Ona haya maajabu ya BVR sasa

Ona haya maajabu ya BVR sasa

Nimejiandikishia Kagera lkn kituo changu cha kazi ni Kigoma hii ina maana ya kwamba hata siku ya uchaguzi nitakuwa Kigoma

Nadhani kutakuwa na muda wa kuhakiki wale waliohama vituo,sina uhakika kama na mwaka huu hii Tume ya Mkude Simba itafanya.Lakini utapiga kaka
 
Katoe taarifa kwa mkurugenzi wako wa uchaguzi, yaani mkurugenzi wa wilaya huko kigoma. Yeye ataandika barua kwenda kwa tume aki quote namba yako ya kadi, kituo ulichojiandikishia na kituo kipya utakacho pigia kura. Halafu tume itabadilisha na utapiga kura. Usi panic

Naona kama hili ni wazo zuri tatizo nitamkuta ofisini au atanisikiliza kweli kabla sijatolewa nduki na PS wake
 
Jamani naombeeni msaada juu ya hili. Hili zoezi la kujiandikisha kupiga kura limenikuta nje ya mkoa wangu maana nilisafiri kikazi nikaja mkoani Kagera. Sasa kule kwetu zoezi linaendelea sawa na hapa Kagera.

Sasa tumeshauliwa eti tukajiandikishe popote pale hivi vitambulisho vitatuwezesha kupiga kura eneo lolote lile Tz.

Sasa baada ya kwenda kujiandikisha huku nilipo watu wananiambia eti kura yangu imeshapotea sitaweza kupiga kura nikiwa nje ya mkoa/kituo nilichojiandikishia.

Sasa nawaza hapa si ndio nishapoteza haki yangu? Maana mm sina shida na kitambuslisho vitambulisho ninavyo vingi nachotaka haki ya kupiga kura.

Halafu walichonishangaza ni kwamba unaandikwa bila kukuuliza document yoyote hii inamaanisha wahamiaji haramu ni rahisi sana kujichomeka hapa.

Ushauri katika hili wataalamu vp nitapiga kura kweli?

= tumeshauriwa
 
Ndugu zangu nimejiandikisha na katika kujiandikisha huko nilimuuliza muandikishaji juu ya uchaguzi kunikutia mahali ambapo sijajiandikishia amenijibu hivi
Unaweza kumchagua rais popote pale utakapokuwepo Tanzania lakini Mbunge na Diwani hutaweza lazima urudi pale ulipojiandikishia ukitaka kuchagua mbunge na diwani' lakini kwa rais ni popote utakapokuwepo

Waongo hao mwaka 2010 tatizo hili tena lilinikumba tena nikiwa mkoa huohuo niliojiandikisha nilivyoenda kupiga kura ya Rais nikaambiwa haiwezekani maana Summation ya kura za urais hufanyika kijimbo kwa hiyo bora nisingekuwa kituo kile kile lkn nikawa ndani ya jimbo nililojiandikisha.

Kwa ufupi mwaka ule niliambiwa hivi.

1. Kura za madiwani hujumlishwa kwa vituo ktk kata na lazima upige kituo chako tu. Hapa utamchagua Diwani, mbunge na Rais

2. Kura za mbunge hujumlishwa kwa kata kwa hiyo unaweza ukawa popote pale lkn uwe ndani ya kata uliyojiandikishia hapa utamchagua Mbunge na rais tu.

3. Kura za Rais hujumlishwa kwa jimbo husika kwa hiyo unaweza kupiga kupiga kura hii ukiwa popote pale lkn ndani ya jimbo ulilojiandikishia. Hapa utamchagua rais tu.

4. Ukiwa nje ya jimbo ulilojiandikisha imekula kwako sijajua kwa BVR nao ni yale yale sasa.
 
Kajiandikishe kwako mkuu hawana uwezo wa kujua duplicate!
Wanadanganyika sana tu!

Ofcn tulikuwa tunabisha, dogo mmoja kajitosa, mpaka ninavyokwambia anavitambulisho viwili tayar, alichofanya ni kubadilisha vituo tu!

Kwa BVR tutachemka sana tumekurupuka

Mna jidanganya tu, halavyo watu wengine ni wagumu sana kuelewa , hizo kiti zinakuwa na local information
Na unaweza kujiandikisha hata mara 10 kwenye vituo tofaut , pala watakapo jiunganisha na vituo vyote kenye data base lazima utaoneka tu na hapo ndio kimbembe kitatokea
 
nilipata kuhudhuria mafunzo ya BVR kama mtia nia kwa maelezo yao kutakua na marekebisho mwezi wa nane kujiandikisha mara mbili ni kosa na adhabu yake ni kifungo cha miaka miwili hapa wilayani kwangu tayari mtu ameshakamatwa vijana tusirubuniwe kufanya makosa ya makusudi labda wawe WAMETUDANGANYA KAMA WALIVYOZOE WAMEZOEA VYA KUCHINJAA.....................
 
Nimejiandikishia Kagera lkn kituo changu cha kazi ni Kigoma hii ina maana ya kwamba hata siku ya uchaguzi nitakuwa Kigoma

washasema wataweka muda wa kuhamisha kumbukumbu ili upigie kule utakapo kuwa
 
Msihangaike kutakuwa na kipindi maalum cha uboreshaji daftari kabla ya uchaguzi. Utakwenda kwa msimamizi wa uchaguzi na utabadilishiwa kituo tena sasa ni rahisi kwa kuwa maelezo yote yako kwenye kadi ya kura. Tume ilikwisha kutoa Maelezo haya.

Naona kama muda si rafiki
 
Mna jidanganya tu, halavyo watu wengine ni wagumu sana kuelewa , hizo kiti zinakuwa na local information
Na unaweza kujiandikisha hata mara 10 kwenye vituo tofaut , pala watakapo jiunganisha na vituo vyote kenye data base lazima utaoneka tu na hapo ndio kimbembe kitatokea

Sawa tukisubir kimbembe!
Labda kama sio Tz hii
 
Back
Top Bottom