Ongea ya Mbowe na watu kukaa kimya

Ongea ya Mbowe na watu kukaa kimya

eden kimario

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2015
Posts
10,356
Reaction score
16,400
WanaJF,

Ni mara ya tatu katika mikutano yake ilianza kule Mbeya ikaja Arusha na jana Mwanza kila ikifika muda wa mwenyekiti wa CHADEMA kuongea hata kama watu walikuwa wakisemezana basi wananyamaza ili kutega sikio lao kumsikiliza huyu jamaa. Nimekuwa najiuliza kwanini ila sijapata majibu halafu ni yeye tu uwanja unakuwa tulivu mpaka nashangaa.Ukiacha baba wa taifa yeye ni wa pili watu wote wanakuwa makini kumsikiliza, kwanini inakuwa hivyo?
 
Kwa sababu lile dili la kumkaribisha Lowasa Ukawa na kudai sio fisadi liliwashangaza watu.

Hivyo akisimama kuongea watu wanasikiliza kujua atakuja na mpya gani.
 
Mkuu hata bungeni ilikuwa hivyo hivyo, kila aongeapo bunge zima hata wale wagonga meza wanatulia
 
Kila Mmoja Anataka Ajue Anatoa Speech Gani? Maana Ni Mzee Wa Speech Zenye Mashiko
 
anafanana sana na baba wa nchi kuanzia sauti hadi face ni kopraiti hata madaraka na makongoro hawamfikii
 
Kwa sababu lile dili la kumkaribisha Lowasa Ukawa na kudai sio fisadi liliwashangaza watu.

Hivyo akisimama kuongea watu wanasikiliza kujua atakuja na mpya gani.
Ndugu yangu utapoteza muda tu kuleta hizi porojo,watanzania hata hawana muda wa kukusikiliza wao wameshaamua bora nusu shari kuliko shari kamili....muulize Humphrey Polepole,alikuwa anasikilizwa na kupendwa balaa lakini kaanza tu kumshambulia nusu shari wa watanzania tayari tumeshaanza na kumpoteza......nenda na wakati maana hata maandiko yaliandika.....Kila jambo na wakati wake....
 
Wana jf ni mara ya tatu katika mikutano yake ilianza kule mbeya ikaja arusha na jana mwanza kila ikifika muda wa mwenyekiti wa chadema kuongea hata kama watu walikua wakisemezana basi wananyamaza ili kutega sikio lao kumsikiliza huyu jamaa nimekua najiuliza kwa nini ila sijapata majibu halafu ni yeye tu uwanja unakua tulivu mpaka nashangaa ukiacha baba wa taifa ye ni wa pili watu wote wanakua makini kumsikiliza kwa nini inakua hivyo??!!

Kauza chama huyo
 
Ulishawahi kuhudhuria mikutano mingapi kijana?
 
Me nafikiri ni mimi mwenyewe naonaga hivyo kumbe wengi hata jana kuna watu walihoji hili swala kwanin Mbowe akiongea kuna ukimya mkubwa sana na sauti yake inakuwa nzito na kubwa sana unaisikia vizuri.
 
Anafaa kwani katuletea Lowassa na marafiki zake fisadi na kumpoteza dr slaa.
 
Mbowe alipewa uwezo wa kipekee wa kujenga hoja na kuhamasisha hadhira yake... Amekuwa akifanya hivyo toka miaka ile akiwa anazunguka mwenyewe na chopa...!!!Hadi leo hii jamaa bado hajakata tamaa bali anazidi kusonga mbele...!! Go, go, go, #Kamanda Mbowe..!!
 
Ndugu yangu utapoteza muda tu kuleta hizi porojo,watanzania hata hawana muda wa kukusikiliza wao wameshaamua bora nusu shari kuliko shari kamili....muulize Humphrey Polepole,alikuwa anasikilizwa na kupendwa balaa lakini kaanza tu kumshambulia nusu shari wa watanzania tayari tumeshaanza na kumpoteza......nenda na wakati maana hata maandiko yaliandika.....Kila jambo na wakati wake....

Mkuu nimetoa maoni yangu kulingana na swali la mleta mada.
 
Kwa kweli hotuba zake huwa ni tamu sana, hakuna anayependa apitwe na hata neno moja, kama siasa kipaji basi Mbowe kajaaliwa
 
Back
Top Bottom