Mwizukulu wa Buganda
JF-Expert Member
- Nov 19, 2024
- 657
- 1,792
Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa'ichi OFMCap, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, anasikitika kuwatangazia kwamba leo tarehe 30/01/2026 saa 10.31 alfajiri mpendwa wetu Padre Paul Nsekela Mboje SABUNI, Paroko wa Parokia ya IPTL, ameitwa nyumbani kwa Baba wa Milele akiwa katika matibabu katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam.
Mazishi yatafanyika siku ya Jumatano tarehe 04.02.2026 katika Makaburi ya Mapadri yaliyopo katika kituo cha hija Pugu. Misa ya Mazishi itaanza saa 3:00 asubuhi.
Habari ziwafikie Maaskofu, Mapadri, Mashemasi, Watawa, Wanafamilia, Waamini wote walei wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Ndugu, Jamaa na Marafiki wote wenye mapenzi mema.
Raha ya Milele umpe Ee Bwana na Mwanga wa Milele Umwangazie, Apumzike kwa Amani; Amina