Ombi Maalum Kwako Rais Samia, Tuondolee Mgao Wa Umeme Wakati Huu wa Sikukuu za Mwisho Wa Mwaka

Mchanya

JF-Expert Member
Jul 29, 2015
976
1,525
Kwako Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan

Kwa Heshima na taadhima, na kwa unyenyekevu mkubwa, naleta ombi kwako wewe Mheshimiwa Rais, utusaidie kuondoa ukali ya mgao na ukosefu wa umeme angalau katika kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka. Baada ya kuteseka sana na mgao mkali wa umeme karibu mwaka mzima nadhani zawadi bora kabisa ya sikukuu unayoweza kuwapatia wananchi wako ni upatikanaji wa uhakika wa umeme angalau katika kipindi hiki sikukuu za Xmas na Mwaka mpya.
Wanachi wako wengi hawako kazini katika kipindi hiki, wengi pamoja na familia zao wako mapumzikoni hivyo ni muda mzuri kwa wao kuwa pamoja na familia zao wakifurahia mapumziko yao, lakini ukosefu wa umeme unawafanya wawe wanyonge, wawe na huzuni na wajikute wakiwa hawana kitu cha kufanya kutokana na kukosa umeme.

Ukosefu wa umeme umeanza kujenga chuki na hasira kutoka kwa wananchi dhidi ya serikali yao na hali hiyo huenda ikazidi kama hali ya umeme itaendelea kuwa hivi.

Mengi yameshasemwa kuhusu sababu, mikakati upembuzi yakinifu ya kuboresha umeme lakini kwa sasa watu hawataki kusikia maneno hayo tena, wamechoka wanachotaka ni umeme uwepo majumbani mwao

Nawasilisha.
 
Rais anao wajibu wa kuhakikisha nchi ina umeme wa uhakika, hivyo Mimi simuombi aondoe mgao, bali namfahamisha kuwa watanzania hawa wanaolipa Kodi kila siku wanadai huduma ya umeme.
 
Kwako Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan

Kwa Heshima na taadhima, na kwa unyenyekevu mkubwa, naleta ombi kwako wewe Mheshimiwa Rais, utusaidie kuondoa ukali ya mgao na ukosefu wa umeme angalau katika kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka. Baada ya kuteseka sana na mgao mkali wa umeme karibu mwaka mzima nadhani zawadi bora kabisa ya sikukuu unayoweza kuwapatia wananchi wako ni upatikanaji wa uhakika wa umeme angalau katika kipindi hiki sikukuu za Xmas na Mwaka mpya.
Wanachi wako wengi hawako kazini katika kipindi hiki, wengi pamoja na familia zao wako mapumzikoni hivyo ni muda mzuri kwa wao kuwa pamoja na familia zao wakifurahia mapumziko yao, lakini ukosefu wa umeme unawafanya wawe wanyonge, wawe na huzuni na wajikute wakiwa hawana kitu cha kufanya kutokana na kukosa umeme.

Ukosefu wa umeme umeanza kujenga chuki na hasira kutoka kwa wananchi dhidi ya serikali yao na hali hiyo huenda ikazidi kama hali ya umeme itaendelea kuwa hivi.

Mengi yameshasemwa kuhusu sababu, mikakati upembuzi yakinifu ya kuboresha umeme lakini kwa sasa watu hawataki kusikia maneno hayo tena, wamechoka wanachotaka ni umeme uwepo majumbani mwao

Nawasilisha.
Acha uchawa wewe, tunajua maofisi mengi na sehemu nyingi za kazi watu watapumzika hivyo umeme utapatikana majumbani. Unataka kuwaaminisha maccm kwamba samia ana umeme atawasha siku za sikukuu?
Acha ujinga.
 
Acha uchawa wewe, tunajua maofisi mengi na sehemu nyingi za kazi watu watapumzika hivyo umeme utapatikana majumbani. Unataka kuwaaminisha maccm kwamba samia ana umeme atawasha siku za sikukuu?
Acha ujinga.
Hivi huwezi kutoa maoni yako bila kumwita mtu 'mjinga' au 'chawa'?! Hili ni jukwaa huru huna haja ya kutusi watu.
 
Back
Top Bottom