Open-Source Intelligence: Silaha ambayo Iran Haikulazimika Kuinunua

Open-Source Intelligence: Silaha ambayo Iran Haikulazimika Kuinunua

zitto junior

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2013
Posts
24,225
Reaction score
39,773
Kwa miaka mingi Marekani imewekeza trilioni za dola kwenye satelaiti, ndege za upelelezi, drones, rada na mashirika ya kijasusi ili kupata taarifa za adui. Lakini inaonekana Iran imegundua njia rahisi zaidi na ya gharama nafuu: bando la jero na kufungua tu TikTok, X, Instagram au Facebook.

Ripoti zinaonyesha kuwa CENTCOM imeanza kuwaonya wanajeshi wake kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii baada ya kubainika kuwa video na picha wanazopakia zinawasaidia wapinzani kuona kwa haraka makombora yamepiga wapi, yameleta uharibifu kiasi gani, na kama kuna haja ya kufanya secondary attack ili kuongeza madhara. Kwa kifupi, baadhi ya wanajeshi walikuwa wanatoa "battle damage assessment" bure kabisa bila kujua.

View: https://youtube.com/shorts/A_iCvFNeiLE?si=plvI0gqT6s5hdUtm

Ni jambo la kuchekesha ukilitazama kwa mbali. Marekani inatumia mabilioni kupeleka satelaiti angani, halafu mtu mmoja akiwa kambini anaamua kupost video ya "Bro, tulipigwa lakini niko salama," na ndani ya dakika chache adui anapata taarifa ambayo ingegharimu mamilioni kuikusanya kwa njia za kawaida.

Hii ndiyo nguvu ya open-source intelligence (OSINT) katika vita vya kisasa. Wakati mwingine taarifa muhimu hazitoki kwa jasusi aliyejificha gizani, bali zinatoka kwa mtu aliyeshika simu na kutafuta likes.


View: https://youtube.com/shorts/2DXnHa5c0mw?si=abXhBvsik4dwSPjJ
Vita vya leo havipiganwi kwa makombora pekee. Vinapiganwa pia kwenye screen za simu. Na wakati mwingine, adui hahitaji kuvunja mfumo wa siri; anasubiri tu mtu "ajimwambafy" maisha yake mtandaoni.

Inaonekana CENTCOM imeamua kwamba silaha rahisi ya kuizuia Iran kupata taarifa si kombora jipya, bali ni kuwaambia wanajeshi wake: "Wekeni simu chini kwanza."

Source: US commander warns troops their videos help Iran, sources say
 
Kwa miaka mingi Marekani imewekeza trilioni za dola kwenye satelaiti, ndege za upelelezi, drones, rada na mashirika ya kijasusi ili kupata taarifa za adui. Lakini inaonekana Iran imegundua njia rahisi zaidi na ya gharama nafuu: bando la jero na kufungua tu TikTok, X, Instagram au Facebook.

Ripoti zinaonyesha kuwa CENTCOM imeanza kuwaonya wanajeshi wake kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii baada ya kubainika kuwa video na picha wanazopakia zinawasaidia wapinzani kuona kwa haraka makombora yamepiga wapi, yameleta uharibifu kiasi gani, na kama kuna haja ya kufanya secondary attack ili kuongeza madhara. Kwa kifupi, baadhi ya wanajeshi walikuwa wanatoa "battle damage assessment" bure kabisa bila kujua.

View: https://youtube.com/shorts/A_iCvFNeiLE?si=plvI0gqT6s5hdUtm

Ni jambo la kuchekesha ukilitazama kwa mbali. Marekani inatumia mabilioni kupeleka satelaiti angani, halafu mtu mmoja akiwa kambini anaamua kupost video ya "Bro, tulipigwa lakini niko salama," na ndani ya dakika chache adui anapata taarifa ambayo ingegharimu mamilioni kuikusanya kwa njia za kawaida.

Hii ndiyo nguvu ya open-source intelligence (OSINT) katika vita vya kisasa. Wakati mwingine taarifa muhimu hazitoki kwa jasusi aliyejificha gizani, bali zinatoka kwa mtu aliyeshika simu na kutafuta likes.


View: https://youtube.com/shorts/2DXnHa5c0mw?si=abXhBvsik4dwSPjJ
Vita vya leo havipiganwi kwa makombora pekee. Vinapiganwa pia kwenye screen za simu. Na wakati mwingine, adui hahitaji kuvunja mfumo wa siri; anasubiri tu mtu "ajimwambafy" maisha yake mtandaoni.

Inaonekana CENTCOM imeamua kwamba silaha rahisi ya kuizuia Iran kupata taarifa si kombora jipya, bali ni kuwaambia wanajeshi wake: "Wekeni simu chini kwanza."

Source: US commander warns troops their videos help Iran, sources say

Niliwahi kugundua sehemu mke wangu anakutana na mchepuko wake kwa kutumia "metadata" za picha zake za Instagram & Facebook na "Geotag".

Open Source Intelligence inasaidia kwa watu wasio makini na teknolojia.
 
OSINT kwa mara ya kwanza naiona inatumika serious ni kwenye vita ya Nagorno-Karabakh.
Baadae kwenye vita ya Urusi OSINT imetumika sana hasa mwanzoni dhidi ya upande wa Urusi, maana Ukraine ndio walianzisha targeted attacks.

Israel ilipoanza kuzuia waandishi wa habari kupost picha na video za maafa ya mashambulizi ya Iran, Watindiga wa huku kwetu wakaanza kusema Israel inaficha madhara. Kumbe Israel inajijua ina eneo dogo sana, ukionyesha launch site hata moja tu inaweza kuwa geo-located ikaonekana ilipo.

OSINT inawafaa sana upande wa wanyonge, maana ni ya kutegeshea uzembe wa adui yako au kujiamini sana kwake. Upande superior hauitegemei maana una means za kufanya battle damage assessment. Urusi ilivyopiga marufuku maofisa wake kujiamini na kuwa exposed na apps za mazoezi na camera hovyo, mashambulizi ya Ukraine dhidi yao yalipungua sana.

Pia kwenye maisha ya kawaida rapper PnB Rock aliuwawa na vibaka kisa girlfriend wake alipost live location Instagram.
 
Pia kwenye maisha ya kawaida rapper PnB Rock aliuwawa na vibaka kisa girlfriend wake alipost live location Instagram.
Aisee ni hatari sana hii, pengine hata Polepole kuna hesabu ndogo alijisahau kwenye kuruka live na baadhi ya "clues" zikaonekana na jamaa ikawa rahisi kujua alipo.

Hapa tulipofika mitandao imekua source kubwa ya kijasusi ukizingatia uwepo wa vitu kama Google lens au reverse image search inaweza kutrack ulipo hata kwa detail ndogo sana
 
Niliwahi kugundua sehemu mke wangu anakutana na mchepuko wake kwa kutumia "metadata" za picha zake za Instagram & Facebook na "Geotag".

Open Source Intelligence inasaidia kwa watu wasio makini na teknolojia.
Hatari sana teknolojia na kwa sisi wabongo ambavyo hana "digital literacy" tunaweza kujua pattern ya maisha ya mtu kwa kuangalia tu status zake za WhatsApp na Facebook na ukaweza kuunganisha dots kwamba ni nani, anafanya kazi wapi, anapenda kutembelea wapi n.k inarahisisha utapeli na hata mtu kukudhuru kama ana nia mbaya.
 
Lakini nani aliweza kuamini kama mbabe wa dunia anachapwa na kinchi alicho iwekea vikwaze miaka zaidi ya arubaini.

Zile movies za Rambo na Komandoo kumbe upuuzi mtupu🤣🤣
Propaganda zilikua nyingi sana, Imagine kambi zinalindwa na radar za mabilion ya dollar na makombora tuliyoambiwa hayakosagi shabaha ila kambi zinashushiwa mvua ya makombora mpaka wanapoteana.

Sasa fikiria Iran isingekua na vikwazo kwa miaka 45 hali ingekuaje
 
Aisee ni hatari sana hii, pengine hata Polepole kuna hesabu ndogo alijisahau kwenye kuruka live na baadhi ya "clues" zikaonekana na jamaa ikawa rahisi kujua alipo.

Hapa tulipofika mitandao imekua source kubwa ya kijasusi ukizingatia uwepo wa vitu kama Google lens au reverse image search inaweza kutrack ulipo hata kwa detail ndogo sana
Hata zamani kabla ya mitandao, ujasusi unafanya mambo mengi kwa taarifa ndogo ndogo. Ila sio majasusi wetu hawa wa unanijua mimi nani.

CIA walipiga picha kila member aliyehudhuria Nuremberg trials kutoka pande zote, waliamua kuhisi kuwa mtu wa kawaida tu hawezi letwa na serikali mahakamani kuja kushuhudia. Miaka kama 30 baadae ndio walikuja kugundua wana picha ya Markus Wolf, mkuu wa Foreign Intelligence ya STASI, shirika la kijasusi la East German.

Sasa Wolf alijulikana vipi, West Germany ilikuwa na chama cha siasa hiki tawala cha sasa SPD. Muhula ule kilikuwa upinzani, intelligence ya West Germany ikaonyesha kada wake muhimu wa SPD anaenda Sweden kukutana na mtu anaitwa Dr. Werner. Ikawataarifu majasusi wa Sweden.

Swedish intelligence wakafuatilia huyo mpinzani anaongea na nani. Sasa cha ajabu wakashangaa huyu Dr. Werner mbona yuko very sophisticated, ana umakini mkubwa kwenye kila hatua, ana manouvers kali mno kama trained spy aliyefuzu viwango vya juu sana, movements zake kama boss hivi sio rank za chini, tena alikuwa na mke wake naye ni kama spy aliyeiva. Cha ajabu hakuwa na mlinzi hata mmoja.

Swedish wakaona hakuna mtalii au kigogo wa serikali ana sifa za hivi. Wakatumia kamera za kijasusi kumpiga picha nyingi tu. Alikuja kutambuliwa miezi ya baadae kama mkuu wa foreign intelligence, miaka 26 baada ya kuwaumiza sana maadui wa nchi yake.

Kwahiyo suala la picha, video na vifaa vya mawasiliano vina matokeo kwenye usalama.
Ndio maana Osama bin Laden hakuwa na simu, laptop wala radio communication. Yeye ni mwendo wa kijumbe tu, kijumbe anawasiliana na watu ambao hawajui Osama yuko wapi.
 
Hata zamani kabla ya mitandao, ujasusi unafanya mambo mengi kwa taarifa ndogo ndogo. Ila sio majasusi wetu hawa wa unanijua mimi nani.

CIA walipiga picha kila member aliyehudhuria Nuremberg trials kutoka pande zote, waliamua kuhisi kuwa mtu wa kawaida tu hawezi letwa na serikali mahakamani kuja kushuhudia. Miaka kama 30 baadae ndio walikuja kugundua wana picha ya Markus Wolf, mkuu wa Foreign Intelligence ya STASI, shirika la kijasusi la East German.

Sasa Wolf alijulikana vipi, West Germany ilikuwa na chama cha siasa hiki tawala cha sasa SPD. Muhula ule kilikuwa upinzani, intelligence ya West Germany ikaonyesha kada wake muhimu wa SPD anaenda Sweden kukutana na mtu anaitwa Dr. Werner. Ikawataarifu majasusi wa Sweden.

Swedish intelligence wakafuatilia huyo mpinzani anaongea na nani. Sasa cha ajabu wakashangaa huyu Dr. Werner mbona yuko very sophisticated, ana umakini mkubwa kwenye kila hatua, ana manouvers kali mno kama trained spy aliyefuzu viwango vya juu sana, movements zake kama boss hivi sio rank za chini, tena alikuwa na mke wake naye ni kama spy aliyeiva. Cha ajabu hakuwa na mlinzi hata mmoja.

Swedish wakaona hakuna mtalii au kigogo wa serikali ana sifa za hivi. Wakatumia kamera za kijasusi kumpiga picha nyingi tu. Alikuja kutambuliwa miezi ya baadae kama mkuu wa foreign intelligence, miaka 26 baada ya kuwaumiza sana maadui wa nchi yake.

Kwahiyo suala la picha, video na vifaa vya mawasiliano vina matokeo kwenye usalama.
Ndio maana Osama bin Laden hakuwa na simu, laptop wala radio communication. Yeye ni mwendo wa kijumbe tu, kijumbe anawasiliana na watu ambao hawajui Osama yuko wapi.
Umenikumbusha Hermman Gouring.
 
Makala nzuri sana hii.
Kwa kifupi Marekani kakutana vita ambayo hakuitarajia.
Kashikwa pabaya sana.
Atatafuta Kila aina ya mchawi.
Iran ni ndogo sana Kwa Marekani, Marekani hakutakiwa kulalamikia vitu vidogo.
Hapa vita hii ndipo ilipotakiwa Marekani aoneshe U supa pawa wake,lkn imekua kinyume.
Aliwalaumu NATO kua hawamaaidii,
Amewalaumu, Urusi,akawalaumu China,Sasa anawakataza wanajeshi wake wasitumiane picha.
Lakini mashambulizi dhidi Yao yataendelea TU.
Juzi TU katoka kujisifu kuhusu Venezuela Leo Kila siku anaomba kusimamisha vita kwa muda ili akachimbe sawa,kumbe anajikuaanya upya.
 
OSINT kwa mara ya kwanza naiona inatumika serious ni kwenye vita ya Nagorno-Karabakh.
Baadae kwenye vita ya Urusi OSINT imetumika sana hasa mwanzoni dhidi ya upande wa Urusi, maana Ukraine ndio walianzisha targeted attacks.

Israel ilipoanza kuzuia waandishi wa habari kupost picha na video za maafa ya mashambulizi ya Iran, Watindiga wa huku kwetu wakaanza kusema Israel inaficha madhara. Kumbe Israel inajijua ina eneo dogo sana, ukionyesha launch site hata moja tu inaweza kuwa geo-located ikaonekana ilipo.

OSINT inawafaa sana upande wa wanyonge, maana ni ya kutegeshea uzembe wa adui yako au kujiamini sana kwake. Upande superior hauitegemei maana una means za kufanya battle damage assessment. Urusi ilivyopiga marufuku maofisa wake kujiamini na kuwa exposed na apps za mazoezi na camera hovyo, mashambulizi ya Ukraine dhidi yao yalipungua sana.

Pia kwenye maisha ya kawaida rapper PnB Rock aliuwawa na vibaka kisa girlfriend wake alipost live location Instagram.
Kabisa...zile Himars za Ukraine ziliisumbua sana Urusi mpaka walipojirekebisha.
 
Aisee ni hatari sana hii, pengine hata Polepole kuna hesabu ndogo alijisahau kwenye kuruka live na baadhi ya "clues" zikaonekana na jamaa ikawa rahisi kujua alipo.

Hapa tulipofika mitandao imekua source kubwa ya kijasusi ukizingatia uwepo wa vitu kama Google lens au reverse image search inaweza kutrack ulipo hata kwa detail ndogo sana
Hatari sana...

Hii mitandao inahifadhi kumbukumbu kila unapotumia hivyo ni rahisi watu wanaokutafuta kupata pa kuanzia.

Polepole kama hakusalitiwa basi huenda kuna namna walimuwinda kupitia mawasiliano yake.
 
Kwa miaka mingi Marekani imewekeza trilioni za dola kwenye satelaiti, ndege za upelelezi, drones, rada na mashirika ya kijasusi ili kupata taarifa za adui. Lakini inaonekana Iran imegundua njia rahisi zaidi na ya gharama nafuu: bando la jero na kufungua tu TikTok, X, Instagram au Facebook.

Ripoti zinaonyesha kuwa CENTCOM imeanza kuwaonya wanajeshi wake kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii baada ya kubainika kuwa video na picha wanazopakia zinawasaidia wapinzani kuona kwa haraka makombora yamepiga wapi, yameleta uharibifu kiasi gani, na kama kuna haja ya kufanya secondary attack ili kuongeza madhara. Kwa kifupi, baadhi ya wanajeshi walikuwa wanatoa "battle damage assessment" bure kabisa bila kujua.

View: https://youtube.com/shorts/A_iCvFNeiLE?si=plvI0gqT6s5hdUtm

Ni jambo la kuchekesha ukilitazama kwa mbali. Marekani inatumia mabilioni kupeleka satelaiti angani, halafu mtu mmoja akiwa kambini anaamua kupost video ya "Bro, tulipigwa lakini niko salama," na ndani ya dakika chache adui anapata taarifa ambayo ingegharimu mamilioni kuikusanya kwa njia za kawaida.

Hii ndiyo nguvu ya open-source intelligence (OSINT) katika vita vya kisasa. Wakati mwingine taarifa muhimu hazitoki kwa jasusi aliyejificha gizani, bali zinatoka kwa mtu aliyeshika simu na kutafuta likes.


View: https://youtube.com/shorts/2DXnHa5c0mw?si=abXhBvsik4dwSPjJ
Vita vya leo havipiganwi kwa makombora pekee. Vinapiganwa pia kwenye screen za simu. Na wakati mwingine, adui hahitaji kuvunja mfumo wa siri; anasubiri tu mtu "ajimwambafy" maisha yake mtandaoni.

Inaonekana CENTCOM imeamua kwamba silaha rahisi ya kuizuia Iran kupata taarifa si kombora jipya, bali ni kuwaambia wanajeshi wake: "Wekeni simu chini kwanza."

Source: US commander warns troops their videos help Iran, sources say

Hizo story za vijiweni unaona ndo facts za mbinu za kupambana na marekani.
 
Back
Top Bottom