Antony Fereji
Member
- Sep 29, 2016
- 46
- 63
Huwa nakereka sana pale mbunge, tena mtu mzima badala kuongelea musuala ya msingi, anaanza kuongea masuala binafsi, mipasho, na majungu.
Mfano, mtu anakurupuka, "Mh naibu spika tutoe ile sanamu Posta tuweke ya Diamond". Haya nimatope au akili?
Tabia nyingine chafu, utakuta mtu anasimama, " Mh naibu spika, mke wangu ni mvumilivu sana, alizaa mtoto wa kwanza akafa, akazaa wapili akafa, huyu watatu nitampa jina lako" (nge nge nge) wabunge wakigonga meza utafikiri hoja ya muhimu. Mtu kama huyu si angekwenda kwenye kituo cha redio akatoe historia yake? Sio bungeni.
Kuna tabia ya wabunge wa "ndiooooo", hawa huwa hawaonekani kabisa, lakini linapokuja suala linalohusu kupitisha masuala muhimu ya taifa utasikia " ndiooo". Huu ni umbea, ni ukasuku.
Saizi hata wasomi waliopo bungeni wameweka usomi wao pembeni wamejawa na umbea tu. Watu tumewaamini, badala yakujadili mambo ya msingi, yanaanza kufanya mipasho, shit!!
Mfano, mtu anakurupuka, "Mh naibu spika tutoe ile sanamu Posta tuweke ya Diamond". Haya nimatope au akili?
Tabia nyingine chafu, utakuta mtu anasimama, " Mh naibu spika, mke wangu ni mvumilivu sana, alizaa mtoto wa kwanza akafa, akazaa wapili akafa, huyu watatu nitampa jina lako" (nge nge nge) wabunge wakigonga meza utafikiri hoja ya muhimu. Mtu kama huyu si angekwenda kwenye kituo cha redio akatoe historia yake? Sio bungeni.
Kuna tabia ya wabunge wa "ndiooooo", hawa huwa hawaonekani kabisa, lakini linapokuja suala linalohusu kupitisha masuala muhimu ya taifa utasikia " ndiooo". Huu ni umbea, ni ukasuku.
Saizi hata wasomi waliopo bungeni wameweka usomi wao pembeni wamejawa na umbea tu. Watu tumewaamini, badala yakujadili mambo ya msingi, yanaanza kufanya mipasho, shit!!