selina rose
Member
- Jun 18, 2016
- 32
- 60
Yeye atafute maisha yake, ajiendeleze kielimu, njia anayoichagua haitamsaidia, njia hiyo imewapeleka kubaya wengi, his father had a very sad ending, huwezi kuibuka mshindi katika vita hiyo hata ukiua watu million, baba yake ulimwengu mzima ulimuona shujaa, lakini kwa kadri miaka ilivyozidi kwenda alikosa pa kukimbilia, aliishi kama digi digi ndani ya compound moja tu Bila kutoka, aliishi kama mfungwa mwenye kuletewa kila mlo ndani kama jela, familia yake ilishindwa kutoka hata nje ya geti kwa hofu ya kukamatwa, watoto walishindwa hata kwenda hata shuleni
Mwisho Osama kaja kuuawa kama kuku, hakukutwa hata na bunduki ya kusingiziwa, hakujijitetea hata kidogo, badala yake mwanamke, mkewe mdogo amal ndie anasimama mbele ya Osama kumkinga mumewe, akiwarushia wa marekani viatu na mito na kila kitu, wanamwonea huruma binti mdogo waanamua kumpiga risasi ya mguu na kisha wanaendelea na kazi iliyowaleta hapo
Huo unakua mwisho wa Osama
Leo mwanae anataka kufuata njia hiyo hiyo iliyomshinda babake, hata kabla ya kuuawa Osama, alqaida ilikufa long time, walibaki viongozi wanaoishi kwa kujificha, hawajawahi kufanya shambulio lolote la maana katika nchi za magharibi kwa miaka sasa, hata kiongozi wake mkuu mpya dk Ayman Al zawahir anaishi kama digi digi kwa kujificha, lakini one day marekani itamfikia aliko
Adui mkubwa wa uislam duniani ni alqaida na Osama, ndie aliefanya uislam uonekane dini mbaya, thank God vijana wengi katika ulimwengu wa kiislam hasa uarabuni walikuja kugundua Osama na alqaida yake hawakua wanapigania uislam, maana baada ya kushindwa kulipua nchi za kimagharibi na kuanza kulipua nchi za kiislam hivyo kupoteza uungwaji mkono, na ikawa ndio anguko lao, sawa sawa na isis au daesh itakavyoanguka, maana imeanza kulipua nchi za kiislam mfano madina
Bahati nzuri, hakuna sheria inayomfunga huyu kijana, hajawahi kujihusisha na ugaidi, hivyo ajitenge na maisha hayo aishi maisha ya kiraia