On a serious note: CUF halali, acheni kwenda kufanya usafi Jumapili

Stabilaiza

JF-Expert Member
Jul 11, 2012
1,843
1,143
Kama mwananchi, ninatoa wito wa dhati kutoka katika sakafu ya moyo wangu, tena bila hila yoyote ndani mwangu kwamba CUF halali msiende Buguruni Jumapili. Ninafahamu kwamba Lipumba si halali CUF kwa kuwa alishajivua uongozi, CUF ilisharidhia kujiuzulu kwake na alishavuliwa uanachama wa CUF. Hivyo amejipachika uongozi haramu wa CUF. Ikumbukwe kuwa CUF haramu inabebwa na serikali kwa kupitia Msajili wa Vyama vya siasa. Uvamizi walioufanya CUF haramu kwenye mkutano wa waandishi wa habari ulikuwa na support ya wenye dola. Vingenevyo, CUF haramu wangeshafurushwa Buguruni na kupelekwa kunakohusika- Lupango.

CUF halali wasidhani kwamba aliyekatwa kisigino na wabwana zake wamefurahi. Watakuwa wanatafuta muda muafaka wa ku-strike back. Usafi wa jumapili unaweza kuwa fursa ya CUF haramu na mabwana zao kujibu mapigo, ingawa wao ndio waliovamia kikao. Kwa usalama wa CUF halali, ninawaomba wafute mpango wao. Habari hii imufikie Mtatiro Julius ili awaarifu wanachama wa CUF kuhusu kuachana na usafi wa Jumapili. CUF halali waendelee kutumia njia za kidemokrasia na kisheria za kuwafurusha CUF haramu kwenye ofisi zao. Huu ndiyo ujumbe katika uzi huu, uzingatiwe na hatua zichukuliwe haraka ili kuwalinda wananchi dhidi ya uharamia wa CUF haramu na mabwana zao.
 
Cuf haramu wakilianzisha tunawafuata hata kule kwenye vibanda vya kuku tuviangamize. Hatutaki ushari, miezi sita walileta fujo, sasa tuone kama kweli dola inaweza kuwalindia hata migomba yao mashambani. Wewe Khalifa ngoja kwanza nikuporomoshee haya madafu yote katika minazi yako, ili uanze kuona joto.
 
Huu ushauri ni mzuri sana mku. Kumbuka kuna jambo linaendelea mimi na ww hatujui nini kinapangwa kwani mwenzetu ana uwezo wa kutishia kwa bastola lakini hakuchuliwa hatua yeyote. Mimi ushauri wangu ni huu Wabunge Wote wa Cuf wakubaliane kushiriki jambo la kijamii ktk Jimbo moja waanzie na Temeke kwa ajili ya usafi tuu sisi wananchi huku tutaungana nao. Hili la usafi mtakuwa mmeonyesha njia nzuri ya kuonyesha hakuna anayekubaliana na Lipumba Kuanzia kwa wanachama
 
Umeandika upuuzi huu usitutie uoga kwanza itakuwa umetumwa na Ccm usafi tuachie wenyewe Cuf wewe km nani?
Uhai wa mtu ni muhimu zaidi ya Chama,kutumia nguvu kwa CUF halali kutawapelekea kuonekana kama nao ni sawa na CUF haramu. Ustaarabu na kuepusha shari kwa kutotaka wanachama wa CUF halali wawekwe ndani bila sababu ni muhimu zaidi.
Maalim Seif ni mstaarabu na amevumilia mengi kwa maana angekuwa muumini wa umwagaji damu hali ya Zanzibar ingekuwa mbaya sana lakini uvumilivu na kutafuta haki kwa amani ni suala zuri hasa pale mwenzio anapokuwa na ulinzi wa dola.
 
CUF wakimuendekeza LIpumba ndio kifo chao yeye anakula kwa kuku wa mrija sasa ni za uso kwa uso uone mwisho wake maana kesi mahakamani haitishwi sijui Jaji hajapangiwa what do you expect tungoje wafanye watakavyo eti kwa kuogopa kukatwa visigino basi twendeni tukakatane visigino
 
Kusafisha nyumba yako nako unangoja upangiwe na jambazi? Imetosha sasa, kundi LA wachache hawawezi kuwafanya wengi wajinga kwa muda mrefu. Lolote likitokea serikali ndio itabeba lawama hasa kwa kuwalinda majambazi hao kwa muda mrefu
 
Kwanza hawana ubavu huo. Kesho saa 11 wazee watatanda buguruni nzima
 
Kusafisha nyumba yako nako unangoja upangiwe na jambazi? Imetosha sasa, kundi LA wachache hawawezi kuwafanya wengi wajinga kwa muda mrefu. Lolote likitokea serikali ndio itabeba lawama hasa kwa kuwalinda majambazi hao kwa muda mrefu
Kwa hiyo na wewe utaenda?
 
Kama mwananchi, ninatoa wito wa dhati kutoka katika sakafu ya moyo wangu, tena bila hila yoyote ndani mwangu kwamba CUF halali msiende Buguruni Jumapili. Ninafahamu kwamba Lipumba si halali CUF kwa kuwa alishajivua uongozi, CUF ilisharidhia kujiuzulu kwake na alishavuliwa uanachama wa CUF. Hivyo amejipachika uongozi haramu wa CUF. Ikumbukwe kuwa CUF haramu inabebwa na serikali kwa kupitia Msajili wa Vyama vya siasa. Uvamizi walioufanya CUF haramu kwenye mkutano wa waandishi wa habari ulikuwa na support ya wenye dola. Vingenevyo, CUF haramu wangeshafurushwa Buguruni na kupelekwa kunakohusika- Lupango.

CUF halali wasidhani kwamba aliyekatwa kisigino na wabwana zake wamefurahi. Watakuwa wanatafuta muda muafaka wa ku-strike back. Usafi wa jumapili unaweza kuwa fursa ya CUF haramu na mabwana zao kujibu mapigo, ingawa wao ndio waliovamia kikao. Kwa usalama wa CUF halali, ninawaomba wafute mpango wao. Habari hii imufikie Mtatiro Julius ili awaarifu wanachama wa CUF kuhusu kuachana na usafi wa Jumapili. CUF halali waendelee kutumia njia za kidemokrasia na kisheria za kuwafurusha CUF haramu kwenye ofisi zao. Huu ndiyo ujumbe katika uzi huu, uzingatiwe na hatua zichukuliwe haraka ili kuwalinda wananchi dhidi ya uharamia wa CUF haramu na mabwana zao.

Wewe unaamini CUF halali kweli watakwenda kufanya usafi buguruni ?

Kwa maoni yangu CUF hawatakwenda lakini wamefanikiwa kuwavuwa nguo wale wote walio nyuma ya LIPUMBA.

Kumbuka serikali ilimlinda Lipumba alipovamia buguruni na polisi walikuwepo. Aliachwa mpaka leo yupo hakukuwa na visingizio vya kuvugwa amani. Leo hii polisi watanasa mtego huu. Kwa kisingizio cha amani hilo moja.

Pili, Serikali kama ina lengo la amani basi wamewashiwa taa ya kijani na CUF kutumia njia za kisheria kumuondowa Lipumba kabla hajaleta madhara, kumbuka kwa mujibu wa katiba ya CUf Lipumba si Mwenyewkiti tena wala si mwanachama, Kuikalia ofisi ya Chama na kufanya ubatili ule anaofanya ni kinyume cha sheria kwa nini serikali inamuacha pale kuhatarisha amani ?

Tatu kesi iliyoko mahakamani ni kuhusu uenyekiti wa lipumba, na kwamba matumizi ya Ofisi ya CUF si kwa ajili ya Lipumba pekee, sasa kama kuna viongozi wengine wa CUf akiwemo Katibu Mkuu wana haki ya kuitumia, sasa ikiwa Polisi itawazuiuya wengine wasende buguruni na kumuacha Lipumba kufanya hujuma itakuwa ni yale yale ya kuegemea upande wa Lipumba na huku ndiko kuvuka nguo wenyewe.

Nafikiri serikal ingekuwa katikati tokea awali, lakini walishachagua upande hili ndilo lina wacost.

CUF halali imeucheza mchezo kitaalamu. na unakaribia mwisho.
 
Back
Top Bottom