Operation UKUTA dalili za mapinduzi?

Operation UKUTA dalili za mapinduzi?

Mzururaji

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
1,558
Reaction score
1,274
Wakat CHADEMA wakiendelea na maandalizi yao ya operation UKUTA ambapo wamepanga kuzunguka nchi nzima kwa kufanya mikutano mimi kwa upande wangu naona sasa hizi ni dalili za jaribio la wazi la mapinduzi kwa serikali inayoongozwa na Mhe, JPM.

Bara la afrika na nchi nyinginezo duniani tulizoea kuona mapinduzi mengi kutokea jeshini ambapo wanajeshi hujikusanya wale wenye uchu wa madaraka halafu hupindua serikali halali iliyowekwa na wananchi na wakiingia madarakani huvua magwada na kuanza kuongoza kiraia kuna mifano ya maraisi wengi ambao mpaka Leo wanaongoza lakini waliingia kwa style hiyo mtu kama Museveni na Kagame hawa ni mifano ya mapinduzi ya kijeshi

Lakini kwa sasa bala la Africa linashuhudia style mpya ya mapinduzi, haya yakiongozwa na vyama vya upinzani, Asasi zisizo za ki Raia. Hapa huitwishwa maandamano yasiyo ya kikomo na mikutano isiyo na mwisho mpaka Lengo la wanasiasa hawa la uchu wa madaraka kutimia

Kwanza; Kwa historia ya hivi karibun mapinduzi mengi kwa nchi za afrika yalifanikiwa kwa kupitia style hii ya maandamano na mikutano isiyo na kikomo ambayo yalianza kutangazwa kwa masikhara hivi lakini jinsi siku zilivyosonga mbele ndivyo yalipozidi kupanda chati mpaka kupelekea kushindwa kuyadhibiti nchi kama Misri chini ya Hosn Mubarak, Morocco, Syria na nchi nyinginezo. Maandamano ya aina hii yamewezekana baada ya maandalizi ya mizaha kama haya yaliotangazwa ya UKUTA


Pili; Nia ya mwanasiasa yeyote ni kukamata dola hapa ndipo utakapoona njia mbalimbali zikitumia ambayo ya mwisho huwa kama hii ya maandamano nchi nzima kwa kukaidi katazo halali kutoka mamlaka halali kabisa la kuzuia maandamano ama mikutano yenye dalili ya uvunjifu wa amani kwa nchi nzima hivyo kupelekea mapinduzi

Baada ya mapinduzi ya aina hii ndipo mlolongo wa uvunjifu wa amani ukiendelea kama mauaji ya raia wasio na hatia pato la taifa kushuka, wizi ubakaji na mambo mengine kama hayo.

Hivyo basi kwa kumshauri Mhe, raisi wahenga walisema mchelea mwana kulia hulia yeye yaan ukicheka na hii mizaha kama ya UKUTA ipo utakimbia hii nchi ukaishi uhamishoni huku ukiwaacha wanasiasa wenye uchu wa kwenda ikulu kwa njia yoyote wakiwa ikulu

CHADEMA ya sasa imekamatwa na watu wa aina hiyo ambapo wamekuwa wakiitafuta ikulu wa miaka mingi sana na kwa gharama kubwa sana hapa ndipo utakapoona juhudi kama fedha ikibidi usaliti wa wao kwa wao na njia nyinginezo ovu hapa ndipo utagundua operation UKUTA ndio njia ya mwisho waliyokuwa wanaisubiri kwa hamu sana kama tiketi ya kuwapeleka ikulu ya Tanzania

Mhe Rais kupitia dola wekeni mikakati imara ili kuweza kudhibiti hali hii mapema sana kabla haileta machafuko na uvunjifu wa aman kwa mzaha zaha mwisho hutumbua usaha na hapa tunasema mzaha mzaha nchi inaweza kutumbukia kwenye machafuko.

Mwisho, Niwashauri viongozi wa CHADEMA wote kwa ujumla kuanzia tawi mpaka taifa kuingia katika operation UKUTA mkiwa na familia zenu yaani baba mama na watoto kwani ninyi ndio mtakaofaidika na baada ya maandamano kabla ya sisi wananchi mnaosema mnatupigania

Pia Mhe, raisi endelea kuboresha maisha ya wananchi wako ili upate uungwaji mkono kutoka kwa wananchi wako wa kawaida kwa ujumla wao wakiweko wafanyakazi wakulima na wafanyabiashara hapa ndo utaona umuhimu wake kama yaliyotokea UTURUKI ambapo wananchi kwenye nia Njema na wakawaida kabisa walijaribu kuzima jaribio la mapinduzi, hawa wananchi walijua fika hii ni kete ya nchi yao kuingia kwenye machafuko.

Kwa sasa acha niishie hapa nikaendelee na jukumu langu la uzururaji huku niendelea kuiombea nchi yangu.
 
Unalijua zuio halali kwanza??? Hamna zuio halali linalopingana na katiba,anayekiuka katiba ya nchi ndiye muhaini
kwan polisi sio mamlaka halali hata kama kuna weza kutokea uvunjifu Wa aman kisa tuu katiba imeruhusu
 
Uvunjifu gani huo unaousema? Kwa hiyo walio madarakan hawana uchu wa madaraka?? Acheni kutisha watu. Acheni watu watoe mawazo yao...naona mnayakana maneno mliokuwa mnaimba wakati wa kampeni....
Waacheni waandamane eee.....
 
Nakubaliana na wewe mleta mada kwa asilimia kadhaa.

Lakini jambo ambalo linanipa wasiwasi ni jinsi hawa watu wa UKUTA wanavyopanga hii kitu.

Ingekuwa vizuri sana kama wao wenyewe kwanza wangeelewana ili kila mtu awe na nia ya dhati ya kushiriki katika hayo maandamano,lakini kwa jinsi mimi ninavyowajua hawa CHADEMA wameshatoa matamko mengi sana ambayo baadhi tu ndiyo yametekelezwa.....

Pia kama hawa jamaa kweli watauwa na nia ya kushika madaraka kwa njia ya mapinduzi ilibidi kwanza wapate wananchi wa vijijini ambao ndiyo asilimia kubwa lakini kitendo cha hawa jamaa kukaa tu mjini kitakuwa ni kikwazo katika kufikia haya unayosema mtoa mada.

CHADEMA pia inabidi wajifunze kuwa na "common say" siyo kila mtu ndani ya chama anakuwa msemaji,kitu ambacho kinaleta picha mbaya kwamba wenyewe hawana msimamo na wanachokipigania.....
 
Uvunjifu gani huo unaousema? Kwa hiyo walio madarakan hawana uchu wa madaraka?? Acheni kutisha watu. Acheni watu watoe mawazo yao...naona mnayakana maneno mliokuwa mnaimba wakati wa kampeni....
Waacheni waandamane eee.....
hakuna aliye yakana ila nime angalia kwa jicho la tatu
 
Unalijua zuio halali kwanza??? Hamna zuio halali linalopingana na katiba,anayekiuka katiba ya nchi ndiye muhaini

Kwani mikutano si taratibu zake kwa mujibu wa katiba hiyo hiyo na sheria ya political parties act ambapo mkuu wa POLISI wa eneo husika ana mamlaka ya kuzuia mikusanyiko yenye kuashiria uvunjufu wa amani au yenye kasoro mbali mbali, usiropoke usiyoyajua, we subiri kuvunjwa uti wa mgongo tu.
 
Huu ndio uchochezi ulovuka mipaka. Yaani wewe unatakiwa kuhojiwa kwa kuleta uchochezi dhidi ya serikali na vyama vya siasa.

Misri sio tanzania..hakuna vyama kisheria, hakuna katiba inayotambua vyama vingi
Libya pia haikua na vyama vingi

Na Tunisia pia
Umetaja mifano hio kuleta uchochezi ...

Wapinzani hawadai jengine ila kupewa uhuru wa kikatiba ambao uko wazi..nao ni uhurru wa kukosoa na kufanya mikutano kuendesha shughuli za vyama vyao...wamefanya hivi miaka 23 sasa ...iweje uchochee sasa
 
Una maana gani unaposema "wanazunguruka nchi nzima" au una matatizo ya ulimi
 
Kwanza; kwa historia ya hivi karibun mapinduzi mengi kwa nchi za afrika yalifanikiwa kwa kupitia style hii ya maandamano na mikutano isiyo na kikomo ambayo yalianza kutangazwa kwa masikhara hivi lakini jins siku zilivyo songa mbele ndivyo yalipo zidi panda chati mpaka kupelekea kushindwa kuyadhibiti nchi kama misri chini ya hosn Mubarak Morocco, Syria na nchi nyinginezo. Maandamano ya aina hii yamewezekana baada ya maandalizi ya mizaha kama haya Yalio tangazwa ya UKUTA
Kuna dhana ya miaka ya zamani sana iliyokuwa ikisema lengo la chama chochote cha siasa ni kushika dola lakini wanasayansi wa siasa za kisasa wanapinga wazi kauli hizo kuwa chama cha siasa kama lengo lake ni kushika dola uwezekano wa kufanikiwa ni mdogo.

Wanasayansi wa siasa za kisasa wanabainisha kuwa lengo lolote la chama chochote cha siasa iwe ni kushika mioyo ya wananchi walio wengi ambao mbeleni ndio wawezao kukipa kura na kukiingiza madarakani kupitia sanduku la kura.

Vyama ambavyo lengo lake hulenga tu kushika dola huwa havishughuliki na wananchi walio wengi hujikita zaidi kushughulika na walio wachache.Na kwa sababu hiyo huwa havifanikiwi kushika dola.

Mfano Alkaeda,ISIS, vyama vilivyohusika na Arab springs huko moroco,algeria,Libya,MISRI nk na Alshabab ni makundi au vyama ambavyo lengo lake ni kukamata dola katika nchi mbalimbali.Lakini pamoja na kuwa na lengo hilo kwa kuwa hawakulenga kushika mioyo ya wananchi walio wengi kushika dola imekuwa haiwezekani na ni shida kwao kutokana na ukosefu wa kuungwa mkono na walio wengi ambao hawakuwalenga toka mwanzo.Ndio unaona nchi nyingi kama Libya,misri,algeria,uturuki,yemen nk kote vyama hivyo vilivyokuwa lengo lao ni kushika dola tu havipati mafanikio nchi hazitawaliki mambo hayaendi na wao hawashiki nchi kama akina Gadafi walivyokuwa wakiweza ambao walilenga kushika mioyo ya walio wengi.

CHADEMA inafanya kosa lile lile inasema lengo lake ni kushika dola lakini ukitizama mikakati yake unaona imejikita kabisa sio kuingia na kukubalika kwa walio wengi bali kukubalika na walio wachache

mifano
1.Bungeni walisusa bunge wakitaka maslahi yao wao wachache yasikilizwe.Walitaka bunge lionyeshwe live ili wao wachache waonekane.Wakati lengo la bunge na wanachoendea bungeni ni kuwakilisha hoja za walio wengi waliowatuma kwa mawaziri husika ili kero zitatuliwe.Kwa hivyo kwa kufanya hivyo kunawafanya wao kukosa kuingia na kuiteka mioyo ya watanzania walio wengi ambao mahitaji yao sio bunge LIVE wanahitaji huduma nzuri za afya,maji,elimu nk

2.Muda mwingi CHADEMA wanashindana na watu wachache (viongozi wa serikali,Bunge na mahakama) badala ya kujikita kwa wananchi walio wengi kuwasaidia kimaendeleo ili wawapende.Muda mwingi na nguvu nyingi zinatumika kushindana na raisi,polisi,viongozi wa serikali,viongozi wa bunge kama Tulia,Mahakamani kila siku kushindana na mahakimu na majaji.Muda mwingi wanahangaika na wachache!!!!!!!

3.Ukiangalia mkakati wao wa utetezi wa kutetea watu unaona wakifanya utetezi wanatetea zaidi walio wachache mfano wezi,wakwepa kodi na wanaotumbuliwa na Magufuli,Majambazi ambayo Raisi kaagiza yashughulikiwe papo kwa papo,Mabalozi wa nje ambao hawaruhusiwi kuzurura huko na huko bila kibali cha wizara ya mambo ya nchi za nje!Ukiangalia makundi wanayoyatetea ni ya wachache hayagusi walio wengi

4.Ukiangalia pia mkakakati wa maandamano,ubabe na vurugu pia una walakini.Jamii ya watanzania walio wengi hawapendi maandamano,siasa za ubabe wala vurugu.Ni watanzania wachache mno wenye kupenda hayo mambo.Hapa pia unaona wazi kuwa CHADEMA wanalenga zaidi kwa walio wachache kuliko walio wengi katika mikakati yao ya maandamano,ubabe wa kisiasa na vurugu.Hivi hata kwa akili za kawaida hawajawasoma watanzania walio wengi kuwajua wakoje?

Nikitizama CHADEMA kama mlipa kodi ambaye kodi zangu zinatumika kwa ruzuku naona CHADEMA wanatumia mkakati uliopitwa na wakati wa kuamini kuwa Lengo kuu la chama cha siasa ni kushika dola kwa namna yoyote iwe kwa maandamano,vurugu,migomo nk Hawako sahihi
 
Hii topicc ni garbage at high level, kufanya mapindui kunahitaji jeshi, kunahitaji watu waliofunzwa silaha, kunahitaji silaha, kunahitaji pesa nyingi tu kama utatumia askari wa kukodi hebu toa ushahidi kwa vigezo hivyo na si kutisha, naona mleta mada bado yupo usingizini akiamini kutisha kunaweza okoa jahazi
 
Hii topicc ni garbage at high level, kufanya mapindui kunahitaji jeshi, kunahitaji watu waliofunzwa silaha, kunahitaji silaha, kunahitaji pesa nyingi tu kama utatumia askari wa kukodi hebu toa ushahidi kwa vigezo hivyo na si kutisha, naona mleta mada bado yupo usingizini akiamini kutisha kunaweza okoa jahazi
Kwani jeshi la waasi huwa linajianika wazi? Huwenda liko msituni tutajuaje?
 
Kuna dhana ya miaka ya zamani sana iliyokuwa ikisema lengo la chama chochote cha siasa ni kushika dola lakini wanasayansi wa siasa za kisasa wanapinga wazi kauli hizo kuwa chama cha siasa kama lengo lake ni kushika dola uwezekano wa kufanikiwa ni mdogo.

Wanasayansi wa siasa za kisasa wanabainisha kuwa lengo lolote la chama chochote cha siasa iwe ni kushika mioyo ya wananchi walio wengi ambao mbeleni ndio wawezao kukipa kura na kukiingiza madarakani kupitia sanduku la kura.

Vyama ambavyo lengo lake hulenga tu kushika dola huwa havishughuliki na wananchi walio wengi hujikita zaidi kushughulika na walio wachache.Na kwa sababu hiyo huwa havifanikiwi kushika dola.

Mfano Alkaeda,ISIS, vyama vilivyohusika na Arab springs huko moroco,algeria,Libya,MISRI nk na Alshabab ni makundi au vyama ambavyo lengo lake ni kukamata dola katika nchi mbalimbali.Lakini pamoja na kuwa na lengo hilo kwa kuwa hawakulenga kushika mioyo ya wananchi walio wengi kushika dola imekuwa haiwezekani na ni shida kwao kutokana na ukosefu wa kuungwa mkono na walio wengi ambao hawakuwalenga toka mwanzo.Ndio unaona nchi nyingi kama Libya,misri,algeria,uturuki,yemen nk kote vyama hivyo vilivyokuwa lengo lao ni kushika dola tu havipati mafanikio nchi hazitawaliki mambo hayaendi na wao hawashiki nchi kama akina Gadafi walivyokuwa wakiweza ambao walilenga kushika mioyo ya walio wengi.

CHADEMA inafanya kosa lile lile inasema lengo lake ni kushika dola lakini ukitizama mikakati yake unaona imejikita kabisa sio kuingia na kukubalika kwa walio wengi bali kukubalika na walio wachache

mifano
1.Bungeni walisusa bunge wakitaka maslahi yao wao wachache yasikilizwe.Walitaka bunge lionyeshwe live ili wao wachache waonekane.Wakati lengo la bunge na wanachoendea bungeni ni kuwakilisha hoja za walio wengi waliowatuma kwa mawaziri husika ili kero zitatuliwe.Kwa hivyo kwa kufanya hivyo kunawafanya wao kukosa kuingia na kuiteka mioyo ya watanzania walio wengi ambao mahitaji yao sio bunge LIVE wanahitaji huduma nzuri za afya,maji,elimu nk

2.Muda mwingi CHADEMA wanashindana na watu wachache (viongozi wa serikali,Bunge na mahakama) badala ya kujikita kwa wananchi walio wengi kuwasaidia kimaendeleo ili wawapende.Muda mwingi na nguvu nyingi zinatumika kushindana na raisi,polisi,viongozi wa serikali,viongozi wa bunge kama Tulia,Mahakamani kila siku kushindana na mahakimu na majaji.Muda mwingi wanahangaika na wachache!!!!!!!

3.Ukiangalia mkakati wao wa utetezi wa kutetea watu unaona wakifanya utetezi wanatetea zaidi walio wachache mfano wezi,wakwepa kodi na wanaotumbuliwa na Magufuli,Majambazi ambayo Raisi kaagiza yashughulikiwe papo kwa papo,Mabalozi wa nje ambao hawaruhusiwi kuzurura huko na huko bila kibali cha wizara ya mambo ya nchi za nje!Ukiangalia makundi wanayoyatetea ni ya wachache hayagusi walio wengi

4.Ukiangalia pia mkakakati wa maandamano,ubabe na vurugu pia una walakini.Jamii ya watanzania walio wengi hawapendi maandamano,siasa za ubabe wala vurugu.Ni watanzania wachache mno wenye kupenda hayo mambo.Hapa pia unaona wazi kuwa CHADEMA wanalenga zaidi kwa walio wachache kuliko walio wengi katika mikakati yao ya maandamano,ubabe wa kisiasa na vurugu.Hivi hata kwa akili za kawaida hawajawasoma watanzania walio wengi kuwajua wakoje?

Nikitizama CHADEMA kama mlipa kodi ambaye kodi zangu zinatumika kwa ruzuku naona CHADEMA wanatumia mkakati uliopitwa na wakati wa kuamini kuwa Lengo kuu la chama cha siasa ni kushika dola kwa namna yoyote iwe kwa maandamano,vurugu,migomo nk Hawako sahihi
JPM hajaribiwi, waache watatulizwa tu.
 
Poor poor poor / hakuna dalili zozote za mapinduzi hapa!!!, acha hizo,/ nakuuliza ni wapi yalifanyika mapinduzi ukajua tarehe...../ na siku..../

-->>ninalojua ni kwamba maandamano yanaweza tokea,polisi yapaswa wawe makini sana kuangalia jinsi ya kutodhuru mtu au kuua mtu,kwani kwa ufahamu wangu mdogo mauaji hukoleza..Ghasia.../ na hupanda chuki,extreme power zitatugharimu...
"Mungu ibariki tanzania"
 
Back
Top Bottom