Ombi letu kwa wabunge wote wa bunge la tanzania

JATELO1

JF-Expert Member
Oct 31, 2011
1,230
301
JAMANI WABUNGE WA TZ;
Kwa niaba ya Watanzania na hatima ya nchi yetu kwa vizazi vya sasa na vijavyo, TUNAWAOMBENI SANA huo muswada wa KATIBA MPYA msikubali isomwe kwa mara ya pili na kupitishwa na Bunge letu. Hili ombi halijali wewe ni Mbunge kutoka Chama gani cha Siasa, isipokuwa ni kwa wabunge wote bila kujali imani yako, rangi yako, kabila yako, kanda yako, Jinsia yako, una miaka mingapi Bungeni, au una itikadi gani ya kisiasa. Ni kwa Wabunge wote wa Bunge la Tanzania. Ni hakika Watanzania mnaowawakilisha huko wanawaombeni sana msikubali kupitisha huo muswada. Ndugu zetu Wabunge, japokuwa twajua kwamba kuna tofauti kati yenu ktk masuala mengine, lkn katika hili tunawaomba kwa dhat kabisa mshirikiane ili kuweza kuepusha hatari inayoweza kutokea iwapo hiyo rasimu itasomwa kwa mara ya pili na kupitishwa.

Wabunge wetu ndiyo mmebaki kuwa tumaini letu pekee ktk hili na Serikali yetu imetusahau kabisa, kwani angalieni jinsi wanavyochezea mambo ya msingi yenye hatima ya Taifa letu kwa kisingio cha Utandawazi na Soko Huria. Angalieni rasilimali zetu zinavyotoroshwa kwenda nje huku tukiachiwa mashimo hasa za madini wkt mali yote inakwenda nje na hata hizo pesa hazirudi kwenye Uchumi wetu, japo kwenye RECORD Zetu inaonyesha kwamba Export za Madini zinaongezeka mwaka hadi mwaka.

Spika wa Bunge, Mh. Anne Makinda; wananchi wamehoji mambo mengi sana kuhusu utendaji wako; tafadhali sana ktk hili tunaomba uwe upande wa Wananchi na si upande wa Serikali; kwani Bunge ni chombo huru na ndiyo yenye wawakilishi wa wananchi waliowapigia Kura. Tafadhali sana Mama saidia ktk hili.

Katibu wa Wabunge wa CCM; Mimi nikiwa mwanachama mwaminifu wa CCM, ninakuomba sana ktk hili la KATIBA, tafadhali wabunge wetu wa CCM ambao ndiyo wengi Bungeni, wasiitwe kabisa Chemba ili kupewa maagizo. Tunakuomba sana Katibu.

Mwisho natoa pendekezo kwa Wabunge; Tafadhali takeni kwenye mchakato wa kuandaa KATIBA MPYA; ndg. Fredrick Werema-Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Celina Kombani-Waziri wa Sheria na Katiba; wasihusishwe kwani tayari walishautangazia umma wa watanzania kwamba HAWAONI UMUHIMU WA KATIBA MPYA.

WanaJF; tafadhali wekeni maoni yenu kuhusiana na suala hili nyeti la KATIBA MPAYA.

Waberoya tunaomba mchango wako hapa pia.




Spika wa
 
HESHIMA MBELE WAKUU.

Kwanza inashangaza kwa Wabunge wetu kukubali muswaada huo kuletwa mbele yao na watu waliokataa kata kata kwamba hakuna umuhimu wa katiba mpya mbele ya rais. Kwa maana nyingine ni kwamba Muswaada huo umeletwa mbele ya bunge kama changa la macho baada ya kuwepo mgandamizo mkubwa kutoka kwa waTanzania. Pia Katiba Mpya haikuwa agenda ya Chama cha Ma-Used (CCM). Waziri Kombani ni zao la CCM, AG naye ndio kabisa. Kwani hulka na mambo anayo yafanya hayalingani na taaluma yake ya sheria. Zaidi ni kutekeleza ya ki- CCM.

WaTanzania tujiandae kuingia barabarani kwani kwa wabunge wa-CCM tusitarajie kilicho kwa maslahi ya waTanzania. Tuamue sasa kuingia barabarani na kupinga waziwazi ukandamizaji huu ulio kithiri. Kumekuwa na genge la watu wanaojiona ndiyo wenye haki ya kufaidi rasilimali za waTanzania peke yao. Tufikie mahala tuseme sasa IMETOSHA.

"HAKI HAIJI KAMA MANA" (Dr. W. Slaa, Uwanja wa NMC Arusha).
 
Muda ndio huu...Hatulali mpaka kieleweke KATIBA MPYA tunaihitaji ambayo itasaidia mabadiliko ya nchi yetu
 
Nimesikia na tetemeka baada ya kusoma maombi haya kwa washika mpini waliopo Bungeni. Kwa uwazi kabisa hatima ya Taifa hili na damu za wanyonge wanaokosa kuishi kwa raha ndani ya nchi yao kwa nafasi waliyopewa na Mwenyezi Mungu ipo mikononi mwao hapo kesho_Ole wa yule atakaeendekeza ushabiki wa kichama na kimaslahi na kuweka uzalendo na umma wa wananchi wezake nyuma.Damu itakayokuwa shidani na kupotea itakuwa juu yake yeye na familia yake.NAWAKILISHA.Ngoja nikanywe maji kwanza..
 
Tunahitaji katiba mpya haraka sana.Tunawataka wapinzani wasiwe kikwazo cha watz kukosa fursa hiyo ya kupata katiba.Maandamano na vurugu bila hoja za msingi ati kwanini kikwete anashirikishwa sana ni hoja mfu na ya kibaguzi.kuweka mchakato wa katiba mikononi mwa jukwa la katiba ni kuuweka mikononi mwa wakoloni maana wao ndio wanaowafadhili.Watu hawa wanatumika na wafadhili wao.tuwe macho watz.
 
Ndugu yangu twahil;
Naona unaleta utani na ushabiki hata katika mambo ya msingi yatakayoamua hatima ya hata yule bibi wa kule kijijini Nkasi. Ushauri wangu kwako ni kwamba; SI LAZIMA UJIBU KILA HOJA HAPA JUKWAANI. Siyo dhambi ukisoma na kuendelea na mambo yako bila kuleta utani wa HATARI kama huo katika mambo ya Msingi kama ya Katiba ya Tanzania.
 
Ole wao waipitishe kwa sababu wamepewa ganji na hao mafisadi,kitakachokuja kutokea baada ya hapo itabidi tutafutane mtaa kwa mtaa nyumba kwa nyumba kitongoji kwa kitongoji,nimeisha choka na manyanyaso wanayotupa hawa mafisadi vilaza.
 
Tunahitaji katiba mpya haraka sana.Tunawataka wapinzani wasiwe kikwazo cha watz kukosa fursa hiyo ya kupata katiba.Maandamano na vurugu bila hoja za msingi ati kwanini kikwete anashirikishwa sana ni hoja mfu na ya kibaguzi.kuweka mchakato wa katiba mikononi mwa jukwa la katiba ni kuuweka mikononi mwa wakoloni maana wao ndio wanaowafadhili.Watu hawa wanatumika na wafadhili wao.tuwe macho watz.

Kuna jamaa ananiuma sikio kwamba uliwahi kuumwa na kenge kijijini ukioga mtoni so yote usemayo ni kutoka na kuumwa huko una kichaa cha kenge je ni kweli ? Maana si kawaida uje na hoja kinyesi hivi.
 
Kuna jamaa ananiuma sikio kwamba uliwahi kuumwa na kenge kijijini ukioga mtoni so yote usemayo ni kutoka na kuumwa huko una kichaa cha kenge je ni kweli ? Maana si kawaida uje na hoja kinyesi hivi.

tatizo la huyu jamaa ni kuweweseka na ccm yake juu ya cdm, na ndio maana hawezi kutofautisha masuala ya kitaifa na siasa, ukimwambia unawaza kwa kutumia makalio anaona kama vile hujamtendea haki
 
Tunahitaji katiba mpya haraka sana.Tunawataka wapinzani wasiwe kikwazo cha watz kukosa fursa hiyo ya kupata katiba.Maandamano na vurugu bila hoja za msingi ati kwanini kikwete anashirikishwa sana ni hoja mfu na ya kibaguzi.kuweka mchakato wa katiba mikononi mwa jukwa la katiba ni kuuweka mikononi mwa wakoloni maana wao ndio wanaowafadhili.Watu hawa wanatumika na wafadhili wao.tuwe macho watz.
Ondoka na usengenyaji wako hapa.
 
Natabiri wabunge wengi wa ccm kuchangia kwa njia ya maandishi ama sivyo Tv zitazimwa ama la Symbion wataondoa megawat zao
 
HESHIMA MBELE WAKUU.

Kwanza inashangaza kwa Wabunge wetu kukubali muswaada huo kuletwa mbele yao na watu waliokataa kata kata kwamba hakuna umuhimu wa katiba mpya mbele ya rais. Kwa maana nyingine ni kwamba Muswaada huo umeletwa mbele ya bunge kama changa la macho baada ya kuwepo mgandamizo mkubwa kutoka kwa waTanzania. Pia Katiba Mpya haikuwa agenda ya Chama cha Ma-Used (CCM). Waziri Kombani ni zao la CCM, AG naye ndio kabisa. Kwani hulka na mambo anayo yafanya hayalingani na taaluma yake ya sheria. Zaidi ni kutekeleza ya ki- CCM.

WaTanzania tujiandae kuingia barabarani kwani kwa wabunge wa-CCM tusitarajie kilicho kwa maslahi ya waTanzania. Tuamue sasa kuingia barabarani na kupinga waziwazi ukandamizaji huu ulio kithiri. Kumekuwa na genge la watu wanaojiona ndiyo wenye haki ya kufaidi rasilimali za waTanzania peke yao. Tufikie mahala tuseme sasa IMETOSHA.

"HAKI HAIJI KAMA MANA" (Dr. W. Slaa, Uwanja wa NMC Arusha).
...................dr slaa yupi?????? ni yule yule aliyepora mke wa mtu????ni yule yule alieanguka bafuni wakati anapiga nyeto?????achana na mawazo ya kutaka upewe bure wewe,au nawe sio riziki nini.
 
Back
Top Bottom