Ombi maalum kwa Dr.Asha-Rose Migiro

Ombi maalum kwa Dr.Asha-Rose Migiro

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,143
Kwanza,nimpongeze Dr.Asha-Rose Migiro kwa uteuzi wake wa kuwa Waziri mpya wa Katiba na Sheria.Baada ya kuapishwa kesho,Dr.Migiro atachukua nafasi ya Waziri Mathias Chikawe ambaye anahamia Wizara ya Mambo ya Ndani. Mhe.Migiro,nikiri hapa,kwamba ombi langu ni la 'kibinafsi' sana. Ni kuhusu Mahakama ya Mwanzo,Mailimoja Kibaha Pwani.

Mahakama hii ni kongwe na chakavu sana. Inahitaji ukarabati.Kwa jinsi inavyohitajika katika kutoa haki kwa Wilaya nzima ya Kibaha,ni vyema ikakarabatiwa. Iko Mailimoja usoni kabisa mwa Mji wa Kibaha.

Dr.Migiro,hongera na nikuombe upokee ombi langu
 
Nilidhani mahama ya kadhi

Kama nihiyo ondoa shaka
 
Ninalo swali kwa Dkt. A. R. Migiro.
Ndani ya CCM, moja ya shughuli anazozisimamia ni kuwaambia wanachama wa CCM kupinga MUUNDO WA SERIKALI TATU.
Sasa ni Waziri wa Katiba.
Je, ataendeleza jitihada hizo kama Waziri?
Dkt. A. Migiro, utaungana na nguli wenzako wa sheria au utajitenga nao hivyo uonekane kumdhihaki
msomi mwenzako Dkt. Edmund Sengondo Mvungi?
 
Kwanza,nimpongeze Dr.Asha-Rose Migiro kwa uteuzi wake wa kuwa Waziri mpya wa Katiba na Sheria.Baada ya kuapishwa kesho,Dr.Migiro atachukua nafasi ya Waziri Mathias Chikawe ambaye anahamia Wizara ya Mambo ya Ndani. Mhe.Migiro,nikiri hapa,kwamba ombi langu ni la 'kibinafsi' sana. Ni kuhusu Mahakama ya Mwanzo,Mailimoja Kibaha Pwani.

Mahakama hii ni kongwe na chakavu sana. Inahitaji ukarabati.Kwa jinsi inavyohitajika katika kutoa haki kwa Wilaya nzima ya Kibaha,ni vyema ikakarabatiwa. Iko Mailimoja usoni kabisa mwa Mji wa Kibaha.

Dr.Migiro,hongera na nikuombe upokee ombi langu

Mahakama za mwanzo (hata za Wilaya) nyingi zina hali mbaya sana. Tembelea huko mikoani ujionee mwenyewe. Unaweza kulia kabisa!!
 
Sehemu waliyompa huyu mama ndio watazidi onesha jamii kuwa ni kimeo,afadhali angepewa wizara mfu kama ya Simba sophia,huku sasa hivi mapungufu ya UN tutayaona
 
Binafsi nakushauri kwa kuwa umeteuriwa kuwa Waziri wa sheria na katiba na hivi ninavyo andika hapa tupo katika harakati za kuanza rasimi kwa bunge la katiba,chonde chonde tunahitaji Serikali yetu ya Tanganyika kama wenzetu wa Zanzibar walivyo jirejeshea Serikali yao ya Zanzibar na hivyo kuhalarisha kuvunja muungano,maana hayumukiniki ukapata serikali kamili inayoitwa Zanzibar kisha ujidanganye kuwa kuna muungano! pengine mtu huyo hajui historia ya kuzaliwa NENO TANZANIA Kuwa ni mjumuiko wa TAN......GANYIKA na ZAN......ZIBAR Kisha ile nia iliyowaleta pamoja nayo ni NIA.=IA

Sasa tujumlishe au tuunganishe TAN+ZAN+IA= TANZANIA Huu ndiyo ulikuwa muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Nje ya hapa hapajawahi tokea nchi huru inayoitwa Tanzania,bali kuna nchi huru na iliyojipatia Uhuru 9-12-1961 Nchi hiyo inajulikana kama Tanganyika hivyo basi kwa kuwa wenzetu wa visiwani wamerejesha Nchi yao huru ya zanzibar,ni kazi yako sasa kama Waziri mwenye dhamana na Katiba kuhakikisha unatupatia Serikali TATU [3]Na siyo vinginevyo. Karibu Ofisini Mama.:hand:
 
Wamempa wizara hiyo kwa kujua atapambana vyema na akina Tundu Lisu na wengineo huko Chadema pale Bungeni.. Inafaa aende tu achape kazi vinginevyo atakuwa Bi Kiroboto namba 2 na kudhihirisha kabia maoni ya wengi huko ng'ambo kwamba Ba ki Moon Alimtema kwa ku under perfoming .
 
Mimi najiuluza maswali mengi bila kupata majibu. Inasemekana CCM Zanzibar wanajiandaa kupinga serikari tatu, lakini walishupalia kupata serikali yao ya Zanzibar. Kitugani hasa kinawafanya watuzuie watanganyika tusipate serikali yetu? Swali la kwamza kwa Asha roze
 
Mahakama za mwanzo (hata za Wilaya) nyingi zina hali mbaya sana. Tembelea huko mikoani ujionee mwenyewe. Unaweza kulia kabisa!!
Ni kweli Mkuu.Kuna haja ya kufanyika ukarabati wa hali ya juu ili haki itendeke katika mazingira mazuri
 
Tatizo sio hilo la Mahakama ya Mwanzo,Mailimoja Kibaha Pwani tu. Mtu unapotembelea Ma wilayani tena vijijini huko ndio utajua nasema nini. Mahakama zni choka mbaya sana na vyoo ndio hata usiseme.

Kwa
sababu jengo ni choka mbaya pale meza kuu hakimu anapoendeshea kesi basi unaweza hata kumrushia /ponda na jiwe ukiwa nje barabarani na halafu ukakimbia zako na wasikupate. Hivyo usalama wa hakimu na wafanyakazi wa mahakama uko mashakani saa zote kusema unaishi nchi ya Taliban.


 

Similar Discussions

Back
Top Bottom