Oya shika mchuma!

kilimasera

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2009
Posts
3,068
Reaction score
277
*Kondakta *: Kaa mkao wa pesa.
*Abiria *: Si tumetosha? Twende basi!
*Kondakta*: Tunafanya kazi kwa hesabu mama mdogo.
*Abiria*: Hebu twendeni. Kuna watu huko mbele.
*Kondakta*: Kama una haraka ungeenda toka juzi. Tuko kazini hapa.
*Mpiga debe*: Wenye haraka wanaonyesha. Wenye haraka huchukua teksi.
*Abiria*: Tukichukua teksi mtakula wapi. Hebu acheni dharau. Twendeni, gari
si imejaa?
*Mpiga debe*: Jamani, mchuma haujai. Inayojaa ni ndoo ya maji. Haya,
Kariakoo, Kariakoo... gari nyeupe hii.
 
Ni saa tano usiku. Siku ya jumamosi. Kituo cha mabasi Mwenge. Tunaelekea
Mbezi Beach.
*Abiria*: Dereva twende bwana...saa za majeruhi hizi.
*Kondakta*: Bado vichwa babu. Gari haiendi mswaki hii hata siku moja.
*Abiria* (amelewa chakari): Nina haraka ya kufumania. Nimeambiwa saa tano na
nusu ndio saa ya kumfumania mbaya wangu.
Mara abiria huyu aliyelewa anaanza kutapika.
*Abiria 1*: Jamani watu wameanza kutapika humu ndani.
*Abiria 2*: Nipisheni nitoke miye...
*Abiria 3*: Afadhali niende kwa miguu.
*Kondakta*: Kuna wagonjwa huku?
*Abiria 4:* Twendeni. Hamjui ni mambo ya wikiendi haya?
*Abiria 5*: Pombe za bure hizo.
*Kondakta*: Kama sio pombe za bure basi ni za mkopo. Shuka bwana mzee.
Walevi hawa kwanza huwa hawataki kulipa.
 
Wanakosaga jibu wale???????
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…