Ombi langu kwa watawala

Ombi langu kwa watawala

Ed n Edd nEddy

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2011
Posts
5,345
Reaction score
6,078
Nimepitia mabandiko mengi humu pia twitter hasa yanayohusu vifo au ajali zinaonesha zaidi chuki iliyojengeka baina wananchi kwa wananchi, watawala na wananchi.

Ukipitia bandiko la kifo/ajali utaona watu wanavyotupiana lawama kwa maneno ya kejeli na kusahau utu baina yetu. Watu hufika mbali sana hata kuhukumu wao wenyewe, kwenye ajali utaona wengine waki-comment kuhusu mtu huyo kama tayari ashafariki ama vipi? Na kukuta pole za kumtakia majeruhi kupona zikiwa chache.

Naichukia siasa sababu imeanza kutujengea matabaka ya wazi kabisa. Kwa sasa tuna taifa ambalo watu wake ndani wame-hold grudge kwanini tufike huku?

Wale tuliowapa mamlaka ya kutuongoza kwanini muwe chanzo cha visasi baina yetu na nyie?.


Alfred Nobel ali-invent dynamite,
gelignite, ballistite. Ambazo zilikuwa na madhara ya moja kwa moja kwa binadamu. Mwaka 1888 Ludvig Nobel (kaka ake Alfred) alifariki, magazeti yakadhani ni Alfred ndiyo amefariki yakachapisha 'The merchant of death is dead'. Alfred akaona jinsi watu wanavyo na watakavyo mchukulia baada ya kifo chake, akaanzisha Nobel prize na kubadilisha mitazamo ya watu mpaka Leo.

Kumbukeni cheo ni dhamana mjitahidi ku-build a better legacy. Shaurikeni na mbadilike.

Make a better place for you and for me.

Save Tanzania
 
Uzi wako Utapata wachangiaji Mkuu ungeandika Mange kimambi ashauri ungeona kundi la Malofa wakicomment hapa
 
Back
Top Bottom