Godi haule
Member
- Nov 15, 2022
- 6
- 11
Kwanini NSSF Wasiweke Mfumo wa Riba Kwenye Michango ya Wanachama Wao?
NSSF chini ya sheria yake inamuagiza mwajiri kuwasilisha 20% ya ujira wa kila mfanyakazi wake kila mwezi, ambapo sheria inaeleza mfanyakazi hatakiwi kuchangia zaidi ya 50% ya kiwango hicho.
Fedha hizi huwekezwa kwenye miradi mbalimbali ambayo lengo ni kutengeneza faida.
Kama lengo la uwekezaji ni kutengeneza faida, kwanini mchangiaji hapati chochote kama gawio/riba kwenye michango yake kutoka kwenye hiyo faida?
Nchini India kuna India’s Employees’ Provident Fund (EPF), EPF ni sawa na NSSF kwa hapa Tanzania.
EPF huwekeza fedha za michango ya wanachama wake katika sehemu mbalimbali kama vile hati fungani za serikali & hisa.EPF haiishii hapo; wao hutoa riba kwa wachangiaji wake kwa kiwango cha 8% hadi 9% kwa mwaka, lengo ni kumuandalia mazingira mazuri mchangiaji anapostaafu/kuchukua mafao yake kwani atakua na pesa ndefu itayompa nafuu ya maisha baada ya utumishi.
Swali la kujiuliza; Kama NSSF inatengeneza faida kutokana na uwekezaji wa michango ya wanachama wake kwenye miradi mbaliambali, kwanini mchangiaji asifaidike na hilo hata kupitia riba kwenye michango yake?
Hii haitakuza mfuko wa mwanachama pekee, bali itahamasisha hata wale ambao sio waajiriwa wataona umuhimu wa kujiwekea akiba kwa kupeleka michango yao NSSF.
NSSF chini ya sheria yake inamuagiza mwajiri kuwasilisha 20% ya ujira wa kila mfanyakazi wake kila mwezi, ambapo sheria inaeleza mfanyakazi hatakiwi kuchangia zaidi ya 50% ya kiwango hicho.
Fedha hizi huwekezwa kwenye miradi mbalimbali ambayo lengo ni kutengeneza faida.
Kama lengo la uwekezaji ni kutengeneza faida, kwanini mchangiaji hapati chochote kama gawio/riba kwenye michango yake kutoka kwenye hiyo faida?
Nchini India kuna India’s Employees’ Provident Fund (EPF), EPF ni sawa na NSSF kwa hapa Tanzania.
EPF huwekeza fedha za michango ya wanachama wake katika sehemu mbalimbali kama vile hati fungani za serikali & hisa.EPF haiishii hapo; wao hutoa riba kwa wachangiaji wake kwa kiwango cha 8% hadi 9% kwa mwaka, lengo ni kumuandalia mazingira mazuri mchangiaji anapostaafu/kuchukua mafao yake kwani atakua na pesa ndefu itayompa nafuu ya maisha baada ya utumishi.
Swali la kujiuliza; Kama NSSF inatengeneza faida kutokana na uwekezaji wa michango ya wanachama wake kwenye miradi mbaliambali, kwanini mchangiaji asifaidike na hilo hata kupitia riba kwenye michango yake?
Hii haitakuza mfuko wa mwanachama pekee, bali itahamasisha hata wale ambao sio waajiriwa wataona umuhimu wa kujiwekea akiba kwa kupeleka michango yao NSSF.