba anacheza mpira na kuwa Kona ambayo haikuzaa bao
Pamba wanajibu Counter Attack mbele kuleee lakini golikipa Beno anadaka
88' Goooooooooooooaaal gooal
Yusuf Mhilu anaipatia Simba SC bao la nne | Simba SC 4-0 Pamba FC
90+3'
Kuelekea kumalizika kwa mchezo huu
Wanamiliki mpira Simba, wanacheza eneo la nyuma, kwake Wawa sasa
Free Kick inapigwa kuelekea Simba SC, inapigwa kulee lakini mpira unatoka nje ya kuwa goal kick
Mpira umekwisha ambapo Simba SC wameibuka na ushindi mnono wa mabao manne kwa bila dhidi ya Pamba FC, na kutinga hatua ya Nusu Fainali
FT: Simba SC 4-0 Pamba FC
Kwa matokeo haya, sasa Simba itakipiga dhidi ya Yanga katika nusu fainali.
Mchezo unatarajiwa kuwa mkali hasa baada ya Pamba FC kutaka kuwavuruga Simba SC katika mipango yao ya kutetea ubingwa huu wa Kombe la Azam Sports Federation Cup.
Kocha wa Simba SC Pablo Franco Martin amesema kuwa anahitaji ushindi hivyo atapanga kikosi kamili kulingana na umuhimu wa mchezo huu.
"Michuano hii hakuna timu rahisi, huu ni mchezo muhimu kwetu tunahitaji kushinda ili kusonga mbele tutapanga kikosi kamili kwa wachezaji wote walio tayari kwa mchezo" amesema Kocha Pablo
Naye Kocha wa Pamba FC Athuman Kairo amesema kuwa wamakuja kupambana kupata matokeo ya ushindi.
"Tumekuja kupambana na Simba SC, tuajua kuwa ni timu kubwa, ngumu, nzuri, lakini sisi kama Pamba FC tunawaheshimu na tutacheza kwa nidhamu ili mwisho wa siku tupate ushindi na kuweza kusonga mbele kwenye nusu fainali" amesema Kocha Kairo.
Yote kwa yote ni dakika 90 za jasho na damu kuamua..Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 1: 00 Usiku.. Usikose Ukaambiwa.
Kulipewa Mwana Kulitaka Mwana
..... Ghazwat.....
======================
Wakati wowote mpira utaanza Uwanja wa Mkapa | Simba SC Vs Pamba FC
00' Naaam mpiraaaaaaa umeanza
03' Peter Banda anashindwa kuweka mpira kambani baada ya kutokea Krosi ya Kibu, ilikuwa hatari lango la Pamba FC.
05' Nafasi nyingine tena kwa simba kushindwa kuandika bao, Mhilu anakosaaaaaa.
07' Bocco na Kibu wanashindwa kutumia nafasi nzuri ya kufunga, Simba hizi nafasi watajutia kama hawatapata ushindi.
10' Yusuf Mhilu tena anashindwa kuunganisha Krosi bomba ya Banda
Pamba FC hawajapata nafasi ya kumfikia golikipa wa Simba, Beno kutokana na mashambulizi yao kuishia kwa mabeki wa Simba SC
18' Jaribio la kwanza kwa Pamba FC kwa shuti kali, lakini golikipa Beno anarukaaaa na kuokoa hatari ile na kuwa Kona ambayo haikuzaa matunda
20' Simba SC 0-0 Pamba FC
Free Kick inapigwa kuelekea Simba SC lakini golikipa Beno, anadaka bila wasiwasi, Pamba FC wameamka sasa.
23' Nafasi nyingine kwa Simba, Bocco, anakosaaaaaa kichwa cha John Bocco kinashindwa kulenga lango, ilikuwa nafasi nzuri ya kufunga.
28' Simba SC wamepata Kona tatu mfululizo bila mafaniko ya kufunga.
33' Salum Sheshe wa Pamba FC anaonyeshwa KADI ya Njano kwa kumvuta Jezi Hussein
37' Robert Makidala anakosa nafasi nzuri ya kufunga, ilikuwa Shambulizi kali kuelekea Simba | wakati huo huo Mohamed Said ameoneshwa Kadi ya Njano kwa kumchezea madhambi Kibu
43' Pascal Wawa anaonyeshwa KADI ya Njano kwa mchezo mbaya, Pamba wanacheza eneo lao la nyuma kuwavuta Simba
45' Goooooooooooooaaal gooal
Peter Banda anaipatia Simba bao la kwanza | Simba SC 1-0 Pamba FC
45' Mwamuzi anakamilisha kipindi cha kwanza
Timu zinaingia kwa ajili ya kipindi cha pili
46' Simba wanafanya mabadiliko, anatoka John Bocco anaingia Meddie Kagere
48' GOOOOOOOOOOOOOOOOOOO
Kibu Denis anafunga bao la pili kwa Simba kwa kichwa, akimalizia mpira uliotoka kwa Mohamed Hussein 'Zimbwe Jr'
50' Simba wanaendelea kumiliki mchezo.
52' GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO
Yusuph Mhilu anaipatia Simba bao la tatu kwa kichwa, amemalizia mpira kutoka kwa Kagere
Ametoka Mzamiru na ameingia Lwanga upande wa Simba SC
74' Mchezaji Mbaruku anaonyeshwa KADI ya Njano kwa kumchezea madhambi Peter Banda
76' Wawa yupo chini akipatiwa matibabu baada ya kugongana na mchezaji wa Pamba FC
78' Yusuf Mhilu anapiga shutii lakini golikipa wa Pamba anacheza mpira na kuwa Kona ambayo haikuzaa bao
Pamba wanajibu Counter Attack mbele kuleee lakini golikipa Beno anadaka
88' Goooooooooooooaaal gooal
Yusuf Mhilu anaipatia Simba SC bao la nne | Simba SC 4-0 Pamba FC
90+3'
Kuelekea kumalizika kwa mchezo huu
Wanamiliki mpira Simba, wanacheza eneo la nyuma, kwake Wawa sasa
Free Kick inapigwa kuelekea Simba SC, inapigwa kulee lakini mpira unatoka nje ya kuwa goal kick
Mpira umekwisha ambapo Simba SC wameibuka na ushindi mnono wa mabao manne kwa bila dhidi ya Pamba FC, na kutinga hatua ya Nusu Fainali
FT: Simba SC 4-0 Pamba FC
Kwa matokeo haya, sasa Simba itakipiga dhidi ya Yanga katika nusu fainali.