Bravo magufuli.tz hatuwwezi kuwa na mfumo mzuri wa barabara kama sheria zitakiukwa kila siku.ni ajabu sana mtu anapotekeleza sheria analaumiwa. Wakati wa ujenzi wa barabara inayoanzia ubungo tanesco(ubungo maziwa) via kigogo,jangwwani to kariakoo inaanza kujengwa,eneo la kuanzi pale mabibo mwisho anzia pale relini karibu na marie stopes mpaka eneo la shungashunga(junction ya njia ya kwenda external mandela road) bomba la ges la Songas lilikuwa limefukiwa eneo la barabara na ilichukua muda sana kulihamisha,sasa jiulize wakati wanachimbia bomba hilo hawakujua ni eneo la barabara? Au kwa sababu waliona ni eneo la wazi tu wakaamua kuchimba mitaro na kufukia bomba ilimradi kazi imeisha. Ni lazima sheria za hifadhi za barabara na za mipango miji zizingatiwe.hatuwezi kuwa na barabara nzuri na miji mizuri kama kila mtu atakuwa anajiamulia kujijengea kibanda kila sehemu anayotaka ilimradi afanye biashara.