Orodha Mafisadi wa Elimu Tanzania na Msemakweli

Orodha Mafisadi wa Elimu Tanzania na Msemakweli

Joined
May 28, 2013
Posts
91
Reaction score
17
Hiki ni kitabu kipya kilichoandikwa na Msemakweli Kainerugamba. Kati ya mambo mengine mwandishi anatoa orodha ya majina ya watu vyeti bandia. Baadhi ya “mafisadi wa elimu” ni viongozi wakubwa serikalini.

Mfano ni Makongoro Mahanga ambaye tayari ameshakwenda mahakamani kudai fidia kwa kudhalilishwa na Msemakweli. Taarifa kutoka kwenye mtandao, wengine ndani ya kitabu hicho ni Lukuvi, Mary Nagu, Kamalla,Diallo na Nchimbi.

Tanzania Commission of Universities (TCU) jana wametoa tamko juu ya orodha hiyo.Prof Nkunya akiongea na vyombo vya habari aliwataka wote walioandikwa wapeleke vyeti vyao TCU kwa uhakiki na udhibitisho kama ni halali au bandia.

Msemakweli kama Mwanasheri na mwandishi naona yeye ametimiza wajibu wake kuutarifu umma. Kazi ni kwa mahakama na walalamikaji kudhibitisha kwamba vyeti vyao ni halali. Swala la vteti feki, kwa kweli limechukua muda mrefu kushughulikiwa na serikali.

Bado yapo maswaliya msingi yatakiwa majibu. Iweje TCU mpaka kitabu kitoke ndio wao wawatake washutumiwa kupeleka vyeti vyao kwa ukaguzi? Je hii sio “reactive management” wakati kwa taasisi nyeti kama yao walipaswa kuwa na “proactive management”.

Binafsi bado sijapata nafasi ya kukisoma kitabu hicho. Kwa wenye taarifa juu ya upatikanaji wake tafadhali mtujulishe.
 
Mwanaharati Msemakweli aliwahi kutoa kitabu cha Mafisadi wa Elimu.Katika kitabu hicho ambacho katika jalada la mbele kimepambwa na picha za
viongozi kumi ambao alidai kuwa wamegushi vyeti.

Viongozi hao ambao ni makada wa CCM na waliowahi kushika nyadhifa mbalimbali ikiwepo ubunge na uwaziri,ni pamoja na aliyewahi kuwa Waziri wa Jumuia ya Afrika Mashariki, Dk. Diodorus Kamala, Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk. Mary Nagu, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Vijana na Ajira, Dk. Makongoro Mahanga.

Wengine ni Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Emmanuel Nchimbi, Waziri wa Ardhi Mbunge wa Ismani, William Lukuvi, Victor Mwambalaswa, Omar Kwaang?w, pamoja, Anthony Diallo.
 
Hivi Kaenerugaba Msemakweli alipotelea wapi? Nakumbuka alisema angekuja na ufisadi mwingine lakini ghafla akapotea
 
Jamani,jamani,jamani ajidhaniaye amesimama na aangalie asije akaanguka anguko kuu.Kitabu kilikuwa kimeandikwa kikomedi zaidi,ikawa ndiyo mwisho wake.
 
mahanga anatakiwa kulipa fidia kwa msemakweli sasa,sijui keshalipa?
 
Kama una cheti feki ondoka mwenyewe mapema usisubiri kuaibishwa.
Jamani,jamani,jamani ajidhaniaye amesimama na aangalie asije akaanguka anguko kuu.Kitabu kilikuwa kimeandikwa kikomedi zaidi,ikawa ndiyo mwisho wake.
 
Mbona hawakumshtaki

Walimshitaki na akawashinda baadhi yao na wengine kesi zinaendelea mahakamani. Makongoro inatakiwa amlipe shilingi kama 13,000,000/= ama afungwe ambapo anayetakiwa kulipa gharama za mfungwa huyo kuishi gerezani ni Kainerugaba mwenyewe. Hili suala lipo kwenye mchakato pindi ikiwa tayari anaelekea jela kumlipia mteja wake
 
Hii ni orodha iliyotoka kwenye vyanzo mbalimbali vya habari ambayo inaonesha baadhi ya viongozi ambao kwa kipindi flani walipata kashfa juu ya kufoji elimu zao.............. Rashid Kawawa...enzi za awamu ya kwanza,Fredrick Sumaye hadi kupewa jina la Mr zero,Freeman Mbowe bado kuna utata juu ya elimu yake ya kidato cha sita,John Mnyika ..wanasema alishindwa kumalizia degree yake,Ole sendekka...,hamis kigangwallah,mwigykllu ,makamba jr,llukkuvi,Mbilinyi,joseph,Haule.......napekuhusu elimu yake ya master mzumbe......mwenye orodha zaidi ataongezea. Kwa ufupi nawezza kusema Makonda suo wa kwanza kutuhumiwa kwa hiyo kama tunafuatilia elimu tuchimbue haswa la suvyo hizi kashfa za elimu zitarudia kutwa kucha......Kutuhumu kimmahaba sio sahihi tutuhumu na ushahidi usio na mashaka........kila la heria wazee wa kufoward udaku
 
alilipa 2 mil. mwezi uliopita, mwezi huu mahakama iliagiza akamatwe sijui kama kashatiwa mbaroni.
 
Ole Sendeka alikua head prefect pale Old Moshi alichukua Pumba, Cabbage na Biskuti. Alipata division zero. Alivyogundua kwamba siasa haihitaji akili .......jazia mwenyewe
 
Back
Top Bottom